Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. NDAISABA G. RUHORO aliuliza: - Je, lini Serikali itaanza ujenzi wa mradi mkubwa wa bilioni 41 wa kupeleka maji safi Ngara?

Supplementary Question 1

MHE. NDAISABA G. RUHORO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Naomba kwanza turekebishe taarifa kidogo. Jimbo la Ngara linaitwa Jimbo la Ngara na siyo Jimbo la Ngara mjini, naomba turekebishe taarifa.

Mheshimiwa Spika, nina maswali mawili ya nyongeza. Kwa kuwa kwenye Taarifa ya Mheshimiwa Naibu Waziri amekiri kwamba wananchi 170,000 wa Ngara Mjini, Kanazi, Kidimba, Nyamiaga na Murukulazo hawana huduma ya maji; na kwa kuwa visima viwili vya milioni 600 vinavyojengwa sasa haviwezi kutekeleza mahitaji ya maji ya wananchi wote hawa.

Je, Serikali ipo tayari kuanza kujenga mradi huu mkubwa wa bilioni 41, kwa kutumia mapato ya ndani yanayotoka Serikali, wakati ikiendelea kutafuta fedha kutoka nje?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; hivi karibuni Mheshimiwa Waziri wa Maji alifika Ngara na kuahidi kumlipa Baraka Makogwe hela yake ya fidia ya shilingi milioni 104, ambye bwana huyu ardhi yake uimechukuliwa na Wizara ya Maji nae neo lake limejengwa tenki kubwa la maji na huyu bwana hajalipwa kwa muda mrefu sana;

Je, ni lini, Serikali italipa fedha ya bwana Baraka Makogwe? Ahsante.

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ndaisaba, Mbunge wa Ngara kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusu kuweza kutumia mapato ya ndani kuanza mradi wa bilioni 41; Mheshimiwa Mbunge ushauri umepokelewa kwa sababu tumekuwa tukifanya hivi kwenye miradi mingi naamini na hili nalo tutalitupia jicho la ziada.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na kulipa fidia, Mheshimiwa Mbunge ahadi ni deni kwa sabbau Mheshimiwa Waziri mwenye dhamana ameweza kuahidi; nikuhakikishie huyu mwananchi atalipwa fidia kadiri ambayo inatakikana.