Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Mohamed Keissy

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE.ALLY K. MOHAMED aliuliza:- Vituo vya Polisi vya Kabwe na Kirando vimechakaa sana na hata polisi hawana nyumba za kuishi:- Je, ni lini Serikali itajenga au kukarabati vituo hivyo na kuwajengea polisi nyumba za kuishi?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY K. MOHAMED: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Vituo vya Kirando na Kabwe ni majengo ambayo Wizara ya Mambo ya Ndani ilinunua kwa wananchi wa kawaida. Ni majengo yaliyojengwa kwa tofali mbichi na hata leo akienda kuyaona hayana milango, saruji na yanabomoka na baadhi ya nyumba za uani wanazolala polisi hazina milango kabisa. Je, katika hizo nyumba 4,136 vituo vya Kirando ni miongoni mwa vituo vitakavyokarabatiwa?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, je, Mheshimiwa Naibu Waziri yuko tayari kufanya ziara katika Wilaya ya Nkasi kuvitembelea Vituo vya Polisi Kirando na Kabwe na vituo vya Uhamiaji vya Mwambao wa Ziwa Tanganyika ambavyo viko katika hali mbaya sana, havistahili Polisi kuishi wala kufanyia kazi?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, ujenzi wa nyumba 4,136 hausiani na ukarabati wa vituo vya Kabwe na Kirando. Hata hivyo, kama nilivyozungumza katika jibu langu la msingi ni kwamba tuna program vilevile ya ujenzi wa vituo vya polisi nchi nzima. Ingawa kutokana na udharura wa vituo vya Kabwe na Kirando kwa kuwa ujenzi wa vituo na uimarishaji wa usalama katika nchi yetu unakwenda sambamba na maendeleo ya nchi hii, basi ikiwa Mheshimiwa Mbunge ataona inafaa si vibaya katika Mfuko wa Jimbo akaangalia uwezekano wa kukarabati vituo hivyo. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili kuhusiana na ziara, tutaangalia uwezekano huo. Kama ambavyo nimekuwa nikizungumza kila siku, wajibu wetu ni kuweza kufanya ziara nchi nzima katika maeneo yote kuangalia changamoto zinazokabili vyombo hivi ambavyo viko chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani na Nkasi ni moja ya sehemu hizo.

Name

Mwanne Ismail Mchemba

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Tabora Mjini

Primary Question

MHE.ALLY K. MOHAMED aliuliza:- Vituo vya Polisi vya Kabwe na Kirando vimechakaa sana na hata polisi hawana nyumba za kuishi:- Je, ni lini Serikali itajenga au kukarabati vituo hivyo na kuwajengea polisi nyumba za kuishi?

Supplementary Question 2

MHE. MWANNE I. MCHEMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi na mimi niulize swali dogo. Kwa kuwa matatizo ya Wilaya ya Nkasi yanafanana na matatizo ya Mkoa wa Tabora na kwa kuwa nyumba za Polisi na Magereza za Mkoa wa Tabora ni mbovu sana ikiwa ni pamoja na miundombinu ya vyoo. Pamoja na kipaumbele katika Mkoa wa Tabora yuko tayari twende naye kwa gharama zangu akaone hali halisi ya vyoo?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMABO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, nipo tayari lakini siyo kwa gharama zake. (Kicheko)
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa bahati nzuri nilikuwa na ratiba ya kutembelea Tabora pamoja na Rukwa katika kipindi hiki kwenye ile ziara yetu pamoja na Waheshimiwa Wabunge wanaotokea huko kwenye kambi za makazi ya waliokuwa wakimbizi. Basi tutaunganisha ziara hiyo weekend moja kabla hatujaondoka Dodoma, tuwasiliane baadaye kwa ajili hiyo.

Name

Martha Moses Mlata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE.ALLY K. MOHAMED aliuliza:- Vituo vya Polisi vya Kabwe na Kirando vimechakaa sana na hata polisi hawana nyumba za kuishi:- Je, ni lini Serikali itajenga au kukarabati vituo hivyo na kuwajengea polisi nyumba za kuishi?

