Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza: - Je, Serikali ipo tayari kufanya utafiti wa madini katika Kata ya KIA Jimbo la Hai?

Supplementary Question 1

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na ninashukuru kwa majibu mazuri ya Serikali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Kata ya KIA kumekuwa na viashiria vinavyoonesha kwamba, kuna Madini ya Tanzanite green na madini mengine na ikizingatiwa tuko ukanda mmoja na Arusha ambapo yanapatikana madini haya ya Tanzanite. Sasa ni lini, Serikali itafanya utafiti mahsusi kwenye madini ya aina hii ili tuweze kujiridhisha kama kweli yapo na tuweze kuyazalisha? (Makofi)

Swali langu la pili, kwa kuwa Serikali imebaini kwenye Kata ya Masama Rundugai kuna madini aina ya chokaa; je, Serikali ipo tayari kubainisha umahsusi wa eneo linalopatikana chokaa hiyo na kututafutia mwekezaji aanze kuvuna madini haya?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikianza na swali la kwanza la kuhusu utafiti. Tunao mpango kiongozi wa kuhakikisha tunalifanyia utafiti wa kina eneo kubwa zaidi la nchi yetu ya Tanzania na tumeligawa katika blocks sita kubwa, ikiwemo block ambayo inahusisha eneo la Mererani pamoja na Mkoa wa Kilimanjaro ikiwemo Wilaya ya Hai.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge ya kwamba, katika utafiti huu tutagusa eneo kubwa na kwa kuanzia mwaka huu wa fedha, tunaanza majaribio kupitia ndege nyuki katika eneo la Mererani, ili kuweza kubaini uwepo wa madini ambapo itakuwa imetapakaa katika maeneo ya Wilaya ya Hai. Hivyo taarifa za awali pia zitakuwa ni sehemu ya kuongoza wananchi wa Wilaya ya Hai katika eneo hili la uchimbaji wa madini.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza: - Je, Serikali ipo tayari kufanya utafiti wa madini katika Kata ya KIA Jimbo la Hai?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Kwa kuwa, Mheshimiwa Naibu Waziri alipotembelea Machimbo ya Nyakabangala katika Jimbo la Isimani, aliwaahidi kuwaleta watafiti na kuwapatia vifaa ili wananchi waweze kuchimba kwa uhakika zaidi.

Je, ni lini sasa ile ahadi itatimia? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli, hivi sasa tumeanza kuwatawanya sana wataalam wetu kupita maeneo tofauti tofauti ya nchi, na lengo letu ni kuhakikisha kwamba tunawaongoza wachimbaji waweze kuchimba katika kanuni na taratibu za kisheria pasipo kubahatisha. Kwa hivi sasa tumeanza kusambaza pia mitambo yetu ya uchorongaji ambayo itawasaidia wachimbaji wadogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Kanda ya Mikoa ya Iringa, Njombe pamoja na Mkoa wa Mbeya tayari tuna mtambo ambao uko kule. Tutatoa maelekezo kwamba uwafikie pia na wachimbaji wa eneo hilo ambalo Mheshimiwa Mbunge amelisema ili nao waweze kupata huduma. (Makofi)

Name

Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE aliuliza: - Je, Serikali ipo tayari kufanya utafiti wa madini katika Kata ya KIA Jimbo la Hai?

Supplementary Question 3

MHE. NUSRAT S. HANJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, ni lini Serikali itawapa wachimbaji wadogo eneo namba moja, Kata ya Mang’onyi, Jimbo la Singida Mashariki, ambao wameondolewa tangu mwaka 2015?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA MADINI: Mheshimiwa Mwenyekiti, katika eneo ambalo amelitaja Mheshimiwa Mbunge, nitakwenda kufanya ziara eneo hilo kwa sababu nina ziara katika eneo hilo. Pia, moja kati ya jukumu langu kubwa ni kwenda kuzungumza nao na hasa katika kuhakikisha kwamba tunaendelea kuwapatia maeneo wachimbaji wadogo kwa sababu, haya ni maelekezo ya Mheshimiwa Rais.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge ya kwamba nitafika mwenyewe katika maeneo hayo na kuona namna ya kuweza kutoa utaratibu mzuri kama ambavyo tumefanya katika Mlima wa Sekenke na maeneo mengine ya Sekenke ambayo tulitoa leseni kwa ajili ya wachimbaji wadogo.