Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zuena Athumani Bushiri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZUENA A. BUSHIRI aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Soko la kisasa Holili Wilayani Rombo?

Supplementary Question 1

MHE. ZUENA A. BUSHIRI: Mheshimiwa Spika, ahsante, pamoja na majibu mazuri ya Serikali, ninayo maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa ujenzi wa soko hili ulitokana na ahadi ya Mheshimiwa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan wakati huo akiwa ni Makamu wa Rais; na kwa kuwa Waziri Mkuu alipokuja kwenye ziara wananchi wa Rombo walikumbushia ahadi yao: Je, nini kauli ya Serikali kuhusu ujenzi wa soko hili?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, shilingi milioni 75 ni fedha ndogo sana katika ujenzi huu. Je, Serikali kwa nini isiweke ujenzi wa soko hili katika miradi ya kimkakati ili kutimiza ahadi ya viongozi hawa wawili? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Zuena Athumani Bushiri, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie kwamba ahadi za viongozi wetu wa kitaifa ni kipaumbele katika utekelezaji ndani ya Ofisi ya Rais, TAMISEMI. Kwa kuwa ni kweli fedha ambayo imetengwa ni kidogo, nitumie fursa hii kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, kumwelekeza Mkurugenzi wa Halmashauri ya Rombo kufanya tathmini ya kina na upembuzi yakinifu wa gharama zinazohitajika, kwa ajili ya ujenzi wa soko hili na kuziwasilisha Ofisi ya Rais, TAMISEMI ili tuweze kuona kama fedha itatoka Central Government au wanaweza kugharamia kwa mapato ya ndani, ahsante. (Makofi)

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. ZUENA A. BUSHIRI aliuliza:- Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa Soko la kisasa Holili Wilayani Rombo?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa hii nafasi. Halmashauri ya Meru iliwasilisha michoro ya soko la kisasa TAMISEMI mwaka jana mwezi Novemba, kwa maana ya mwaka 2023; soko hili linategemewa kujengwa Eneo la Madira; je, ni lini ujenzi wa soko hili utaanza?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante na naomba kujibu swali la Mheshimiwa Pallangyo, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Spika, tulikuwa na utaratibu wa kuwasilisha miradi ya kimkakati lakini tunafanya tathmini na upembuzi kuona kama fedha kwanza ya Serikali ipo, na pia kama halmashauri zenyewe zinaweza zikagharamia kupitia mapato ya ndani. Kwa hiyo, kwa sababu Mheshimiwa Mbunge anatoa taarifa kwamba limeshawasilishwa Ofisi ya Rais TAMISEMI, naomba tulichukue suala, tutalifanyia kazi tufuatilie, andiko liko wapi, limefikia hatua gani, ili tuweze kuona namna gani tunafanya ili kwenda kujenga soka la kisasa katika eneo hili la Madira, ahsante.