Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Antipas Zeno Mgungusi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza:- Je, kwa nini Makocha wa Mpira wa Miguu Tanzania hawafundishi nje ya nchi hata katika Ukanda wa Afrika Mashariki au Nchi za SADC?

Supplementary Question 1

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu ya Serikali. Nina maswali mawili ya nyongeza. La kwanza, hao makocha ambao amewataja, wamesoma Leseni A ya CAF mwaka 2016, mpaka leo TFF haijawapatia vyeti vyao, hali ambayo inawakwamisha kutafuta ajira nje ya nchi. Je, ni lini watapewa vyeti vyao?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili: Ni utamaduni wa nchi yetu kulinda ajira za ndani dhidi ya wageni mpaka pale itakapothibitika taaluma hiyo haipo hapa ndani. Hapa tuna makocha wengi ambao wapo mtaani hawana kazi, lakini wageni wamekuwa wakija kwa wingi sana kufundisha vilabu vyetu hata vile vya daraja la kwanza. Wenzetu wa Zambia na Namibia wameweka utaratibu kuwalinda makocha wazawa kwa maana ya kwamba, kufundisha ligi kuu ya kwao, mpaka uwe umefundisha timu ya Taifa huko ulikotoka: Je, Serikali ya Tanzania ina mpango gani kulinda walimu wa mpira wa ndani?

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa nafasi, naomba nijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Antipas Zeno, Mbunge wa Malinyi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, Mheshimiwa Antipas amependa kufahamu hatima ya makocha hawa ambao walipewa mafunzo mwaka 2016 chini ya TFF pamoja na CAF. Naomba niliarifu Bunge lako Tukufu kwamba jambo hili limekuwa likifuatiliwa kwa karibu na wenzetu wa TFF, na bahati nzuri miongoni mwa watu ambao walikuwa kwenye mafunzo haya ni pamoja na Katibu Mkuu wa TFF Kidau na jambo hili wamekuwa wakiwasiliana ni jinsi gani walimalize ili hawa makocha waweze kupata haki yao.

Swali la pili, alipenda kufahamu mkakati wa Serikali wa kuweza kuwalinda makocha wa ndani kwa sababu sasa tumeshaanza kuwazalisha. Sisi kama Wizara tunafahamu kwamba vijana wetu wanapokuwa na sifa lazima tuwalinde. Tuna mkakati wa Wizara yetu wa kukuza michezo wa mwaka 2021 mpaka 2031, miongoni mwa vitu ambavyo tunakwenda kuzingatia ni kuhakikisha tunatoa kozi kwa makocha wetu. Ndiyo maana hata sasa kozi inaendelea, zaidi ya nchi tatu zinashiriki. Watakapofuzu vijana zaidi ya 20 wa Kitanzania, maana yake wataendelea kupewa fursa, ahsante. (Makofi)

Name

Fatma Hassan Toufiq

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza:- Je, kwa nini Makocha wa Mpira wa Miguu Tanzania hawafundishi nje ya nchi hata katika Ukanda wa Afrika Mashariki au Nchi za SADC?

Supplementary Question 2

MHE. FATMA H. TOUFIQ: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa fursa niweze kuuliza swali la nyongeza. Nilipenda kufahamu: Nini mkakati wa Serikali wa kuwaandaa makocha wengi wanawake ili waweze kufanya ukocha hapa nchini na nje ya nchi? (Makofi)

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kwa niaba ya Waziri wa Utamaduni, Sanaa na Michezo, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Toufiq, Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, mikakati tuliyonayo pia ni kuhakikisha kwenye ile michezo yetu ya kipaumbele kwa Wizara ambayo tuna michezo sita ya kipaumbele kwa Taifa ni pamoja na kuhakikisha pia tunapata makocha wanawake. Kwa hiyo, jambo hili Mheshimiwa Toufiq tunalizingatia pia.

Name

Grace Victor Tendega

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI aliuliza:- Je, kwa nini Makocha wa Mpira wa Miguu Tanzania hawafundishi nje ya nchi hata katika Ukanda wa Afrika Mashariki au Nchi za SADC?

Supplementary Question 3

MHE. GRACE V. TENDEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuniona. Tumeona michezo mbalimbali ya wanawake wanafika mbele wanaenda hadi Kombe la Dunia: Ni nini mkakati sasa wa Serikali kuhakikisha kwamba michezo yote; Volleyball, Basketball na michezo mingine tunapata makocha wanawake ambao wanaweza wakazi-train hizi timu ili ziweze kufika mbali zaidi? (Makofi)

Name

Pauline Philipo Gekul

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Babati Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UTAMADUNI, SANAA NA MICHEZO: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Grace Tendega, Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara yetu tumedhamiria kwa dhati kuhakikisha kwamba tunanyanyua vipaji vya wanawake wa Kitanzania. Vile vile kwenye michezo ya kipaumbele mchezo wa mpira wa miguu wanawake upo na mchezo wa mpira wa pete upo. Kazi kubwa iliyopo mbele yetu ni kuhakikisha walimu wa michezo hiyo wanatokana na wanawake wenyewe. Mheshimiwa Grace utuamini, tunaendelea na kazi hiyo.