Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omar Issa Kombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wingwi

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatatua changamoto ya mawasiliano ya simu Micheweni, vijiji vya Sizini, Dodeani, Michungani, Mapofu, Msuka na Makangale?

Supplementary Question 1

MHE. OMAR ISSA KOMBO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nimpongeze Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri lakini naomba niulize maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwenye majibu Serikali imesema itavifanyia tathimini vijiji vilivyobakia je ni lini tathimini hii itaanza?

Mheshimiwa Spika, vilevile asilimia kubwa ya wananchi wa Wilaya ya Micheweni hutumia mitandao ya simu ya halotel na tigo lakini huduma zake zimekuwa ni hafifu mitandao hii. Je, Serikali inachukua jitihada gani kuwaondolea usumbufu wananchi wa maeneo ya vijiji hivi? Ahsante.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Kombo, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kipengele cha kwanza ni lini tutafanya tathimini? Tayari tumeishamaliza kufanya tathimini katika vijiji 2,116 na hivyo naelekeza timu ya wataalam kutoka Wizarani kwetu wakishirikiana na UCSAF waende wakafanye tathimini mara moja katika kata ambazo Mheshimiwa Mbunge ameziomba.

Mheshimiwa Spika, kipengele cha pili ni cha kiufundi na kibiashara, pia ni cha kisheria, kwa sababu kinaangukia katika upande wa sheria kwa mujibu wa Sheria Namba 12 ya Mwaka 2003, na kwa kanuni zetu za mwaka 2018 inampatia TCRA mamlaka ya kuhakikisha kwamba inaangalia ubora wa huduma ya mawasiliano. Hivyo, basi nitumie fursa hii kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri kuwaelekeza TCRA kwenda kufanya tathmini na kujiridhisha na quality of service katika maeneo hayo ili tujue ni hatua gani tunazichukua kulingana na majibu ambayo watayaleta, nakushukuru.

Name

Furaha Ntengo Matondo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatatua changamoto ya mawasiliano ya simu Micheweni, vijiji vya Sizini, Dodeani, Michungani, Mapofu, Msuka na Makangale?

Supplementary Question 2

MHE. FURAHA N. MATONDO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itamaliza tatizo la mawasiliano katika Wilaya ya Ukerewe, Kata ya Bukiko ambayo inatumia Mnara wa Halotel 2G na mawasiliano ni ya kusua sua sana? (Makofi)

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Furaha, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ilianza kupandisha hadhi minara ambayo inatoa huduma ya 2G kwenda kwenye 3G mpaka 4G. Tayari Serikali kupitia Mradi wa Tanzania ya Kidijitali tumepandisha hadhi minara 304. Hivyo tunaamini kwamba itakapokamilika tutaangalia baadhi ya meaeneo ambayo bado yana uhitaji huo. Kwa Kata ya Lukiko ambayo ipo katika Jimbo la Ukerewe tumeiingiza kwenye utekelezaji kwa kuhakikisha kwamba tunakwenda kupeleka mnara pale, nakushukuru. (Makofi)

Name

Mohammed Said Issa

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Konde

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatatua changamoto ya mawasiliano ya simu Micheweni, vijiji vya Sizini, Dodeani, Michungani, Mapofu, Msuka na Makangale?

Supplementary Question 3

MHE. MOHAMED SAID ISSA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwa kuwa Mheshimiwa Naibu Waziri, katika jibu lake kwa Mbunge wa Wingwi, ameeleza kwamba atapeleka wataalamu katika maeneo ambayo ameyataja.

Je, wataalamu hao watafika katika Kijiji cha Mkia wa Ng’ombe ambao upo katika Jimbo la Konde, ambako pia tatizo ni sawa na la huko?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mohamed Said, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hili ni ombi, na Serikali ya Chama cha Mapinduzi dhamira yake ni kuhakikisha kwamba inawahudumia Watanzania katika maeneo mbalimbali. Hivyo Wizara tunapokea ombi hilo na tutahakikisha kwamba, wataalamu wetu wanafika katika eneo hilo.

