Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: - Je, mpango wa kuugawa Mkoa wa Morogoro umefikia wapi hasa baada ya kuonekana kuwa na sifa ya kugawanywa.

Supplementary Question 1

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru.

Kwa kuwa, shughuli nyingi za maendeleo zinazofanyika vijijini zinafanywa na wananchi wenyewe na vijiji vingi ni vikubwa kiasi kwamba kumekuwa na mivutano. Serikali haioni kwamba ni wakati sahihi sasa angalau wa kufanya mgawanyo wa vijiji ili shughuli za maendeleo vijijini ziendelee kufanyika vizuri?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, nikijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mnzava, mchakato wa kuanzisha maeneo ya utawala ya Mikoa, Wilaya, Tarafa, Kata na Vijiji ni mchakato unaofanywa kwa mujibu wa Sheria, Kanuni na taratibu zilizopo. Wao wanatakiwa waanzishe wenyewe mchakato ule kupitia vikao vyao na kama ni katika ngazi ya Wilaya wanalipitisha kwenye DCC kisha inakwenda Mkoani kwenye RCC na ndipo mapendekezo yanaletwa.

Mheshimiwa Spika, lakini kama nilivyojibu kwenye majibu yangu ya msingi, kwa sasa Serikali imeweka kipaumbele katika kuyaendeleza yale maeneo ambayo ni mapya ya kiutawala.

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: - Je, mpango wa kuugawa Mkoa wa Morogoro umefikia wapi hasa baada ya kuonekana kuwa na sifa ya kugawanywa.

Supplementary Question 2

MHE. MWITA. M. WAITARA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Mwaka jana Serikali ilitoa maelekezo kwenye Majimbo yetu na Mikoa yetu na wakapeleka masharti wapendekeze maeneo ambayo wanataka kuongeza vitongoji, vijiji na Kata. Kwa hiyo, Kata mbalimbali zilikaa na kutumaini kwamba watapewa maeneo hayo waliyoomba.

Kwa sasa, nini kauli ya Serikali juu ya maelekezo ambayo waliyatoa katika maeneo yetu? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Waitara. Ni kama kwenye majibu yangu ya msingi kwamba kwa sasa, Serikali imeweka kipaumbele katika kuhakikisha yale maeneo mapya ya kiutawala yaliyopo yanapata miundombinu ambayo ni stahiki kwa maeneo yale.

Mheshimiwa Spika, hivi karibuni tumeona Halmashauri nyingi zimekwenda katika maeneo yao ya kiutawala na Serikali imepeleka fedha nyingi katika ujenzi wa miundombinu ikiwemo ofisi za Halmashauri, ofisi za Wakuu wa Wilaya kwenye Wilaya mpya na kadhalika. Kwa hiyo, mpaka pale ambapo Serikali itakapokuwa imekamilisha ujenzi wa miundombinu ya msingi katika maeneo yaliyopo sasa ndipo itaendelea na mchakato wa kuongeza maeneo mengine.

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: - Je, mpango wa kuugawa Mkoa wa Morogoro umefikia wapi hasa baada ya kuonekana kuwa na sifa ya kugawanywa.

Supplementary Question 3

MHE. VITA R. KAWAWA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Namtumbo tulifuata taratibu zote, vikao vya Kata vilifanyika, Halmashauri (DCC na RCC) kuomba kugawanyika kwa vijiji na Kata: Je, Serikali wakati ukifika mtatupatia kipaumbele?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, nikijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Vita Kawawa, Namtumbo ni mojawapo ya maeneo ambayo yameshakamilisha mchakato mzima wa kuomba maeneo mapya ya kiutawala kama ilivyo katika Halmashauri na Wilaya nyingine na Mikoa mingine hapa nchini; na pale Serikali itakapoanza mgawanyo, basi kipaumbele pia kitawekwa kwa wenzetu wa kule Namtumbo.

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA aliuliza: - Je, mpango wa kuugawa Mkoa wa Morogoro umefikia wapi hasa baada ya kuonekana kuwa na sifa ya kugawanywa.

Supplementary Question 4

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Jimbo la Chemba lina Kata tano…

SPIKA: Simamisha kisemeo vizuri.

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Spika, Jimbo la Chemba lina Kata tano ambazo zina vijiji zaidi ya vinane, hivyo imekuwa ni kazi kubwa sana kwa Watendaji wa Kata kufanya kazi. Nini sasa msimamo wa Serikali kugawa Kata hizo? Ahsante. (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, nikijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Monni, nirejee katika majibu yangu ya msingi, pale ambapo miundombinu itajengwa katika maeneo ya kiutawala yaliyopo sasa ya kukidhi mahitaji yote ya wananchi katika maeneo hayo, ndipo Serikali itaenda katika mchakato wa kugawa maeneo mengine.

Mheshimiwa Spika, ni kwa sababu unapogawa kata, maana yake inabidi shule, zahanati na vituo vya afya na huduma nyinginezo ziweze kujengwa.

Mheshimiwa Spika, kwa sasa sote ni mashuhuda, Mheshimiwa Rais wetu, Dkt. Samia Suluhu Hassan ameweka fedha nyingi katika kuhakikisha vituo vya afya vinajengwa, shule mpya zinajengwa katika kata ambazo zilikuwa hazina shule za sekondari. Kwa hiyo, mpaka pale mchakato huu utakapokamilika ndipo Serikali itaanzisha maeneo mapya ya kiutawala.