Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Vedasto Edgar Ngombale Mwiru

Sex

Male

Party

CUF

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. VEDASTO E. NGOMBALE aliuliza:- Tanzania ni moja ya nchi duniani zilizoathirika kutokana na Tawala za Kikoloni na Vita ya Majimaji ni moja ya vielelezo vya athari hizo ambapo vita hiyo vilianzia Wilayani Kilwa katika Kijiji cha Nandete mwaka 1905-1907:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha waathirika wa Vita vya Majimaji wanapata fidia kutoka kwa utawala wa kikoloni wa Kijerumani?

Supplementary Question 1

MHE. VEDASTO E. NGOMBALE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue nafasi hii kumshukuru Mheshimiwa Waziri, lakini pia kukishukuru Kiti chako kwa sababu swali hili nililileta kwa mara ya kwanza halikupata majibu muafaka ya Serikali. Kwa majibu haya kidogo napata faraja kwamba ndugu zangu wale wa Kilwa watakwenda kupata fidia kutoka Serikali ya Ujerumani chini ya usimamizi wa Serikali ya Tanzania. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, niishauri pia Serikali katika suala hili kwamba wenzetu wa Kenya waliendesha mchakato wa kudai fidia za waathirika wa Vita ya Maumau na Serikali ya Uingereza ikatoa fidia kwa waathirika wale. Kwa hiyo, nishauri Serikali nayo ikajifunze kutoka Kenya.
Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nina maswali mawili ya nyongeza. La kwanza, kwa kuwa historia ya Vita ya Majimaji imechanganywachanganywa na kuvurugwa; na kwa kuwa Taifa hili limedanganywa eti kwamba Kinjekitile Ngwale ndiyo kiongozi wa Vita ya Majimaji. Ukweli ni kwamba Kinjekitile Ngwale siyo kiongozi wa Vita ya Majimaji na kiongozi wa Vita ya Majimaji ni Sikwako Mbonde na majemedari wake Ngumbalio Mandai, Lindimio Machela, Ngumbe-kumbe Mwiru na wengine. Serikali iko tayari sasa kufanya utafiti wa kihistoria ili basi kuwaeleza Watanzania ukweli wa jambo hili? (Makofi/Kicheko)
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kwa misingi hiyo ya kuchanganya historia ya Vita ya Majimaji, sherehe za kumbukumbu za Mashujaa wa Vita ya Majimaji kila mwaka zinafanywa Majimaji Songea badala ya kufanywa Nandete Kipatimu. Serikali iko tayari kuhamisha sherehe zile kutoka Majimaji Songea kwenda Nandete Kipatimu ambako ndiko chanzo cha Vita ya Majimaji?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nataka nikubaliane naye kuhusu ushauri anaoutoa kwamba Tanzania ikajifunze kutoka Kenya kwa sababu Wakenya waliweza kudai fidia ya Vita vya Maumau na waliweza kupata fidia hiyo, tunakubaliana naye na tutafanya hivyo ili tuweze kujua wenzetu wanafanyaje. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili la kufanya utafiti wa kihistoria ili kupata ukweli wa vita hii na uongozi wake na kadhalika nao ni ushauri mzuri, tunaupokea tutafanya kazi hiyo. Sasa ni hapo baada ya kupata ukweli huo, ndiyo hilo swali lake la tatu litaweza kupata jibu muafaka. Kwa sababu siwezi kulijibu sasa mpaka pale historia itakapopatikana na ukweli ukajulikana ndipo tutaweza kulizungumza hilo swali lake la tatu.

Name

Riziki Shahari Mngwali

Sex

Female

Party

CUF

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. VEDASTO E. NGOMBALE aliuliza:- Tanzania ni moja ya nchi duniani zilizoathirika kutokana na Tawala za Kikoloni na Vita ya Majimaji ni moja ya vielelezo vya athari hizo ambapo vita hiyo vilianzia Wilayani Kilwa katika Kijiji cha Nandete mwaka 1905-1907:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha waathirika wa Vita vya Majimaji wanapata fidia kutoka kwa utawala wa kikoloni wa Kijerumani?

Supplementary Question 2

MHE. RIZIKI S. MNGWALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, actually swali langu lilikuwa ni nyongeza kwa hapo kwamba katika hiyo historia kinachogombewa zaidi katika kumbukumbu ni ile orodha sahihi ya majina ya mashujaa wetu wale ili waenziwe kwa namna inavyostahiki. Kwa hiyo, nyongeza yangu ilikuwa, je, Serikali katika huo utafiti wake itatuletea pia orodha sahihi ya mashujaa hawa?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa tumeshakiri kwamba tuko tayari sasa kufanya utafiti wa historia, kwa hivyo, orodha kamili itakayopatikana italetwa kama Mheshimiwa Mbunge anavyotaka.

Name

Kabwe Zuberi Ruyagwa Zitto

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. VEDASTO E. NGOMBALE aliuliza:- Tanzania ni moja ya nchi duniani zilizoathirika kutokana na Tawala za Kikoloni na Vita ya Majimaji ni moja ya vielelezo vya athari hizo ambapo vita hiyo vilianzia Wilayani Kilwa katika Kijiji cha Nandete mwaka 1905-1907:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha waathirika wa Vita vya Majimaji wanapata fidia kutoka kwa utawala wa kikoloni wa Kijerumani?

Supplementary Question 3

vya Majimaji ni Mahenge ambako takribani Watanzania wakati ule Watanganyika 30,000 waliuawa kwa njaa kwa sababu wanajeshi wa Ujerumani walichoma chakula cha Watanzania ili wasiweze kuishi na kufa jambo ambalo kwa tafsiri za kivita ni sawasawa na genocide.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa tayari Serikali ya Ujerumani imeomba radhi na kulipa fidia kwenye Vita ya Namaqua na Herero Namibia, Serikali sasa katika mapendekezo ambayo imeyakubali kutoka kwa Mheshimiwa Mbunge itapeleka kwa Serikali ya Ujerumani pamoja na ombi la kuomba radhi rasmi kwa mauaji ambayo wanajeshi wake waliyafanya Tanzania?

Name

Dr. Hussein Ali Mwinyi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwahani

Answer

WAZIRI WA ULINZI NA JESHI LA KUJENGA TAIFA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni dhahiri kabisa kwamba mifano ya nchi zilizoomba fidia kwa vita vilivyotokea kipindi cha ukoloni ni mingi, hapa tumetajiwa Kenya, lakini sasa tunaambiwa Namibia. Kwa hivyo, nitawaomba wenzetu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki wakati wanataka kuanza rasmi taratibu hizi ili tuweze kupata hiyo fidia basi wawasiliane na nchi hizi ili kujua wameanzaje na hatimaye tuweze kupeleka hilo ombi rasmi. Wakati huohuo nataka nikubaliane na Mheshimiwa Zitto kwamba, pamoja na fidia, kama itathibitika kwamba kulikuwa kuna mambo yaliyofanyika ambayo yanaashiria genocide, basi Serikali hiyo iweze kuomba msamaha vilevile.