Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Marwa Ryoba Chacha

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. MARWA R. CHACHA Aliuliza:- Wilaya ya Serengeti ina Mbuga ya Wanyama ya Serengeti inayovutia watalii wengi duniani lakini inakabiliwa na uhaba wa maji. Je, ni lini ujenzi wa chujio na usambazaji wa maji kutoka Bwawa la Manchira kwenda Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mugumu na vijiji vya jirani utakamilika?

Supplementary Question 1

MHE. MARWA R. CHACHA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Kwanza swali langu limejibiwa nusu, mimi nimeuliza ni lini ujenzi wa chujio na usambazaji wa maji utakamilika? Kwa hiyo, yeye amejibu upande mmoja wa ujenzi wa chujio, hajajibu upande wa usambazaji wa maji. Na ujenzi wa chujio hili unasimamiwa moja kwa moja na Wizara ya Maji pengine ndiyo maana Mheshimiwa Naibu Waziri hana picha halisi.
Mheshimiwa Naibu Spika, sasa nina maswali mawili ya nyongeza; la kwanza ni kuhusu usambazaji wa maji katika Mji wa Mugumu baada ya kukamilika kwa ujenzi wa chujio hili. Nataka kumuuliza Naibu Waziri, bahati nzuri ulikuja mwaka jana pale Jimbo la Serengeti pale Mugumu na uliyaona yale maji, ninataka kujua kama kata zote za Mamlaka ya Mji mdogo wa Mugumu, kata saba Kata ya Morotonga, Kata
ya Mugumu, Kata ya Stendi Kuu, Kata ya Getaisamo, Kata ya Kisangura kama zote zitapata maji, pamoja na vijiji vinavyozunguka lile bwawa, Kijiji cha Miseke, Kijiji cha Rwamchanga na Kijiji cha Bwitengi. Hilo ni swali la kwanza, ningependa kujua kwamba wakati wa usambazaji wa maji
haya maeneo yote yatapata?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; huyu mkandarasi ambaye anajenga chujio hili (PET) anadai sasa hivi ana certificate ambayo iko Wizarani ya zaidi ya milioni 200 na kimsingi mradi ule unasuasua pengine kwa sababu hana fedha. Je, Wizara iko tayari kumlipa certificate anayodai ili aendelee na hii kazi mradi ukamilike haraka huo mwezi wa sita?

Name

Eng. Gerson Hosea Lwenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza kabisa hii awamu tulianza kujenga chujio ili kuongeza uzalishaji wa maji ifikie lita milioni tano kwa siku, ambazo zinatosha kwa wakazi kwa sasa kwa wale wa mjini, lakini Serikali kwa kutumia mkopo wa dola milioni 500 tumetenga milioni nane US dollars ambazo ni sawasawa na shilingi bilioni 19 kwa ajili ya kuboresha usambazaji katika maeneo ya vitongoji vya Mji wa Mugumu. Kwa hiyo, naomba Mheshimiwa Mbunge asiwe na shaka, tatizo la kupata maji ya uhakika kwa Mji wa Mugumu na vitongoji vyake linashughulikiwa na Serikali.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lake la pili kuhusu madai ya mkandarasi; madai hayo tutamlipa mara tu baada ya kupata hizo certificates, hakuna shaka ya fedha, fedha tunazo.

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARWA R. CHACHA Aliuliza:- Wilaya ya Serengeti ina Mbuga ya Wanyama ya Serengeti inayovutia watalii wengi duniani lakini inakabiliwa na uhaba wa maji. Je, ni lini ujenzi wa chujio na usambazaji wa maji kutoka Bwawa la Manchira kwenda Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mugumu na vijiji vya jirani utakamilika?

Supplementary Question 2

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi niulize swali dogo la nyongeza. Kama ambavyo Wilaya ya Serengeti inazungukwa na mbuga ya wanyama, vivyo hivyo Wilaya ya Ngorongoro ina changamoto kubwa sana ya kijiografia kutoka tarafa moja kwenda tarafa nyingine ni kilometa nyingi ikiwemo kutoka Tarafa ya Ngorongoro kwenda Tarafa ya Loliondo ambapo kuna takribani kilometa mia na zaidi, na Mheshimiwa Naibu Waziri ulifika umejionea mazingira ya Ngorongoro. Je, Serikali iko tayari sasa, kulingana na ugumu wa jiografia ya Ngorongoro, kuhakikisha upatikanaji wa maji safi na salama kwa wakazi hao inapatikana?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli nilifika Ngorongoro takribani wiki tatu na nusu zilizopita, na ni kweli jiografia ukitoka hapa Karatu wakati unatoka getini pale
mpaka unafika kule Loliondo ni mbali sana na sio hivyo tu, nilifanya jiografia pana sana nikazunguka lile Jimbo la Ngorongoro nikapita mpaka katika Ziwa Natron pale, kweli changamoto ya maji ni kubwa na kama nilivyokuwa kule site niliahidi kwa wananchi kwamba tutafanya kila liwezekanalo kushirikiana na Halmashauri ile ya Ngorongoro kuangalia jinsi gani tutafanya kuhakikisha kwamba tunapata ujenzi wa maji kule kama ni borehole au vyovyote.
Kwa mfano ile Shule ya Sekondari ya Ziwa Natron pale, watoto wako pale lakini na maji yapo pale ila isipokuwa jinsi gani kuyasambaza kufika shuleni. Kwa hiyo, vyote nimeenda kule nimeweza kufanya needs assessment ya eneo lile na naomba nikuhakikishie kwamba kama Serikali na matakwa
yetu ya Kiserikali tutafanya kila liwezekanalo kuwasaidia wananchi wa Ngorongoro.

