Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zahor Mohamed Haji

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mwera

Primary Question

MHE. ZAHOR MOHAMMED HAJI aliuliza:- Je, Serikali ipo tayari kuleta marekebisho ya Sheria baada ya Serikali kukubaliana kuondoa baadhi ya changamoto za Muungano?

Supplementary Question 1

MHE. ZAHOR MOHAMMED HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nikushukuru kwa kunipa nafasi. Sasa naomba Mheshimiwa Waziri anipe majibu; je, ni lini Serikali italeta Muswada wa Mabadiliko ya Sheria ili mambo yote ambayo yameondolewa kwenye changamoto za Mambo ya Muungano yaonekane kwenye Sheria? Nashukuru.

Name

Dr. Selemani Said Jafo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kisarawe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA MAKAMU WA RAIS, MUUNGANO NA MAZINGIRA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nichukue fursa hii nimpongeze sana Mheshimiwa Zahor kwa kazi nzuri anayoifanya Jimboni lakini pia kazi anayoifanya katika kutaka wananchi wajue na wapate taaluma juu ya masuala yanayogusa mnasaba wa Muungano.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika kikao chetu cha tarehe 6 Disemba, 2022, miongoni mwa ajenda ambayo iliibuka katika kikao kile ni namna gani changamoto zilizokuwa zimeshatatuliwa tukaziweka katika legal document. Miongoni mwa kazi ambayo tuliwapa tulitoa maelekezo kwa wanasheria wetu wa pande zote mbili za muungano waende wakakae wakaone namna ya kuweza kuanza mchakato huu ili lengo na madhumuni tuweze kuyaingiza katika legal document. Hii itasaidia kizazi kijacho kuyatambua haya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo nimuombe Mheshimiwa Mbunge awe na subira kidogo, kazi inafanyika, wanasheria tumeshawapa kazi na watakuja kutuletea majibu na hili jambo la kuifanya ikawa kwenye document ya kisheria inakwenda kufanyika, nakushukuru.