Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Anatropia Lwehikila Theonest

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ANATROPIA L. THEONEST aliuliza: - Je, Wanawake wangapi wamekuwa Wabunge wa Majimbo na Madiwani katika chaguzi tatu mfululizo zilizopita?

Supplementary Question 1

MHE. ANATROPIA L. THEONEST: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza. Kutokana na majibu aliyonipatia ni wastani wa wanawake 24 huwaguliwa kila baada ya Uchaguzi Mkuu. Kwa hiyo, naona kwamba ongezeko ni dogo wanawake 24 kila baada ya miaka mitano ni wachache sana kuwakulisha licha ya Serikali kuridhia mikataba mbalimbali ya kimataifa kuongeza ushiriki wa wanawake. Swali langu ni mkakati gani mahususi unaopaswa kuwa revised ili kuongeza idadi ya wanawake kwenye siasa? (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili. Mkakati gani wa Serikali wa kubadilisha Political Parties Act ili kuweka kifungu kitakachovilazimisha vyama vya siasa kuwa na idadi maalumu ya wanawake watakaokuwa wagombea kwenye chaguzi mbalimbali kwenye hii nchi. (Makofi)

Name

Ummy Hamisi Nderiananga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA WAZIRI MKUU SERA, BUNGE NA URATIBU (MHE. UMMY H. NDERIANANGA): Mheshimiwa Naibu Spika ahsante. Kwanza nisema Serikali inatambua na kuthamini sana sana ushiriki wa wanawake katika shughuli za kisiasa na lakini na maeneo mengine. Niseme tu katika eneo hili mkakati uliopo ndani ya msajili wa vyama vya siasa ni kuendelea kutoa elimu kwa makundi mbalimbali ya wanawake kuendelea kujiamini na waweze kujiandaa kugombea nafasi hizo. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, namba mbili, tutaleta Bungeni mabadiliko ya Sheria ya vyama vya siasa ili kuvitaka vyama sasa kuwa na Sera ambayo itaweka mwongozo mahususi wa kujumuisha wanawake kwenye kugombea nafasi mbalimbali. Kwa hiyo, niwaondoe shaka wanawake wenzangu Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anawajali anawathamini na tutaendelea kufanya vizuri kwenye eneo hili la kuhakikisha tunawajumuisha wanawake kwenye ngazi zote za maamuzi, ahsante sana. (Makofi)