Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jacqueline Kandidus Ngonyani (Msongozi)

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza:- Katika Ilani ya CCM 2016/2017 Serikali imeahidi kuinua kipato cha mwananchi mmoja mmoja:- Je, ni lini Serikali itaanza kutoa fedha kiasi cha shilingi 50,000,000 kwa kila Kijiji au Mtaa ili kuwasaidia wananchi kuboresha mitaji yao?

Supplementary Question 1

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Waziri, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Kwanza, Mkoa wa Ruvuma ni miongoni mwa mikoa yenye wananchi wengi sana na katika vijiji ambavyovimeainishwa kwa ajili ya kupewa mikopo hiyo, kila kijiji kina wastani wa wananchi 5,000 ambao wana uwezo wa kufanya kazi za uzalishaji. Je, Serikali ina mpango gani wa kuwapa mikopo yenye tija wananchi hao?
Swali la pili, kama wanakijiji watapata shilingi 1,000 kila mmoja itakayotokana na shilingi milioni 50. Je, watawekeza kwenye biashara gani ili wapate faida kwenye uwekezaji huo?

Name

Jenista Joackim Mhagama

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Peramiho

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WALEMAVU): Mheshimiwa Naibu Spika, nianze kumpongeza sana huyu Mheshimiwa Mbunge wa Viti Maalum kutoka Mkoa wa Ruvuma kwa kazi nzuri na jitihada kubwa anayoifanya ya uwakilishi ndani ya Bunge na hasa kuwawakilisha Watanzania wote, lakini hasa hasa wanawake wa Mkoa wa Ruvuma nampongeza sana. Mheshimiwa Mbunge ameniuliza maswali mawili la kwanza ameonyesha idadi ya watu jinsi ilivyo, katika maeneo mbalimbali kwenye Vijiji vya Mkoa wa Ruvuma, akitaka kujua kama tuna mpango mahususi katika Serikali wa kuhakikisha vijiji hivyo vinapata mikopo.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba, wakati tukipitisha bajeti ya Mheshimiwa Waziri Mkuu, Fungu 65 mradi namba 49, 45 pamoja na hiyo milioni 50. Hata hivyo, Serikali imetenga fedha nyingine bilioni moja kwa ajili ya kuhakikisha kwamba vijana na akina mama wanapata mikopo katika maeneo mbalimbali nchini Tanzania. Hata hivyo, Serikali pia kupitia Halmashauri zetu itaendelea kutenga asilimia tano ya mapato kwa ajili ya akinamama na vijana. Kwa hiyo, namhakikishia kwamba nguvu hizo zote zitasaidia.
Mheshimiwa Naibu Spika, katika swali lake la pili la nyongeza amesema, pia anakadiria wastani wa shilingi 1,000 kama Mfuko huo utakopeshwa kwa wananchi, kwa idadi ya wananchi ambao wanaweza kuifanyia kazi. Namwomba Mheshimiwa Mbunge asubiri kama nilivyosema, tunatengeneza utaratibu na mfumo mzuri ambao utasaidia kuhakikisha kwamba wakopaji watapata fedha yenye tija na wataweza kufanya kazi na biashara ambazo zitainua kipato kwa familia zao na Taifa zima kwa ujumla.

Name

Mary Pius Chatanda

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Korogwe Mjini

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza:- Katika Ilani ya CCM 2016/2017 Serikali imeahidi kuinua kipato cha mwananchi mmoja mmoja:- Je, ni lini Serikali itaanza kutoa fedha kiasi cha shilingi 50,000,000 kwa kila Kijiji au Mtaa ili kuwasaidia wananchi kuboresha mitaji yao?

Supplementary Question 2

MHE. MARY P. CHATANDA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ili niulize swali la nyongeza. Kwenye taarifa ya Waziri wa Fedha aliyoiwasilisha hii ya bajeti, imezungumzia tu suala la milioni 50, kwamba zitakwenda kwenye vijiji, haikuzungumzia Mitaa, kama ambavyo Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Makamu wa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan walizungumza walipokuwa wakipita kwenye kampeni kwamba watahakikisha Mitaa na Vijiji vinapata mikopo ya milioni 50. Je, Serikali inatuambia nini juu ya wananchi wanaoishi mijini, ambao wana mitaa badala ya vijiji?

Name

Jenista Joackim Mhagama

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Peramiho

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WALEMAVU): Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue nafasi hii pia kumpongeza Mheshimiwa Mary Chatanda, Mbunge mwanamke wa Jimbo pia kwa kazi nzuri za uwakilishi anazozifanya na nina imani kule Korogwe Mjini wako salama.
Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyokuwa najibu katika swali langu la msingi, kwamba kazi kubwa ambayo tunaendelea kuifanya sasa hivi ili kufanya maandalizi mazuri ya Mfuko huu, kuweza kutumika kwa Watanzania wote. Kama ilivyoainishwa katika Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi, ni pamoja pia na kutafsiri maana ya Mitaa na Vijiji kwa kuzingatia Sheria ya Local Government kama ilivyoweka mipaka katika maeneo ya mijini na vijijini.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba niwaambie Wabunge wawe na amani, watulie. Serikali yao inafanya kazi na utaratibu utawekwa wazi na tunahakikisha kwamba Watanzania hawa watanufaika na fedha hizi kama vile tulivyoainisha kwenye Ilani ya Uchaguzi ya Chama cha Mapinduzi ya mwaka 2015.

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. JACQUELINE N. MSONGOZI aliuliza:- Katika Ilani ya CCM 2016/2017 Serikali imeahidi kuinua kipato cha mwananchi mmoja mmoja:- Je, ni lini Serikali itaanza kutoa fedha kiasi cha shilingi 50,000,000 kwa kila Kijiji au Mtaa ili kuwasaidia wananchi kuboresha mitaji yao?

Supplementary Question 3

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa muda wa kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Mheshimiwa Waziri ametoa majibu mazuri sana, kwanza nampongeza. Pili kwa kuwa kundi la walemavu limekuwa likisahaulika sana hasa katika suala hili la mikopo, ukizingatia wapo vijana wa kike na wa kiume, lakini je, kwenye mpango huu wa milioni 500, kundi la walemavu limekuwa considered namna gani. Je, Mheshimiwa Waziri anaweza kunithibitishia hilo?

Name

Jenista Joackim Mhagama

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Peramiho

Answer

WAZIRI WA NCHI, OFISI YA WAZIRI MKUU (SERA, BUNGE, KAZI, AJIRA, VIJANA NA WALEMAVU): Mheshimiwa Naibu Spika, nichukue nafasi hii pia kumpongeza sana Mheshimiwa Massay kwa kazi nzuri anayoifanya Bungeni ya kuwawakilisha wananchi wake wa Jimbo la Mbulu na hata walemavu pia.
Mheshimiwa Naibu Spika, Sheria Namba Tisa ya mwaka 2010 ambayo inaongoza na kuratibu shughuli zote za watu wenye ulemavu nchini, zinatutaka na kutukumbusha kwamba, katika kila suala tunalolifanya kwenye nchi yetu ya Tanzania, lizingatie pia kwamba walemavu wanatakiwa wapewe haki sawa katika nchi yetu ya Tanzania. Kwa hiyo, tunapoandaa taratibu na miongozo kwa ajili ya fedha hizi, Sheria Namba Tisa ya mwaka 2010 itachukua nafasi yake, kuhakikisha pia walemavu wanakumbukwa katika mpango huu mzima.