Name

Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. MARWA R. CHACHA Aliuliza:- Wilaya ya Serengeti ina Mbuga ya Wanyama ya Serengeti inayovutia watalii wengi duniani lakini inakabiliwa na uhaba wa maji. Je, ni lini ujenzi wa chujio na usambazaji wa maji kutoka Bwawa la Manchira kwenda Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mugumu na vijiji vya jirani utakamilika?

Supplementary Question 3

MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwanza naomba nimpongeze Naibu Waziri, alipotembelea Wilaya ya Korogwe aliweza kuona hali halisi ya tatizo la maji lililopo katika mji wetu wa Korogwe. Hata hivyo aliahidi kutuletea shilingi bilioni mbili ili angalau tatizo la maji lile liweze kuondoka pale, swali; kwa kuwa
wameshatuletea milioni 500 kwa ajili ya kutoa maji kutoka kwenye Mto Ruvu, je, sasa Serikali zile fedha wameshaziingiza kwenye bajeti ili kusudi ziweze kutusaidia katika kutengeneza miundombinu ile ambayo ni mibovu maana yake
tutakapokuwa tumejenga matenki au tumejenga ule mkondo wa maji bila ya kuwa na matenki ya maji makubwa bado tatizo la maji litakuwa lipo pale Korogwe. Je hizi fedha shilingi bilioni mbili alizosema zimetengwa katika bajeti hii? Nashukuru.

Name

Eng. Gerson Hosea Lwenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

WAZIRI WA MAJI NA UMWAGILIAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli tulitenga shilingi bilioni mbili kwa ajili ya kuboresha maji katika Mji wa Korogwe na tulitoa maelekezo kwamba usanifu ukikamilika tunatangaza tender kwa hiyo ikishatangazwa tender na wakianza kufanya kazi tutakuwa tunalipa kwa certificate jinsi zinavyokuja. Kwa hiyo, naomba nimuondoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge kwamba mradi ule utatekelezwa na fedha zipo kwenye bajeti. Ahsante sana.

Name

Peter Ambrose Lijualikali

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. MARWA R. CHACHA Aliuliza:- Wilaya ya Serengeti ina Mbuga ya Wanyama ya Serengeti inayovutia watalii wengi duniani lakini inakabiliwa na uhaba wa maji. Je, ni lini ujenzi wa chujio na usambazaji wa maji kutoka Bwawa la Manchira kwenda Mamlaka ya Mji Mdogo wa Mugumu na vijiji vya jirani utakamilika?

Supplementary Question 4

MHE. PETER A. LIJUALIKALI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru.
Suala hili la maji kwenye Kijiji changu na Kata ya
Zinginari kuna mradi wa maji ambao unagharimu shilingi milioni 400 umefanywa, muda umeisha lakini mpaka leo maji hayatoki, kimekuwa ni kilio kikubwa sana.
Je, Waziri anafahamu kwamba kuna hii shida na
kama afahamu atakuwa tayari kwenda na mimi kwenye Jimbo langu ili ashuhudie namna ambavyo shilingi milioni 400 hizi zimeliwa na maji hakuna? Nashukuru.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, tuna kesi mbalimbali na kuna baadhi ya maeneo mengine kwamba miradi imetekelezwa lakini wakati mwingine maji hayajapatikana na hii ina maana kwamba inatofautiana kutokana na mazingira. Mengine ni suala zima wakati mwingine zimechimbwa borehole ambapo zile borehole wakati mwingine zinakosa maji, lakini sehemu zingine ni suala
zima la usimamizi na uzembe katika usimamizi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo kwa kulijua kwa kuona jambo hilo kwasababu ni maeneo ya Kilombero peke yake ambayo nilikuwa bado sijafika katika Mkoa wa Morogoro na ni imani yangu hata katika Bunge hili la Bajeti nitafika kule Kilombero. Basi naomba nikifika kule tuweze
kuangalia jinsi gani tatizo lililoko pale halafu tulipatie tiba halisia kutokana na jinsi tutakavyoliona lengo kubwa ni kwamba Wananchi wa eneo lako waweze kupata huduma ya maji.