Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Omar Issa Kombo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wingwi

Primary Question

MHE. OMAR ISSA KOMBO aliuliza:- Je, Serikali inazingatia vigezo gani kugawa fedha za Mfuko wa Jimbo?

Supplementary Question 1

MHE. OMAR ISSA KOMBO: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nampongeza Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri, lakini naomba niulize maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni lini Serikali ilifanya tathmini kwa kuzingatia vigezo hivi sambamba na mgawanyo wa fedha za majimbo?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, tunashuhudia baadhi ya majimbo yakipata fedha kidogo ukizingatia kwamba vigezo alivyovieleza Mheshimiwa Waziri ni vikubwa zaidi ukilinganisha na Majimbo mengine na hata hali ya umaskini ni kubwa zaidi. Mfano mzuri ni Jimbo langu la Wingwi: Je, Serikali haioni iko haja ya kufanyia tathmini vigezo hivi, kwa kuzingatia sensa ya mwaka 2022? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, ni kwamba Serikali inafanya tathmini ya vigezo hivi mara kwa mara ili kuhakikisha kwamba vinakidhi uhitaji wa fedha za Mfuko wa Jimbo katika Majimbo yetu na pia kuona namna nzuri ya kuendelea kuboresha formula za hivi vigezo ili kuweza kutoa fedha kwa ajili ya maendeleo ya Mfuko wa Jimbo kwa ufanisi mkubwa zaidi.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali itaendelea kufanya tathmini mara kwa mara, na mara itakapoona kuna maeneo ambayo vigezo vinahitaji kuongezwa au kupitiwa upya, basi suala hilo litafanyika.

Mheshimiwa Spika, pili, ni kweli kwamba fedha za Mfuko wa Jimbo zinatofautiana kutoka Jimbo moja na Jimbo lingine kwa kuzingatia vigezo hivi. Kama nilivyosema, asilimia 45 ya idadi ya watu katika Jimbo husika; kwa hiyo, Majimbo yenye idadi kubwa ya watu automatically yatakuwa na fedha nyingi zaidi, lakini kiwango cha umaskini kwa asilimia 20 pia na ukubwa wa eneo la kijiografia kwa asilimia 10, ahsante.