Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. RITTA E. KABATI aliuliza Je Serikali inampango gani wa kupandisha Chuo Kikuu Kishiriki cha Mkwawa kuwa Chuo Kikuu kamili?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ili niulize maswali mawili. Kwa kuwa Chuo hiki tayari kina technical na academics staff zaidi ya 231 wakiwemo zaidi ya Maprofesa 70. Pia huduma mbalimbali toshelezi wapo mpaka wanafunzi wenye mahitaji maalum. Ni kwanini sasa Serikali isitoe kibali chuo hiki kijitegemee na muda maalum wa uwangalizi wa vigezo hivyo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili, kwa kuwa Mheshimiwa Rais wetu alipokuja katika Mkoa wa Iringa alipoongea na Wazee aliahidi kutoa fedha kupitia Waziri wa Fedha Dkt. Mwigulu kwa ajili ya ujenzi wa majengo mbalimbali ya chuo.

Je, ni lini sasa Serikali itatimiza ile ahadi ya Mheshimiwa Rais kwa sababu hiki Chuo kinatakiwa kiwe fanisi katika Nyanda za Juu Kusini? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ritta Kabati kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika ni kweli Chuo chetu kina Watumishia hao aliowataja Mheshimiwa Mbunge zaidi ya 231 wakiwepo Maprofesa hao 70 lakini kwa vigezo hivi siyo vigezo pekee ambavyo vinatumika kwa ajili ya kupandisha hadhi chuo hiki na naomba nimpe taarifa tu Mheshimiwa Mbunge, Maprofesa hawa waliopo wengi wao ni wale ambao wameazimwa kutoka katika Chuo Mama kile Chuo Kikuu cha Dar es salaam. Kipekee wale ambao walioajiriwa na Chuo Kikuu cha Mkwawa pale kwa upande wa Maprofesa hatuna hata Profesa mmoja ambaye ameajiriwa kama Mwajiriwa wa chuo kile pale.

Mheshimiwa Spika, nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwanza tumebeba ushauri wake, lakini naomba nimuhakikishie Serikali hivi sasa tumepata Mradi wa HEET ambao unakwenda kusomesha Maprofesa na Maprofesa wasaidizi zaidi ya 100 ambao tutahakikisha sasa baada ya mafunzo yao hawa, chuo hiki kinaweza kupandishwa hadhi kuwa Chuo Kikuu kinacho jitegemea.

Mheshimiwa Spika, katika eneo la pili la upande wa majengo. Tumshukuru sana Mheshimiwa Rais lakini tumshukuru vilevile Waziri wa Fedha kwa upande wa mapato yetu ya ndani mwaka uliopita wa fedha na mwaka huu wa fedha tumeweza kutenga fedha kwa ajili ya ujenzi pale wa majengo na mpaka hivi ninavyozungumza Wakandarasi wawili wako pale site ambae ni SUMA JKT pamoja na Salimu Construction. Salimu Construction anafanya ujenzi pale wa hostel na SUMA JKT wanafanya ujenzi wa library.

Mheshimiwa Spika, vilevile katika Mradi wetu wa HEET tumeishapeleka pale jumla ya dola za kimarekani milioni nane kwa ajili ya kuongeza miundombinu pamoja na majengo mbalimbali kukifanya Chuo kile kiwe na hadhi ya kupandishwa kuwa Chuo Kikuu kamili, nakushukuru.