Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Jafari Chege Wambura

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Rorya

Primary Question

MHE. JAFARI W. CHEGE aliuliza:- Je, lini Serikali itafanya maboresho ya Sera ya Taifa ya Ardhi ya mwaka 1995?

Supplementary Question 1

MHE. JAFARI W. CHEGE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Spika, pamoja na kuendelea kwa maboresho ya Sera ya Taifa ya Ardhi ya mwaka 1995, nataka nijue Mheshimiwa Waziri, ni lini sasa mtaridhia kama Wizara kuhamisha Mabaraza ya Ardhi kutoka kwenye wizara kwenda kwenye mfumo wa kimahakama? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; ili kuongeza ufanisi na usimamizi katika sekta ya ardhi nchini, je, ni lini Serikali itaridhia na kukubali kuanzisha kwa mamlaka ya maendeleo ya ardhi nchini kama zilivyo mamlaka zingine kwa mfano RUWASA na taasisi nyingine, ili kuendelea kuimarisha usimamizi na uimara katika kutatua migogoro nchini? (Makofi)

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Jafari Wambura, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, moja, ni lini Mabaraza ya Ardhi yatahamishiwa kwenye mhimili wa Mahakama. Jambo hili lipo kwenye mchakato na linapitiwa na mamlaka mbalimbali ili kuona uwezekano wa namna ya kuhamisha mabaraza haya kuyarudisha kwenye mhimili wa Mahakama.

Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la kuunda chombo maalum cha kuendeleza na kusimamia ardhi nchini, Wizara yetu ipo kwenye mchakato wa kuanzisha kamisheni ya ardhi ambayo itasimamia mamlaka hii ya ardhi kwa maendeleo ya Watanzania hawa.