Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaboresha Vituo vya Afya vya Kinyangiri na Mkalama katika Halmashauri ya Mkalama kwa kujenga majengo ya upasuaji na wodi ili kuwa na hadhi ya Vituo vya Afya?

Supplementary Question 1

MHE. FRANCIS I. MTINGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na majibu mazuri ya Serikali yanayotia moyo nina maswali mawili ya nyongeza. Kituo cha Afya Mkalama ni kituo chakavu sana kinazidiwa hata hadhi na baadhi ya zahanati. Je, Serikali haioni haja sasa ya kutamka kabisa rasmi kwamba ni lini watakwenda kufanya ukarabati kwenye kituo hiki ambacho kinahudumia tarafa kubwa sana yenye watu wengi?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; Kituo cha Afya Kinyangiri Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi alipita pale na kutoa ahadi na akaweka na dead line kwamba mwezi wa 12 mwaka huu kitakuwa kimeshafanyiwa upanuzi na ukarabati. Mwenyekiti wa CCM ambaye ni Rais wa Jamhuri Muungano wa Tanzania akakazia ahadi hiyo juzi alivyokuja Singida. Je, Serikali haioni kwamba kuna haja sasa ya kutamka rasmi kwamba wanakwenda kufanya ukarabati kwenye kituo hiki kwa kuzingatia kauli za wakubwa wa nchi hii?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Francis Isack Mtinga Mbunge wa Jimbo la Irambva Mashariki kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na Kituo cha Afya hilki cha Mkalama ambacho ni chakavu sana Serikali imekwisha kiainisha kama nilivyotangulia kusema. Hivi sasa tuko kwenye utaratibu wa kutafuta fedha na fedha ikipatikana mapema iwezekanavyo itapelekwa Halmashauri ya Mkalama kwa ajili ya kujenga Kituo cha Afya cha Mkalama.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na wananchi wa Mkalama kwamba Serikali inatambua uchakavu wa Kituo cha Afya. Inatafuta fedha na mapema iwezekanavyo fedha ikipatikana tutahakikisha kinakarabatiwa na kuwa hadhi ya kituo cha afya kama vilivyo vituo vya afya vingine.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusiana na Kituo cha Afya cha Kinyangiri ni kweli ni maelekezo ya Mheshimiwa Rais na Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi. Sisi Ofisi ya Rais, TAMISEMI maelekezo ya Mheshimiwa Rais ni kipaumbele na natoa kauli rasmi kama alivyosema Mheshimiwa Mbunge kwa niaba ya Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwamba tunakwenda kutekeleza ahadi ya Rais. Tunakwenda kutekeleza ahadi ya Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi mapema iwezekanavyo, ahsante.

Name

Dr. John Danielson Pallangyo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Mashariki

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaboresha Vituo vya Afya vya Kinyangiri na Mkalama katika Halmashauri ya Mkalama kwa kujenga majengo ya upasuaji na wodi ili kuwa na hadhi ya Vituo vya Afya?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. JOHN D. PALLANGYO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Changamoto zilizoko Iramba Mashariki zinafanana sana na Changamoto zilizoko Arumeru Mashariki katika Sekta ya Afya. Je, ni lini Serikali itakuja kuboresha Kituo cha Afya Makida ambacho majengo yake yamekuwa magofu? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Pallangyo, Mbunge wa Jimbo la Arumeru Mashariki kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, nichukue hoja ya Kituo cha Afya cha Makida ambacho ni chakavu na kinahitaji ukarabati ili tuweze kutuma wataalam wa Ofisi ya Rais, TAMISEMI lakini pia Mkoa wa Arusha kufanya tathmini na kutuletea makadirio ya gharama zinazohitajika ili tutafute fedha kwa kupitia mapato ya ndani lakini mahususi kupitia Serikali Kuu ili tuweze kukarabati kituo hiki cha afya kiweze kutoa huduma vizuri, ahsante.

Name

Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaboresha Vituo vya Afya vya Kinyangiri na Mkalama katika Halmashauri ya Mkalama kwa kujenga majengo ya upasuaji na wodi ili kuwa na hadhi ya Vituo vya Afya?

Supplementary Question 3

MHE. JEREMIAH M. AMSABI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuwa Kituo cha Afya Iramba, Wilayani Serengeti ni cha muda mrefu na kimechakaa sana ni lini sasa Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ukarabati wa kituo hiki?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Amsabi Mrimi, Mbunge wa Jimbo la Serengeti kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitumie nafasi hii kumuelekeza Mganga Mkuu wa Mkoa wa Mara na Mganga Mkuu wa Halmashauri ya Serengeti kufanya tathmini kwa maana ya gharama zinazohitajika kwa ajili ya ukarabati wa kituo hiki cha afya na kuwasilisha Ofisi ya Rais, TAMISEMI kwa ajili ya kufanya tathmini lakini pia kutafuta fedha kwa ajili ya ukarabati wa kituo hicho, ahsante.

Name

Miraji Jumanne Mtaturu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Mashariki

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaboresha Vituo vya Afya vya Kinyangiri na Mkalama katika Halmashauri ya Mkalama kwa kujenga majengo ya upasuaji na wodi ili kuwa na hadhi ya Vituo vya Afya?

Supplementary Question 4

MHE. MIRAJI J. MTATURU: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana Jimbo la Singida Mashariki lina kata 13 lakini tulijaliwa kupata kata moja tu ndiyo imejengewa kituo cha afya.

Je, ni lini sasa Serikali itajenga vituoa vya afya vya kata ya Misughaa na Issuna ili kuweka uwiano mzuri katika mkakati wa afya? Ahsante sana.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Miraji Mtaturu, Mbunge wa Jimbo la Singida Mashariki kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mpango wa Serikali wa kujenga vituo vya afya vya kimkakati ni endelevu. Hivi sasa Serikali imeendelea kutafuta fedha kupitia mapato ya ndani ya Serikali Kuu, kupitia mapato ya ndani ya halmashauri lakini pia wadau mbalimbali kuhakikisha yale maeneo ambayo yameainishwa kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya kimkakati yanajengwa vituo hivyo. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge Mtaturu kwamba tutatoa kipaumbele katika kata hizi zmbazo ameziainisha iloi pia ziweze kupata vituo vya afya, ahsante.

Name

Charles Muguta Kajege

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwibara

Primary Question

MHE. FRANCIS I. MTINGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itaboresha Vituo vya Afya vya Kinyangiri na Mkalama katika Halmashauri ya Mkalama kwa kujenga majengo ya upasuaji na wodi ili kuwa na hadhi ya Vituo vya Afya?

Supplementary Question 5

MHE. CHARLES M. KAJEGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi. Je, ni lini Serikali itajenga maabara na wodi ya kina mama na Watoto katika Kituo cha Afya cha Kasuguti?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): -Mheshimiwa Mwenyekiti, mpango wa ujenzi wa vituo vya afya ambavyo vina majengo pungufu kwa kadiri ya standard ya vituo vya afya ni mpango ambao unaendelea kutekelezwa. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tutaendelea kuweka mipango kwa ajili ya kutafuta fedha lakini kwa ajili ya kwenda kufanya ujenzi wa majengo hayokatika kituo hiki cha afya, ahsante.