Supplementary Question 3

MHE. MARTHA M. MLATA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa majibu mazuri ya Naibu Waziri lakini naomba, kwa sababu Singida ni center ambapo watu wengi wanaosafiri wanapita mkoa ule na unaona kabisa zile nyumba za maaskari pale kushoto baada ya uwanja wa Namfua. Sasa yuko tayari kuanzia pale kabla hajaenda mikoa mingine ili zile nyumba zikatengeneze sura ya Mkoa wa Singida?

Name

Charles Muhangwa Kitwanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Martha Mlata, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Singida na Tabora siyo mbali basi tutazingatia pendekezo lake.

Name

Omary Ahmad Badwel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bahi

Primary Question

MHE.ALLY K. MOHAMED aliuliza:- Vituo vya Polisi vya Kabwe na Kirando vimechakaa sana na hata polisi hawana nyumba za kuishi:- Je, ni lini Serikali itajenga au kukarabati vituo hivyo na kuwajengea polisi nyumba za kuishi?

Supplementary Question 4

MHE. OMARY A. BADWEL: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja dogo la nyongeza. Kwa kuwa wananchi wengi wameitikia wito wa kusaidiana na Serikali katika kujenga Vituo vya Polisi hususani katika Wilaya yangu Bahi, wananchi wa Kijiji cha Chipanga A, kwa miaka mitano iliyopita wamejenga kituo cha kisasa, kikubwa na kwa asilimia 100 wamejenga wao wenyewe. Licha ya Mheshimiwa Waziri wa Mambo ya Ndani aliyekuwepo Mheshimiwa Shamsi Vuai Nahodha na Naibu Waziri wa baadaye Mheshimiwa Silima kutembelea kituo kile na kumuomba kifunguliwe na wao wakaahidi kitapokelewa na Serikali na kufunguliwa lakini hadi sasa ni miaka mitano mpaka kituo kile kinachakaa hakijafunguliwa. Je, ni lini Serikali sasa itakipokea kituo hicho na kukifungua kabla hatujaamua kukitumia kwa matumizi mengine?

Name

Charles Muhangwa Kitwanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Bahi, kwa jinsi ambayo wameweza kushiriki kikamilifu katika ujenzi wa kituo hicho. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pili, nichukue fursa hii kuwaelekeza Jeshi la Polisi nitakapotoka hapa wanipatie taarifa ni kwa nini mpaka leo kituo hiki hakijafunguliwa. Baada ya kupata taarifa hiyo tutakaa na Mheshimiwa Mbunge tuone utaratibu wa kuweza kukifungua.

Name

Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Primary Question

MHE.ALLY K. MOHAMED aliuliza:- Vituo vya Polisi vya Kabwe na Kirando vimechakaa sana na hata polisi hawana nyumba za kuishi:- Je, ni lini Serikali itajenga au kukarabati vituo hivyo na kuwajengea polisi nyumba za kuishi?

Supplementary Question 5

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Namshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri, majibu yenye matumani makubwa katika Mkoa wetu wa Lindi.
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza niipongeze Serikali kwa kuanzisha Mfuko huu wa UCSAF. Kwa utekelezaji wake katika Mkoa wetu wa Lindi ni kata 25 na vijiji 99 ambavyo tunavitarajia vianze kupata mawasiliano. Ningependa kujua ni kwa namna gani Serikali watapeleka msukumo kwa watoa huduma hii ya mawasiliano ili vijiji hivi 99 na kata 25 za Mkoa wa Lindi ziweze kupata mawasiliano?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza naomba nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa juhudi zake za kufuatilia suala hili. Alikuja ofisini na alikutana na Waziri wangu na kwa kweli pamoja na Wabunge wengine wa Mkoa wa Lindi wanalifuatilia sana suala hili ikiwa ni pamoja na Mheshimiwa Waziri Mkuu.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kuthibitisha kwamba tutayafuatilia haya makampuni yanayotoa huduma. Kwa wale ambao hawana huduma za kutosha tutahakikisha UCSAF inaingilia ili yapatikane mawasiliano kama ambavyo tumekusudia kutoa mawasiliano kwa vijiji vyote vya Tanzania.
NAIBU SPIKA: Mheshimiwa Waziri samahani kidogo. Mheshimiwa kule nyuma umesimama sijaelewa. Mheshimiwa Naibu Waziri naomba umalizie.
NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, nimesema kwamba tutazifuatilia hizi kampuni kuhakikisha kwamba zinatimiza wajibu wake wa kupeleka mawasiliano katika vijiji husika vya Mkoa wa Lindi vyote 99 katika kata 25 pamoja na vijiji vyote Tanzania nzima.

