Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU aliuliza: - Je, Serikali inatoa kauli gani juu ya malipo ya fidia kwenye miradi ya barabara za TANROADS zinazopita kwenye makazi ya watu Kibamba?

Supplementary Question 1

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, pamoja na majibu mazuri ya jumla ya Serikali, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza; ipo barabara ya Makabe – Msakuzi kuelekea Mpiji Magoe ambayo ina sifa hizo ambazo amezizungumza na sasa barabara hii imeanza kutengenezwa, wananchi bado wako kwenye sintofahamu kama watalipwa fidia au lah! Je, ni ipi kauli ya Serikali kwenye barabara hii. (Makofi)

Swali la pili, ipo barabara ya Victoria au inaitwa Mbezi Shule – Mpiji Magohe, kilometa 9.5; ni barabara ambayo ni ahadi ya Mheshimiwa Rais lakini ipo ndani ya bajeti kwa kipindi cha miaka miwili, lakini ina watu takribani 50,000 ambao ni wengi zaidi hata ya majimbo mengine.

Je, ni lini Serikali itaanza kujenga barabara hii kwa kiwango cha lami? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge wa Kibamba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Makabe – Msakuzi, ni barabara ambayo tangu kuwepo kwake iko chini ya TANROADS na wakati ule ilikuwa chini ya ujenzi Mkoa wa Dar es Salaam, TANROADS ilipoanzishwa ikawa imehamia moja kwa moja TANROADS. Kwa hiyo, kwa wananchi ambao watakuwa ndani ya mita 22.5 kutoka katikati hawatastahili kulipwa, ila pale ambapo tutakwenda 7.5 wananchi ambao wako katika barabara hii watalipwa fidia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu barabara ya Victoria, pale kuna barabara mbili, kuna barabara ya Kibamba Shule – Magoe Mpiji na Victoria kwenda Magoe Mpiji. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Kibamba Shule tayari imeshaanza kujengwa kwa awamu, pia, ndiyo tunayoitegemea itakuwa outer ring road ya Mkoa wa Dar es Salaam na usanifu unaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Victoria imekuwa ni barabara ambayo inahitajika sana hasa baada ya kuanzisha stendi ya Magufuli, tunavyoongea sasa hivi Mhandisi Mshauri yuko field kufanya usanifu na tunategemea baada ya kukamilisha kwa bajeti ambayo tunaiandaa iweze kuingia ili ijengwe kwa kiwango cha lami, ahsante. (Makofi)