Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Emmanuel Lekishon Shangai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngorongoro

Primary Question

MHE. EMANNUEL L. SHANGAI aliuliza:- Je ni sheria ipi inawaruhusu Watumishi wa TANAPA, TAWA na NCAA kutoza mifugo shilingi 100,000 pindi iingiapo hifadhini?

Supplementary Question 1

MHE. EMANNUEL L. SHANGAI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa majibu ya Mheshimiwa Naibu Waziri. Nashukuru kwamba, ameshindwa kuthibitisha kwamba mifugo inatakiwa kutozwa shilingi 100,000 kwa kichwa cha ng’ombe wanapoingia hifadhini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa wafugaji wengi Tanzania wamekuwa wakitozwa shilingi laki moja kwa kichwa cha ng’ombe wanapoingia hifadhini na kuna wananchi wametozwa mpaka shilingi milioni sabini kwa wakati mmoja. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nina maswali mawili ya nyongeza. Swali langu la kwanza nini kauli ya Serikali kwa Watumishi wa TANAPA, TAWA pamoja na NCAA ambao wamekuwa wakitoza shilingi laki moja kwa kichwa cha ng’ombe?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili je, Serikali ipo tayari kurejesha fedha za wananchi ambazo wametozwa zaidi ya shilingi milioni kumi? (Makofi)

Name

Dunstan Luka Kitandula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mkinga

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Shangai kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika jibu langu la msingi nimeonyesha sheria inataka nini? Lakini sambamba na eneo hilo niseme tu kwamba, kosa la kuingiza mifugo kwa mujibu wa Sheria ya Hifadhi ya Taifa lipo pia katika Kanuni Na. 7(1) ya Kanuni za Hifadhi ya Taifa GN Na. 255 ya mwaka 1970 kama ilivyorekebishwa ambavyo Kifungu kinazuia kuingiza mifugo Hifadhini na adhabu ya kosa kuingiza mifugo ni kwa kila mfugo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nchi yetu, Serikali yetu ina heshimu Utawala wa Sheria na chombo ambacho kimekasimiwa kutafsiri sheria pale ambapo kuna changamoto ni Mahakama zetu. Nitoe rai kwamba wale wote wanaoona kwamba imepita hukumu ambayo wanaona haikuwatendea haki basi twende kwenye mfumo wa kisheria ili sheria iweze kutoa haki.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu hili la kurejesha bado narudi pale pale yeyote anayehisi kwamba hakutendewa haki tuzitumie Mahakama zetu ili haki iweze kutendeka. (Makofi)