Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tabasamu Hamisi Hussein Mwagao

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Sengerema

Primary Question

MHE. TABASAM H. MWAGAO aliuliza:- Je, lini Serikali itakarabati viwanda vya kuchambua pamba vya Nyakarilo, Nyamirilo na Buyagu vilivyopo Sengerema?

Supplementary Question 1

MHE. TABASAM H. MWAGAO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru.

Mheshimiwa Spika, ni kwamba kwa kuwa viwanda vya Nyakarilo, Buyagu na Nyamirilo havifanyi kazi leo, takribani miaka 21. Huu mpango unaopangwa na Serikali hauoni kama ndio unafifisha zao letu la pamba kwa kuwa Chama Cha Mapinduzi katika Ilani yake imesema ya mwaka 2025 tunakwenda kuzalisha pamba tani milioni moja na tutaboresha viwanda. Leo tunakwenda mwaka wa tatu hakuna kiwanda chochote katika Wilaya ya Sengerema kilichoboreshwa.

Mheshimiwa Spika, haoni kwamba Serikali tayari tena ina mpango wa kupingana na Ilani ya Chama Cha Mapinduzi? Swali la kwanza.

Mheshimiwa Spika, swali letu la pili ni kwamba kwa kuwa, viwanda hivi vipo na vinasimamiwa na vyama vya ushirika chini ya Wizara ya Kilimo na ninyi Wizara ya Viwanda ni sehemu ya Serikali. Mko tayari kufuatana na mimi kwenda Sengerema kukagua hivyo viwanda na kuwaeleza wananchi, lini mtaviboresha?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana, ni kweli kabisa kwamba, kumekuwa na changamoto katika sekta ya viwanda hasa viwanda vya pamba katika maeneo mengi kwamba ni viwanda vya siku nyingi na hivyo vimechakaa, na kama alivyosema Mheshimiwa Tabasam, ni kweli Serikali imeshaweka mkakati maalum.

Mheshimiwa Spika, kwanza changamoto iliyokuwepo kabla ilikuwa ni changamoto ya malighafi kwenye viwanda ambavyo vinafanya kazi, lakini sasa kwa sababu ya uzalishaji mkubwa ambao Mheshimiwa Rais ameshaweka fedha nyingi kwenye sekta ya kilimo, tunaamini kweli kutakuwa na uzalishaji mkubwa kulingana na Ilani ya Chama Cha Mapinduzi ambayo sasa pamba hii inatakiwa kulishwa kwenye viwanda vyetu.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, sisi kama Wizara ya Viwanda na Biashara, lakini kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo tutahakikisha tunapitia na kuona viwanda hivi viaenda kufufuliwa na kufanya kazi.

Mheshimiwa Spika, lakini kuhusu ziara, ni kweli nitafanya ziara ili nijionee na mimi kama Wizara ya Viwanda tunaoratibu viwanda, lakini kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo, ili tuhakikishe sasa mkakati tuliouweka wa kupata mitaji kupitia Benki ya Kilimo, viwanda hivi viweze kufufuliwa ili wananchi wa Sengerema na wengine wanaofanya kazi waweze kunufaika na uwepo wa viwanda hivi, lakini pia kuchochea kilimo cha pamba, nakushukuru.