Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mohammed Said Issa

Sex

Male

Party

ACT

Constituent

Konde

Primary Question

MHE. MOHAMED SAID ISSA aliuliza:- Je, Serikali inaisaidiaje Zanzibar kupata faida ambazo TFF inazipata katika kuendeleza soka la Tanzania?

Supplementary Question 1

MHE. MOHAMED SAID ISSA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nami naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Swali langu la kwanza, kwa kuwa suala la michezo siyo suala la Muungano; na Zanzibar imekosa kuwa mwanachama kwa sababu ya Tanzania tayari ni mwanachama: Je, ni lini sasa TFF itabadili jina badala ya kuwa Tanzania Football Federation iwe Tanzania Bara Football Federation ili kuipa nafasi Zanzibar kuwa mwanachama? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kama hilo haliwezekani, basi ni lini Serikali itaunda MOU ili kuipa faida za kuwa mwanachama wa FIFA Zanzibar kisheria? (Makofi)

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, naomba kujibu swali la pili la Mheshimiwa Mohamed Saidi Issa, Mbunge wa Konde, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye jibu langu la msingi nimeeleza kwamba ni kweli sisi Wizara yetu tunakiri kuna changamoto kupitia ZFF pamoja na TFF. Waziri wetu Mheshimiwa Mchengerwa ameshakutana na Mheshimiwa Waziri wa Zanzibar wa Michezo, dada yangu Mheshimiwa Tabia wamezungumza, na hivi karibuni baada ya Bunge, tutakutana na vyombo hivi viwili; ZFF pamoja na TFF ili tuweke MOU ya pamoja kuona jinsi gani Zanzibar pia inafaidika na mgao wa fedha za FIFA. (Makofi)

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. MOHAMED SAID ISSA aliuliza:- Je, Serikali inaisaidiaje Zanzibar kupata faida ambazo TFF inazipata katika kuendeleza soka la Tanzania?

Supplementary Question 2

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, Soka la Wanawake Tanzania limetuletea heshima kubwa sana. Mbali ya kwamba hatuna makocha, lakini pia hatuna waamuzi uwanjani kwenye soka la akina mama.

Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha tunapata waamuzi akina mama ili wasaidie katika soka hili? (Makofi)

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi. Naomba nijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Prof. Ndakidemi kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la soka la wanawake kwetu sisi ni kipaumbele. Nawapongeza wanawake wote Tanzania kwa jinsi ambavyo wamemwelewa Mheshimiwa Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan kwamba tunahitaji kushiriki na kushinda. Suala la makocha pamoja na ma-referee liko kwenye mpango kazi wetu kuhakikisha kwamba tunakuwa na ma-referee pia wa kutosha.