Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Leah Jeremiah Komanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Meatu

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza:- Je, kwa nini ujenzi wa Skimu ya Umwagiliaji Kijiji cha Mwagwila haukamiliki ingawa Serikali imetuma fedha nyingi?

Supplementary Question 1

MHE. LEAH J. KOMANYA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu ya Serikali. Kwa kuwa mradi huu ulitumia shilingi bilioni 1.2 na haukukamilika; je, Serikali haioni haja ya kuangalia kilichosababisha kutokukamilika ikiwemo halmashauri kutohusishwa kusimamia? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili kwa kuwa Wilaya ya Meatu hatujanufaika na Miradi ya Umwagiliaje je, Serikali pia ipo tayari kutupatia eneo la umwagiliaji katika Kata ya Mwamalole na Mwabuzo eneo moja ambalo tumelipa kipaumbele kama wilaya? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba tu nimuhakikishie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba pamoja na changamoto ambazo zilijitokeza awali na mapendekezo ambayo ameteyatoa sasa hivi tu miradi yote tunahakikisha kwamba inashirikisha watu wote ikiwemo halmashauri, Wabunge wa maeneo husika pamoja na Sekretarieti za Mikoa ili kuhakikisha kunakuwa na ufanisi katika kutekeleza. Kwa hiyo, tumelipokea hilo jambo na tutalifanyia kazi na hata hivyo karibuni tulikaa na Wabunge kuanisha kwenye maeneo ya miradi hiyo kuona namna gani watashiriki katika miradi yao.

Mheshimiwa Spika, la pili, kutoa kipaumbele katika maeneo ambayo ameyataja hapa ikiwemo Mwamalole. Kata ya Mwamalole nimwambie tu Mheshimiwa Mbunge kwamba, Serikali ya Dkt. Samia Suluhu Hassan imepanga kwamba maeneo yote yanayofaa kwa ajili ya umwagiliaji tutayafikia na tutajenga miradi kwa ajili ya Skimu za Umwagiliaji na Mabwawa, ahsante sana. (Makofi)

Name

Anna Richard Lupembe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nsimbo

Primary Question

MHE. LEAH J. KOMANYA aliuliza:- Je, kwa nini ujenzi wa Skimu ya Umwagiliaji Kijiji cha Mwagwila haukamiliki ingawa Serikali imetuma fedha nyingi?

Supplementary Question 2

MHE. ANNA R. LUPEMBE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwakunipa nafasi niulize swali. Naomba niulize swali moja ni lini Skimu ya Usense itakamilika Kata ya Ulurwa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba tu nimuhakikishie Mheshimiwa Anna Lupembe kwamba kwa kuwa ujenzi unaendelea. Sisi tutakachohakikisha ni kum-push Mkandarasi aweze kukamilisha kwa wakati mradi huo kama ulivyopanga, ahsante.