Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA katika Wilaya ya Meatu?

Supplementary Question 1

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na nashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali. Kwa kuwa Serikali imetenga fedha ya kujenga VETA katika bajeti inayoanza Julai, imetenga fedha ya kujenga VETA 36.

Je, Serikali inaweza ikawaambia nini vijana wa Meatu ambao tayari wameshaandaa eneo la kujenga VETA?

Name

Gibson Blasius Meiseyeki

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Arumeru-Magharibi

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimwa Mwenyekiti, ahsante sana, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Komanya, Mbunge wa Meatu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyoanza kueleza kwenye majibu ya msingi kwamba Serikali ina sera ya kujenga chuo katika kila wilaya nchini. Katika bajeti yetu ya Serikali ni kweli tumetenga zaidi ya shilingi bilioni mia moja kwa ajili ya ujenzi wa vyuo 36 au vyuo katika wilaya 36 nchini. Nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwa vile tutaweka vigezo vya namna gani zile Wilaya 36 tunakwenda kuzipata na kwenda kufanya ujenzi na kwa vile ujenzi unafanyika kwa awamu, nimhakikishie tu na niwahakikishie wananchi wa Meatu katika mgao huo ujao tuwahakikishie kwamba na wao Wilaya ya Meatu tutaweza kuzingatia ili tuweze kupata chuo katika eneo hilo. (Makofi)

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA katika Wilaya ya Meatu?

Supplementary Question 2

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi. Nataka kuuliza Je, Serikali katika hivyo vyuo 36 itakavyojenga na Wilaya ya Ubungo nayo imo katika orodha hiyo?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu swali dogo la Mheshimiwa Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wilaya ambazo hazina vyuo hadi hivi sasa ni Wilaya 62 na katika bajeti yetu ijayo Serikali imetenga fedha kwa ajili ya ujenzi katika Wilaya 36, ni ukweli usiokuwa na shaka kwamba siyo wilaya zote zitakazoweza kupata kwa hiyo tunaweka vigezo na vielelezo vya demand analysis ili kuhakikisha yale maeneo yenye uhitaji mkubwa ndio tunaweza kujenga kwanza halafu vingine tutakwenda kujenga katika mwaka ujao wa fedha, nakushukuru sana.

Name

Zuena Athumani Bushiri

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza:- Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA katika Wilaya ya Meatu?

Supplementary Question 3

MHE. ZUENA A. BUSHIRI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa Wilaya ya Siha ina vijana wengi sana ambao hawajapata nafasi ya kuendelea na masomo ya juu.

Je, Serikali ina mpango gani katika hivi vyuo 36 na yenyewe kupata nafasi ya kujenga Chuo cha VETA? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu swali dogo la Mheshimiwa Mbunge Viti wa Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyoeleza kwamba ujenzi huo unakwenda kwa awamu, kwa hiyo kuna maeneo tutayafikia na kwa vile tutaweka vigezo, cha msingi tutaangalia ule uhitaji mkubwa katika maeneo tutakayoyaainisha. Kwa hiyo nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge kwenye hili, kwa vile Wilaya ya Siha ina uhitaji mkubwa na vijana pale ni wengi kwa vyovyote vile Wilaya ya Siha tutaipa kipaumbele, nakushukuru sana.