Name

Omari Mohamed Kigua

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilindi

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatatua changamoto ya mawasiliano ya simu Micheweni, vijiji vya Sizini, Dodeani, Michungani, Mapofu, Msuka na Makangale?

Supplementary Question 4

MHE. OMARI M. KIGUA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, kwenye Kata ya Kilindi Asilia na Kata ya Luhande kwenye Vijiji vya Misufini kuna changamoto kubwa ya minara, kwa maana ya mawasiliano yanakatika mara kwa mara.

Je, Mheshimiwa Naibu Waziri, uko tayari kutuma timu yako kuangalia namna ambavyo mawasiliano yanavyopatikana muda wote?

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Omari Kigua, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tuko tayari kama Wizara kutuma wataalamu wetu kwenda kufanya tathmini ili tujiridhishe na uhalisia wa tatizo na kuchukua hatua stahiki, ahsante.

Name

Joseph George Kakunda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sikonge

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatatua changamoto ya mawasiliano ya simu Micheweni, vijiji vya Sizini, Dodeani, Michungani, Mapofu, Msuka na Makangale?

Supplementary Question 5

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, tarehe 9 Januari nilituma message kwa Mheshimiwa Waziri, Naibu Waziri na kwa Mkurugenzi Mkuu wa UCSAF kuhusu minara 12 ya 2G katika Jimbo la Sikonge na wote mlijibu kwamba tumepokea.

Je, sasa ni lini itapandishwa hadhi ili kuwasaidia watu wa Sikonge upande wa internet?

SPIKA: Sasa hizo message tutajuaje sisi kama umetuma, maana ni suala la ushahidi, uliza tu swali lako Mheshimiwa Kakunda.

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Spika, nilishawasilisha tayari taarifa ya minara 12. Sasa ni lini…

SPIKA: Bunge halitakuwa na ushahidi wa hayo mawasiliano yenu. Kwa hiyo uliza swali unalotaka ujibiwe na Mheshimiwa Naibu Waziri.

MHE. JOSEPH G. KAKUNDA: Mheshimiwa Spika, swali ni lini minara 12 ya 2G katika Jimbo la Sikonge itapandishwa hadhi? Nashukuru sana.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Kakunda, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, binafsi naomba nikiri kwamba Mheshimiwa Kakunda anaendelea kuwasiliana na mimi katika changamoto hiyo. Tayari, kwa maelekezo ya Mheshimiwa Waziri timu yetu inaendelea kufanya tathmini na kujiridhisha namna gani tutaweza kwenda kuanza hatua kwa hatua. Hatuwezi kupandisha yote kwa pamoja kwa sababu miradi hii ina budget implication na inategemea na upatikanaji wa fedha.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Kakunda taarifa yake hiyo tunaendelea kuifanyia kazi na wananchi wake watapata huduma hiyo ya internet.

Name

Shabani Hamisi Taletale

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza:- Je, ni lini Serikali itatatua changamoto ya mawasiliano ya simu Micheweni, vijiji vya Sizini, Dodeani, Michungani, Mapofu, Msuka na Makangale?

Supplementary Question 6

MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kuuliza Serikali ni lini itakuja kukamilisha mawasiliano katika Kata ya Gwata, ukizingatia ipo barabarani karibu Morogoro, kwaheri Morogoro na bado watu hawapatikani? Ahsante.

Name

Kundo Andrea Mathew

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bariadi

Answer

NAIBU WAZIRI WA HABARI, MAWASILIANO NA TEKNOLOJIA YA HABARI: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hamisi Taletale, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, katika minara 758 bahati mbaya Kata hii hatukuiingiza, na kwa bahati nzuri Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendelea kutafuta fedha na kuna minara takribani 636 ambapo katika hiyo, minara 15 inaenda kwenye upande wa TBC.

Mheshimiwa Spika, nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge, Kata yake tutaiingiza kwenye minara hiyo 636, ahsante sana.