Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tunza Issa Malapo

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakarabati Jengo la OPD na kujenga uzio katika Kituo cha Afya Likombe - Mtwara Mikindani?

Supplementary Question 1

MHE. TUNZA I. MALAPO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru; jengo ambalo linatumika sasa hivi kama OPD ni jengo la zamani na limechakaa. Kituo kile kimekuwa kikihudumia wagonjwa wengi sana. Mimi nataka kujua, kwa kutenga shilingi milioni 70 kwa mwaka, maana yake tutachukua muda mrefu kukamilisha jengo lile.

Kwa nini Serikali Kuu isipeleke fedha katika kituo hiki ili waweze kujenga OPD ya kisasa ambayo itaendana na mahitaji yaliyopo? (Makofi)

Swali langu la pili, hoja ya uzio sijajibiwa kabisa bado naendelea kuuliza, kuna mkakati gani wa kujenga uzio katika kituo kile cha afya ili kulinda mali za hospitali pamoja na watu ambao wanahudumiwa pale? Nakushukuru. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Tunza Malapo, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali inatambua umuhimu wa kuwa na miundombinu bora ya kutoa huduma za afya katika vituo vyetu. Ndiyo maana mwaka 2017/2018, Serikali ilipeleka shilingi milioni 500 kwa ajili ya kujenga majengo matano. Tunafahamu kwamba Jengo la OPD ni chakavu na la siku nyingi na tumeanza na shilingi milioni 70 kwenye bajeti ijayo, mwaka 2024/2024. Hii haimaanishi kwamba hatutapeleka fedha nyingine. Kwa hiyo, naomba nikuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, huo ni mwanzo tu wa fedha za mapato ya ndani, wakati huo Serikali Kuu inatafuta fedha kwa ajili ya kukamilisha jengo hilo mapema iwezekanavyo ili liweze kutoa huduma kwa wananchi. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili kuhusiana na uzio, kupanga ni kuchagua. Kwa sababau tuna changamoto ya majengo ya msingi ya kutoa huduma, ni vema tukakamilisha kwanza majengo yale, yaanze kutoa huduma kwa wananchi lakini baadaye tutafuata na hatua ya uzio, ahsante. (Makofi)

Name

Anne Kilango Malecela

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Same Mashariki

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakarabati Jengo la OPD na kujenga uzio katika Kituo cha Afya Likombe - Mtwara Mikindani?

Supplementary Question 2

MHE. ANNE K. MALECELA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Kwanza nianze kuishukuru Serikali ya Chama cha Mapinduzi kwa kunipa vituo vya afya viwili, Kituo cha Afya cha Mtii na Kituo cha Afya cha Miamba. Naomba kuiuliza Serikali kwamba, hivi vituo vya afya vimekamilika na vimeshaanza huduma.

Je, Serikali mna mpango gani wa vituo vya afya vyote hivi viwili kujengewa jengo la kuhifadhi maiti kwa sababu, hivi vituo vya afya vyote viwili viko milimani sana? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, nampongeza Mheshimiwa Mama Anne Kilango Malecela kwa namna ambavyo amefuatilia sana ubora wa huduma katika vituo vyake vya afya, vikiwemo vituo hivi viwili. Nimhakikishie kwamba baada ya kukamilisha majengo yale kuanza kutoa huduma kwa wananchi, tunaendelea na ujenzi wa miundombinu mingine ambayo haijakamilika yakiwemo majengo ya kuhifadhia maiti. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba lipo kwenye pipeline na litafanyiwa kazi, ahsante. (Makofi)

Name

Ally Mohamed Kassinge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kusini

Primary Question

MHE. TUNZA I. MALAPO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itakarabati Jengo la OPD na kujenga uzio katika Kituo cha Afya Likombe - Mtwara Mikindani?

Supplementary Question 3

MHE. ALLY M. KASSINGE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa nafasi ya swali la nyongeza. Kata ya Likawage katika Jimbo la Kilwa Kusini haina kituo cha afya na ipo mbali kutoka katika maeneo ya kutolea huduma, na Mheshimiwa Naibu Waziri alishatoa maelekezo kwa Mkurugenzi aandike andiko ili litumwe Ofisi ya Rais, TAMISEMI. Andiko hilo tayari limekamilika, sasa tunataka kupata commitment ya Serikali, lini Kituo cha Afya Likawage kitajengwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Kassinge. Ni kweli alishafuatilia mara kadhaa Ofisi ya Rais, TAMISEMI kuhusiana na ujenzi wa kituo cha afya katika kata hiyo na tayari Mkurugenzi alishawasilisha andiko ambalo tuna makadirio ya gharama zinazohitajika kwa ajili ya ujenzi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nimhakikishie, kwa sababu tayari ameshaleta kama kipaumbele na katika mwaka ujao wa fedha Mheshimiwa Rais wetu Dkt. Samia Suluhu Hassan ameshatupa idhini ya kutenga bajeti ya vituo vya afya kila jimbo na katika Jimbo lake la Kilwa Kusini tutahakikisha tunapeleka fedha kwa ajili ya kituo hiki cha afya, ahsante. (Makofi)