Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Edwin Enosy Swalle

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga barabara ziendazo maeneo ya mazao ya kimkakati kama chai, kupitia mradi wa Agri-Connect - Lupembe?

Supplementary Question 1

MHE. EDWIN E. SWALLE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, nitumie nafasi hii kuishukuru sana Serikali kwa kutukumbuka watu wa Lupembe kupata barabara ya Agri-Connect. Sasa, hii Barabara ya Lupembe – Kanikelele – Ukalawa ambayo ni Kilometa 18.5 inaishia nyuma kidogo ya Makao Makuu ya Kata ya Ukalawa, umbali kama wa Kilometa moja tu kwenye Makao Makuu ya Kata ya Ukalawa yenyewe.

Je, Serikali haioni haja ya kuongeza hii Kilometa moja ili wafikishe pale Makao Makuu ya Kata ya Ukalawa yenyewe? (Makofi)

Swali langu la pili, ziko barabara kwa mfano ya pale Lupembe Jimboni, kupita kwa Mzee Msambwa kwenda Idamba, kwenda mpaka Mfiriga. Ni lini barabara hii na yenyewe itafanyiwa usanifu na kuanza ujenzi wa lami? Ahsante. (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Swalle, swali lake la kwanza hili la kilometa moja hii ya nyongeza katika zile kilometa 18.5 ili kuweza kufika katika Makao Makuu ya Kata ya Ukalawa, nimtoe mashaka Mheshimiwa Swalle kwamba, mradi huu wa Agri-Connect upo katika Mikoa ya Iringa, Njombe, Mbeya pamoja na Songwe. Hivyo basi, katika usanifu wa awamu inayofuata nitahakikisha kwamba na hicho kipande pia kinaweza kumalizika kuweza kufika katika Makao Makuu ya Kata ya Ukalawa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda kwenye swali lake la pili la usanifu kwa barabara nyingine ambazo amezitaja. Kama ambavyo nimemjibu swali lake la nyongeza la kwanza, katika hatua inayofuata Serikali itaangalia kwa sababu mradi huu bado upo, ni kweli wanazalisha sana chai katika Jimbo lake kule la Lupembe, Serikali itaangalia pia barabara hizi ambazo zimesalia ili ziweze kuweka katika mipango inayofuata. (Makofi)

Name

Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga barabara ziendazo maeneo ya mazao ya kimkakati kama chai, kupitia mradi wa Agri-Connect - Lupembe?

Supplementary Question 2

MHE. JEREMIAH M. AMSABI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, kwa ajili ya kuimarisha shughuli za kiuchumi na kijamii, je Serikali ina mpango gani wa kufanya marekebisho katika barabara za Kata ya Nyamoko, Kisangura, Tarafa ya Ngoreme na Tarafa ya Ikorongo? Ahsante.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu swali la nyongeza la Dkt. Mrimi, kwanza kuhusu hili la marekebisho, kama ambavyo tulizungumza hapa awali katika Bunge hili ambalo linaendelea kwamba, Serikali ilikuwa katika mchakato wa kuhakikisha TARURA inaletewa fedha ya dharura haraka.

Mheshumiwa Mwenyekiti, tathmini imefanyika kote nchini, tathmini ile ilikamilika mwisho wa mwezi Januari mwaka huu wa 2024, ikiwemo kutoka kule kwa Mheshimiwa Mrimi, hivyo basi fedha ile ambayo itapatikana itaenda katika maeneo yale kuweza kuanza kurekebisha barabara zote korofi, ikiwemo kule Jimboni kwa Mheshimiwa Mrimi.

Name

Justin Lazaro Nyamoga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilolo

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga barabara ziendazo maeneo ya mazao ya kimkakati kama chai, kupitia mradi wa Agri-Connect - Lupembe?

Supplementary Question 3

MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kupitia Mradi wa Agri-Connect tulikuwa tumeomba Kilometa 15 ambazo zimo tayari kwenye bajeti ya Agri-Connect zijengwe kutoka Kilolo hadi Kidabaga ambapo ndiko shamba la chai lilipo. MHE. JUSTIN L. NYAMOGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Kupitia Mradi wa Agri-Connect tulikuwa tumeomba Kilometa 15 ambazo zimo tayari kwenye bajeti ya Agri-Connect zijengwe kutoka Kilolo hadi Kidabaga ambapo ndiko shamba la chai lilipo.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli kama anavyosema Mheshimiwa Nyamoga kwamba, mradi huu ulipoanza (Agri-Connect) Mkoa wa Iringa ulikuwa ni Mkoa wa kwanza kabisa kuanza utekelezaji. Vilevile, niliarifu Bunge lako Tukufu kwamba, Mheshimiwa Nyamoga alikuwa beneficiary wa kwanza kabisa wa ujenzi wa barabara hizi za Agri-Connect katika Jimbo lake. Hivyo basi, Serikali pia italiangalia hili la barabara ya Kilolo kwenda Kidabaga ambapo kuna uzalishaji mkubwa wa chai katika awamu ambayo inafuata kama nilivyomjibu Mheshimiwa Swalle ili kuziweka katika mpango na barabara hizi ziweze kujengwa. (Makofi)

Name

Flatei Gregory Massay

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Vijijini

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kujenga barabara ziendazo maeneo ya mazao ya kimkakati kama chai, kupitia mradi wa Agri-Connect - Lupembe?

Supplementary Question 4

MHE. FLATEI G. MASSAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, Barabara ya Orbesh ambayo inatoka kwenye Kata yako kuja Bashneti na kwenda mpaka Haiderere iliahidiwa na Katibu Mkuu kujengwa na sasa hivi hali ni mbaya.

Je, ni lini TARURA itakwenda kujenga barabara ile ili wakulima wapate nafuu ya kuleta mazao yao?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nimemsikia Mheshimiwa Flatei akiuliza kwamba barabara hii inaanzia kwenye, Jimboni kwako Kata yako ya Orbesh na kuelekea Bashneti ambako anatoka yeye Mheshimiwa Flatei. Nitakaa na Mheshimiwa Flatei ili kuona ni namna gani TARURA, Eng. Bwaya, Meneja TARURA Mkoa wa Manyara pamoja na timu yake walivyojipanga katika kuanza utekelezaji wa matengenezo ya barabara hii mara moja. (Kicheko/Makofi)