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE.ALLY K. MOHAMED aliuliza:- Vituo vya Polisi vya Kabwe na Kirando vimechakaa sana na hata polisi hawana nyumba za kuishi:- Je, ni lini Serikali itajenga au kukarabati vituo hivyo na kuwajengea polisi nyumba za kuishi?

Supplementary Question 6

MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa Mkoa wa Katavi, Wilaya ya Mlele, Kata ya Ilunde imesahaulika kabisa kwa mawasiliano. Je, Serikalini ni lini watapeleka mawasiliano Kata ya Ilunde?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI, UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyosema katika jibu langu la msingi, tunakusudia kupeleka mawasiliano vijiji vyote Tanzania nzima. Namhakikishia hicho Kijiji cha Ilunde kitapata mawasiliano. Kumwambia lini, naomba anipe muda zaidi niwasiliane na yule mtu anayehusika kupeleka mawasiliano tupate uhakika, nitakuja kujibu nikishapata majibu sahihi. Namhakikishia mawasiliano yatapatikana katika kata hiyo na nitafuatilia kwa makini. Nakushukuru sana kwa juhudi zako za kufuatilia suala hili.

Name

Omary Tebweta Mgumba

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE.ALLY K. MOHAMED aliuliza:- Vituo vya Polisi vya Kabwe na Kirando vimechakaa sana na hata polisi hawana nyumba za kuishi:- Je, ni lini Serikali itajenga au kukarabati vituo hivyo na kuwajengea polisi nyumba za kuishi?

Supplementary Question 7

MHE. OMARY T. MGUMBA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwa kuwa matatizo yaliyopo katika Mkoa wa Lindi yanafanana kabisa na yaliyopo katika Mkoa wa Morogoro kwenye Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki hasa kwenye Kata za Maturi, Mkulazi, Seregeti na Tununguo. Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka minara katika kata hizi na Vijiji vyake vile vya Usungura, Kidunda na vinginevyo ili kuimarisha mawasiliano katika vijiji hivyo?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba tena kuchukua fursa hii kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kama nilivyotoa maelezo katika jibu la swali la msingi kwamba tuna dhamira ya kuhakikisha kwamba vijiji vyote vinapata mawasiliano. Kwa hiyo, naomba kuchukua fursa hii kumhakikishia kwamba tutafuatilia kuhakikisha katika Jimbo lake na hizo kata alizozitaja, mawasiliano ya simu yanapatikana kupitia Mic, Airtel, Tigo, Vodacom, Viettel pamoja na wengine ambao wanakuja karibuni tutakapotoa tenda ya masafa ya mawasiliano.

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE.ALLY K. MOHAMED aliuliza:- Vituo vya Polisi vya Kabwe na Kirando vimechakaa sana na hata polisi hawana nyumba za kuishi:- Je, ni lini Serikali itajenga au kukarabati vituo hivyo na kuwajengea polisi nyumba za kuishi?

Supplementary Question 8

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa Mkoa wa Kigoma ni kati ya mikoa ambayo iko pembezoni na viko vijiji ambavyo vimepakana na nchi jirani ya Burundi na vijiji hivyo havina mawasiliano. Je, Serikali iko tayari kushawishi makampuni kupeleka minara katika Vijiji vya Kitanga (Kasulu), Kilelema (Buhigwe) na Nyagwijima (Kibondo)?

Name

Eng. Edwin Amandus Ngonyani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Answer

NAIBU WAZIRI UJENZI, UCHUKUZI NA MAWASILIANO: Mheshimiwa Naibu Spika, tupo tayari na kwa kweli ndicho tunachokifanya siku zote hizi. Mheshimiwa Mbunge anafahamu kwamba katika suala la mawasiliano mipakani ni priority namba moja.