Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI (K.n.y. MHE. MAHMOUD H. MGIMWA) aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika Kata ya Ikongosi likiwemo na Gereza la Ilupilo, Kata ya Ikweha yenye Vijiji vya Ukelemi, Uyela, Ugenza, Uhambila, Makongomi, Matelefu, Utosi pamoja na Mbugi.

Supplementary Question 1

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, naomba kwa niaba ya Mheshimiwa Mahmoud Mgimwa, Mbunge wa Mufindi Kaskazini kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, kuna mradi wa densification na underline transformer. Mradi huu unafikisha umeme katika maeneo ambayo REA Awamu ya Pili ulifikisha katika baadhi ya Kata lakini siyo vijiji vyote.
Je, ni nini kauli ya Serikali kuhusiana na maeneo ambayo Kata zile zimefikiwa na umeme lakini siyo vijiji vyote na chini ya mradi huo wa densification na underline transformer inaeleza kwamba unaweza kufikisha umeme ndani ya umbali wa kilometa 10, nini kauli ya Serikali kwa wananchi wa maeneo hayo?
Swali la pili, Mji wa Mafinga ni kati ya miji michache inayokua kwa kasi hapa nchini na ndiyo kitovu cha shughuli za uchumi za Wilaya ya Mufindi, lakini maeneo mengi hayajafikiwa na umeme kama vile Machinjio Mapya, Makalala, Ihongole, Mwongozo na Lumwago. Je, Serikali iko tayari kujenga sub-station ili kuwezesha wananchi kufanya shughuli zao za kiuchumi kwa asilimia mia moja?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa mradi wa REA awamu ya tatu kimsingi una sehemu tatu. Sehemu ya kwanza ni kupeleka umeme katika maeneo yote ambapo kuna miundombinu ya awamu ya pili lakini component ya pili na kwa niaba ya Mheshimiwa Chumi na Waheshimiwa wananchi wa kule Mufindi pamoja na Mafinga ni kwamba awamu ya tatu itahusisha sasa kupeleka umeme kwenye vitongoji na vijiji vyote kupitia mradi aliosema densification.
Mradi wa densification unapeleka umeme kutoka kwenye miundombinu mikubwa kwenda kwenye vijiji na vitongoji. Nimhakikishie Mheshimiwa Chumi kwamba, vijiji vyake vyote vya Sao Hill vitapata umeme kupitia mradi huu, hata pale Changarawe atapata umeme. Isalavanu, Itubiravamu na Ibongoboni vyote vitapata umeme kupitia mradi huu. Nimhakikishie hata Kijiji chake cha Mkalala pamoja na Bubirayinga vitapata umeme kupitia mradi huu wa Itubiravamu.
Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na swali lake la pili juu ya maeneo ya Mafinga. Ni kweli kabisa maeneo ya Mafinga sasa yana kazi kubwa. Mafinga sasa inapata umeme kutoka Iringa ambako ni kilometa 70, pia kutoka Mgololo kilometa 60, sasa ipo haja kwa kweli kujenga sub-station. Nimhakikishie tunajenga sub-station mwaka wa fedha unaokuja.

Name

Juma Selemani Nkamia

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI (K.n.y. MHE. MAHMOUD H. MGIMWA) aliuliza:- Je, ni lini Serikali itapeleka umeme katika Kata ya Ikongosi likiwemo na Gereza la Ilupilo, Kata ya Ikweha yenye Vijiji vya Ukelemi, Uyela, Ugenza, Uhambila, Makongomi, Matelefu, Utosi pamoja na Mbugi.

Supplementary Question 2

MHE. JUMA S. NKAMIA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niulize swali moja tu dogo la nyongeza. Katika mwaka huu wa fedha kuna baadhi ya vijiji katika Wilaya ya Chemba vimeorodheshwa kwamba vitapata umeme. Nataka Mheshimiwa Waziri na Serikali nzima hii inihakikishie mradi huu utaanza kutekelezwa lini?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, miradi yote niliyotaja ya REA awamu ya tatu inaanza kutekelezwa tarehe 15 Desemba, mwaka huu na itakamilika 2019. Kwa hiyo, eneo la Chemba Mheshimiwa Nkamia nimhakikishie vijiji vyake vyote, shule zake zote, pamoja na vituo vya maji vitapatiwa umeme kuanzia mwezi niliotaja na kuishia 2019.