Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO K.n.y. MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza: - Je, ni malambo/mabwawa mangapi yatajengwa katika Halmashauri ya Itigi kwa ajili ya kunyweshea Mifugo?

Supplementary Question 1

MHE. ABEID R. IGHONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana. Pamoja na majibu mazuri ya Mheshimiwa Naibu Waziri, napenda kuuliza maswali mawili ya nyongeza. Hali ya upatikanaji wa maji katika Jimbo la Manyoni Magharibi ni mbaya, eneo lile ni kame. Pamoja na juhudi hizi za Serikali, sasa Naibu Waziri haoni umuhimu wa kuongeza kasi ya kupeleka mabwawa zaidi pamoja na majosho katika Jimbo la Manyoni Magharibi ili kuwasidia wakulima wetu pamoja na wafugaji ambao mifugo yao inapata tabu kwa kipindi cha kiangazi? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, katika Jimbo la Singida Kaskazini katika bajeti ya mwaka 2023/2024, Serikali ilitupatia miradi ya majosho manne katika Kijiji cha Minyenye, Ghalunyangu, Muhamo na Mangida. Kwa bahati mbaya fedha hazikuja kwa ajili ya kutekeleza miradi hii pamoja na kuwa wananchi tayari walishaanda upande wa nguvu kazi.

Je, sasa ni lini Serikali italeta fedha kwa ajili ya kukamilisha miradi hii ambayo inasubiriwa kwa hamu kubwa na wananchi? Ahsante. (Makofi)

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nianze na hili swali la kwanza la Mheshimiwa Mbunge kwamba, mabwawa ambayo yaliahidiwa kwenye bajeti ya mwaka 2023/2024. Kwanza nimwambie Mheshimiwa Mbunge kwamba, mwaka wa fedha wa bajeti bado haujaisha. Namhakikishia kwamba, jinsi ambavyo upatikanaji wa fedha utakavyokuwa unapatikana, tutakwenda kuyajenga hayo mabwaka kama ambavyo bwawa tulilokwishalikabidhi tayari limekwishajengwa katika jimbo lake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake la pili kuhusu kuongeza kasi ya ujenzi wa haya mabwawa, ni kweli kama nilivyokwisha jibu kwamba, tumeshakabidhi bwawa la kwanza na Serikali sasa inaendelea kutafuta fedha zingine kwa ajili ujenzi wa mabwawa mengine. Tunakiri kwamba, Wilaya ya Itigi ni miongoni wa wilaya kame ambazo zinahitaji kuongezewa mabwawa na majosho kwa ajili ya kuisaidia mifugo yetu iliyoko katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba, Serikali inaendelea kufuatilia na inaendelea kutafuta namna ambavyo inaweza kusaidia ujenzi wa mabwawa katika Wilaya hii ya Itigi, ahsante. (Makofi)

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO K.n.y. MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza: - Je, ni malambo/mabwawa mangapi yatajengwa katika Halmashauri ya Itigi kwa ajili ya kunyweshea Mifugo?

Supplementary Question 2

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nataka kuuliza ni lini sasa Serikali ina mpango wa kutekeleza ahadi ya Mheshimiwa Waziri Mashimba Ndaki, alipokuja kwenye Jimbo la Msalala na kuahidi bwawa la kunyweshea mifugo.

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahadi ya Mheshimiwa Waziri wa Mifugo, Mheshimiwa Mashimba Ndaki, Mheshimiwa Waziri wa Mifugo Mstaafu ambayo aliitoa katika Jimbo la Msalala, nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, ahadi za viongozi wote walizokwishazitoa tunazo kama Wizara. Tuna database muhimu ya ahadi hizo. Nimhakikishie, mara ambapo tutapata fedha kwa ajili ya utengenezaji wa mabwawa hayo tutakuja kujenga katika Jimbo lake la Msalala. (Makofi)

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. ABEID R. IGHONDO K.n.y. MHE. YAHAYA O. MASSARE aliuliza: - Je, ni malambo/mabwawa mangapi yatajengwa katika Halmashauri ya Itigi kwa ajili ya kunyweshea Mifugo?

Supplementary Question 3

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa nafasi. Wilaya ya Liwale tulipata shilingi milioni 400 kwa ajili ya kujenga bwawa pale Kijiji cha Kimambi lakini wale wataalamu badala ya kujenga bwawa walijenga Karo. Ni nini kauli ya Serikali juu ya ufisadi ule?

Name

Alexander Pastory Mnyeti

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Misungwi

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI: Mheshimiwa Mwenyekiti, concern ya Mbunge tumeshaipokea na tayari Wizara inajipanga kupeleka wataalam kwa ajili ya uchunguzi wa jambo hili. Mara tutakapojiridhisha kwamba kuna tatizo katika mradi huo tutachukua hatua stahiki kwa mujibu wa sheria za utumishi. (Makofi)