Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yahya Ally Mhata

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyumbu

Primary Question

MHE. YAHYA A. MHATA aliuliza: - Je, ni lini Serikali italeta Sheria ya kuruhusu halmashauri kutumia benki kama wakala wa ukopeshaji na ukusanyaji madeni?

Supplementary Question 1

MHE. YAHYA A. MHATA: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kupata majibu ya Serikali. Nina swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Serikali kwa kipindi hiki imesimamisha utoaji wa mikopo ili kupisha kuandaa utaratibu mzuri wa utoaji mikopo hiyo.

Je, Serikali haioni haja kuwa na mpango wa dharura wa kutoa mikopo wakati tunasuburi utaratibu huo mpya kwa sababu wananchi wnahitaji sana mikopo hiyo hasa kipindi hichi cha kilimo? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, lengo la Serikali kusitisha utoaji wa mikopo hii ilikuwa ni kuhakikisha kwamba fedha zinazotengwa kwa ajili ya mikopo ya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu zinawafikia walengwa lakini pia zinatumika kwa tija na kurejeshwa ipasavyo. Hiyo ndiyo ilikuwa changamoto kubwa iliyopelekea kusitisha utoaji wa mikopo hii.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hivyo nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inaendanalo hili jambo kwa kasi ili mapema iwezekanavyo utaratibu rasmi uwezekutolewa na mikopo ianze kutolewa kwa wananchi badala ya kuwa na utaratibu wa dharura ambao utakuwa hauna tija sana kwa sababu bado utakuwa na mapengo mengi. Kwa hiyo, nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba si muda mrefu sana Serikali itatoa utaratibu na mikopo ya 10% itaanza kutolewa kwa wananchi wetu, ahsante. (Makofi)