Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE Aliuliza:- Wilaya ya Mlele haina Hospitali ya Wilaya. Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali ya Wilaya ya Mlele?

Supplementary Question 1

MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Mlele tayari
imeshatimiza masharti yote ya kujenga maabara, ya kujenga mfumo wa maji safi na taka pamoja na matundu nane ya vyoo; na kwa kuwa wananchi wa Wilaya ya Mlele hususan akina mama wa Tarafa ya Inyonga wanapata shida sana kwa ajili ya matibabu yao kwa sababu kile ni kuwa kituo cha afya lakini Halmashauri yao imefanya juhudi kubwa kwa matengenezo yote waliyoweka vigezo Serikali. Je, ni lini sasa Serikali itatoa kibali ili kile kituo cha afya kiweze kuwa Hospitali ya Wilaya?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, kwa kuwa yale maeneo ambayo yanajengwa majengo mengine wananchi hawajalipwa fidia zao, wanadai sasa muda mrefu hawajalipwa, ni lini Serikali itawalipa pesa zao ili wananchi wa Wilaya ya Mlele hususan Tarafa ya Inyonga waweze kupata pesa zao?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli na mimi nakumbuka nilitembelea katika Mkoa wetu wa Katavi na
miongoni mwa hospitali nilizokwenda kutembelea ni hiki Kituo cha Afya lakini kipindi kile kilikuwa kinakabiliwa na changamoto kubwa sana ya maji na nilitoa maelekezo pale na nimshukuru sana Mbunge wa Jimbo pale amefanya harakati imepatikana fedha hivi sasa mfumo wa maji
umepatikana. Na bahati nzuri hospitali hii kwa watu wasiofahamu ni kwamba ni kweli miundombinu yote imekamilika, na siku ile nilitoa maelekezo kwa Mganga Mkuu wa Mkoa wa Katavi kwamba sasa kwa sababu eneo lile ndiyo
eneo la kimkakati na Makao Makuu ya Wilaya ya Mlele yako pale Iyonga, nikasema kwa sababu vipaumbele vyote vinavyotakiwa na mahitaji yote yameshakamilika basi waanze mchakato kuhakikisha eneo lile sasa linakuwa rasmi, kituo kile kinakuwa rasmi kuwa Hospitali ya Wilaya ilimradi waweze kukidhi vile viwango vya upataji bajeti inayolingana na hospitali ya Wilaya.
Kwa hiyo, Mheshimiwa Anna Lupembe naomba
nikuhakikishie kwamba haya yalikuwa maelekezo yangu nilipokuwa kule site kutokana na mahitaji ya maeneo hayo yalivyo.
Mheshimiwa Naibu Spika, lakini suala zima la wakazi waliokuwa pale; ni kweli, ukiangalia kwamba kuna nyumba nyingi sana zimejengwa katika maeneo yale na bahati mbaya sana kuna watu wanaotaka fidia pale na nilitoa maelekezo katika Halmashauri yetu sasa ipange mkakati jinsi
gani wale watu wataweza kulipwa fidia. Kwa sababu eneo lile likishakuwa hospitali ya wilaya lazima tuwe na eneo la kutosha kwamba wananchi katika eneo lile na hospitali ile iwe na hadhi kwamba maeneo yale sio kuingiliwa na watu na nina imani kwamba katika vipaumbele vya bajeti ya Halmashauri mwaka huu itakuwa imetengwa hiyo. Lengo kubwa ni kuifanya hospitali ile sasa iwe rasmi kuwa Hospitali ya Wilaya.

