Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Godwin Emmanuel Kunambi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlimba

Primary Question

MHE. GODWIN E. KUNAMBI aliuliza: - Je, lini Serikali itarejesha eneo lililokuwa linamilikiwa na RUBADA kwa wananchi wa Utengule – Mlimba?

Supplementary Question 1

MHE. GODWIN E. KUNAMBI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, kwa kuwa Serikali imekiri kwamba hapo awali shamba hili lilikuwa linamilikiwa na Kijiji cha Utengule, na kwa kuwa wananchi hawa kwa nia njema kabisa waliridhia shamba hili litwaliwe na Serikali kwa ajili ya uwekezaji, lakini sasa yapata miaka 13 hamna uwekezaji wowote: Swali langu, ni lini Serikali itakabidhi shamba hili kwa wananchi wa Kata ya Utengule? Ahsante. (Makofi)

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, napenda kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Kunambi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza kabla ya kutoa maelezo ya majibu, nampongeza sana Mheshimiwa Kunambi na wananchi wa Mlimba kwa kumpata kiongozi ambaye ni mfuatiliaji, ana hamasa ya kweli kwa maendeleo ya wananchi wake. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa ujumla, kama nilivyojibu kwenye swali la msingi ni kwamba Serikali kupitia Wizara ya Fedha na Mipango, wanaendelea na mchakato wa jinsi ya kuharakisha maamuzi ya shamba hili aidha kurudishwa sehemu ya shamba hilo kwa wananchi na ile sehemu ambayo imewekwa kwa ajili ya uwekezaji mkubwa wa bwawa letu la Mwalimu Nyerere, nalo kuangaliwa katika umbo zima la namna ya kulilinda.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimpe tu comfort Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali itatoa maamuzi kwa haraka ili kuharakisha manufaa yatakayotokana na matumizi ya ardhi hii ambayo kimsingi haijatumika ipasavyo kwa muda mrefu, ahsante.