Name

Dr. Godwin Oloyce Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Siha

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE Aliuliza:- Wilaya ya Mlele haina Hospitali ya Wilaya. Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali ya Wilaya ya Mlele?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. GODWIN O. MOLLEL: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Hospitali ya Wilaya ya Siha inafanana sana na Wilaya ambayo imetangulia kuulizwa hapa, na Mheshimiwa Waziri aliitembelea Hospitali yetu ya Wilaya ya Siha na ameona kwamba tuna wagonjwa wa nje tu, hatulazi lakini juhudi zinaendelea na hata wiki hii wananchi wamejitolea kuchimba msingi kwa ajili ya kuendeleza hospitali yetu na changamoto kubwa tuliyonayo ni watumishi, hospitali yetu haina watumishi na hata tukifikia mahali pa kulaza na kuweza kufanya operation na huduma nyingine
hatutakuwa na watumishi na madaktari.
Je, anatuambia nini kwa sababu ndani ya mwaka
huu tutaanza kulaza na kufanya operation, je, ni mkakati gani wa dharura utafanyika ili hospitali hiyo iweze kupata watumishi wa kutosha na kazi ianze?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli nilifika pale Siha na nilivyofika pale licha ya hilo suala la watumishi
lakini nilitoa maagizo. Serikali tumepeleka fedha pale kwa ajili ya kuhakikisha tunamaliza miundombinu katika ile floor ya juu, lakini nilitoa maagizo kwa sababu matumizi ya fedha zile, vikao vilivyokaa kwamba inaonkana fedha zile zilikuwa zinakwenda kutumika isivyo halali. Imani yangu ni kwamba katika eneo la Siha, utawala wa Siha utakuwa umefanya utaratibu mzuri jinsi gani tunaenda kupata value for money jengo lile linakamilika wananchi waweze kupata huduma.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika suala zima la
watumishi sasa, Serikali inasema sio Siha peke yake, isipokuwa katika maeneo yote tuna changamoto sana ya watumishi na hasa katika suala zima la uhakiki tulivyopeleka hivi sasa
kuna watu wengine walikimbia vituo. Kwa hiyo, imani yangu ni kwamba kwa sababu tuna mchakato hivi sasa wa suala zima la ajira nadhani Wizara ya Utumishi itakapokuwa tayari basi kibali kitatoka kuhakikisha kwamba tunapata waajiriwa mbalimbali katika sekta mbalimbali hasa ikiwa sekta ya afya na watakuja kule Siha kuwahudumia wananchi wa Siha.

Name

Suleiman Ahmed Saddiq

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mvomero

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE Aliuliza:- Wilaya ya Mlele haina Hospitali ya Wilaya. Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali ya Wilaya ya Mlele?

Supplementary Question 3

MHE. SULEIMAN A. SADDIQ: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi, naomba kuuliza swali moja dogo la nyongeza.
Kwa kuwa suala la Wilaya ya Mlele linafanana kabisa na suala la Wilaya ya Mvomero na kwa kuwa Wilaya ya Mvomero tayari tumeshajenga Hospitali ya Wilaya ambayo imekamilika kwa asilimia 80 na kwa kuwa kuna fedha ambazo
tunazisubiri kutoka Serikalini ili tukamilishe na wananchi waanze kupata huduma; je, Serikali iko tayari kukamilisha ahadi yake ya kuleta zile fedha na hospitali ile iweze kufunguliwa?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, naam, Serikali iko tayari na ndiyo maana katika kipindi cha sasa katika sekta
ya afya tumekuwa tukipelekeza pesa nyingi sana katika eneo hilo, na ndiyo maana naomba nikuhakikishie sio suala zima la miundombinu hata katika suala zima la madawa tumefanya kazi kubwa sana. Kwa hiyo, Mheshimiwa Murad naomba tukitoka hapa tuwasiliane tuangalie jinsi gani katika bajeti yenu ya mwaka huu kipi kimetengwa kwa ajili ya ujenzi wa hospitali hiyo
kuweza kumalizia, lakini jinsi gani tufanye tuweze kusukuma kwamba katika bajeti ya mwaka huu ambayo imetengwa tusukume ilimradi fedha zipatikane suala la ujenzi likamilike ilimradi wananchi wa Mvomero waweze kupata huduma ya afya kama inavyotarajiwa.

Name

Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE. ANNA R. LUPEMBE Aliuliza:- Wilaya ya Mlele haina Hospitali ya Wilaya. Je, ni lini Serikali itajenga Hospitali ya Wilaya ya Mlele?

Supplementary Question 4

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Na mimi naomba niulize swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa tatizo la Mlele linafanana sana na tatizo la Tabora Manispaa, Uyui pamoja na Kaliua, je, Serikali inasema nini kuhusu kukamilisha au kuandaa mpango wa kukamilisha hospitali ambazo hazipo?

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli, Serikali kama tulivyosema kipaumbele chake ni kuhakikisha huduma ya afya inapatikana na ndiyo maana siwezi ku-disclose
information zote, lakini kuna juhudi kubwa sana inafanyika lakini kiukweli ni kwamba kama nilivyosema katika jibu langu la msingi, kwanza kipaumbele cha kwanza kinawekwa na Halmashauri, japokuwa mnajua kwamba katika suala zima la cealing ya bajeti wakati mwingine ile cealing ikishaondoka vipaumbele vingine vinakwama, lakini tutaangalia jinsi gani tutafanya, lengo letu kubwa ni kwamba wananchi katika kila
maeneo waweze kupata huduma. Na ndiyo maana tunafanya harakati mbalimbali kufanya marekebisho makubwa katika sekta ya afya lakini imani yangu ni kwamba tutafika mahali pazuri tutasimama vizuri. Kwa hiyo wananchi, ndugu zangu wa Tabora ambao wengi ni watani wangu naomba msiwe na hofu kwamba Serikali yenu iko nanyi kuhakikisha kwamba mambo yanakuwa mazuri.