Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI K.n.y. MHE. DKT. ALFRED J. KIMEA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Kibo – Mgombezi – Bagamoyo na NMB Benki hadi Magunga hospitali zilizo kwenye mradi wa TACTIC?

Supplementary Question 1

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, je, Serikali kwa sababu miradi hii pamoja na mambo mengine itajenga pia vitega uchumi ambavyo vitakuwa vinazisaidia Halmashauri zetu kupata mapato ya ndani. Je, Serikali iko tayari kuharakisha mchakato ule hasa mara baada ya kutangazwa zabuni?

Swali la pili, kwa kuwa Mafinga ni mnufaika wa mradi huu lakini katika tier ya tatu; je, Serikali iko tayari ku-fast track ili ile tier ya tatu na yenyewe iende sambamba na hii tier ya pili kusudi kuwawezesha Wananchi wa Mji wa Mafinga kupata barabara na kujengewa stendi na kujengewa pia mradi mmoja ambao utakuwa ni chanzo cha mapato ya ndani? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Cosato Chumi, kwanza hili la Serikali kuharakisha zabuni hizi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyokwishasema kwenye majibu yangu ya msingi, mara pale ambapo hawa Wakandarasi Washauri watamaliza kufanya usanifu ule mwezi Agosti mwaka huu, mwezi Septemba zabuni zile zitatangazwa ili waweze kupatikana wakandarasi wa kujenga miradi hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hii si tu kwa barabara tayari usanifu unafanyika pia katika ujenzi wa masoko na ujenzi wa stendi katika maeneo mbalimbali hapa nchini ambayo yamo katika tier 2.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda kwenye swali lake la pili ni kwamba Mji wa Mafinga kweli upo kwenye tier 3 na mara baada ya usanifu kukamilika kwenye tier 2 mwezi Agosti, sasa usanifu utaanza kwenye tier 3 ambayo ni Miji 18 ikiwemo Halmashauri ya Mji wa Mafinga. (Makofi)

Name

Mohamed Lujuo Monni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chemba

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI K.n.y. MHE. DKT. ALFRED J. KIMEA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Kibo – Mgombezi – Bagamoyo na NMB Benki hadi Magunga hospitali zilizo kwenye mradi wa TACTIC?

Supplementary Question 2

MHE. MOHAMED L. MONNI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, Barabara ya kutoka Chemba – Soya – Mwailanje – Zajilwa – Dodoma na Zajilwa ni Jimboni kwake, kwa sasa imeharibika sana, naomba sasa commitment ya Naibu Waziri mwenyewe, ni lini barabara ile itajengwa ili ipitike wakati wowote? Ahsante. (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Monni, nikiri kwamba alipotaja Zajilwa na Itiso zimo katika Jimbo langu la Chamwino na barabara hii ya Chemba – Soya – Mwailanje itaanza ukarabati wake mara moja. Ipo katika bajeti ya mwaka huu wa 2023/2024 na tayari Meneja Maganga pamoja na Lamela - Meneja wetu wa Mkoa na Meneja wa TARURA wa Wilaya ya Chemba, wameshakaa na kuona ni namna gani wanaanza utekelezaji wa ujenzi wa barabara hii, hasa katika maeneo ambayo ni korofi.

Name

Abubakar Damian Asenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilombero

Primary Question

MHE. COSATO D. CHUMI K.n.y. MHE. DKT. ALFRED J. KIMEA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga barabara ya Kibo – Mgombezi – Bagamoyo na NMB Benki hadi Magunga hospitali zilizo kwenye mradi wa TACTIC?

Supplementary Question 3

MHE. ABUBAKARI D. ASENGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana.

Hali ya barabara za Halmashauri ya Mji wa Ifakara katika Kata 19 ni mbaya sana kutokana na mvua hizi. Naishukuru Serikali kwa kutuletea fedha za kujenga kwa lami barabara za Ifakara Mjini, lakini barabara zimejengwa chini ya kiwango na ni mbovu. Naomba kujua Serikali itachukua hatua gani kwa wakandarasi ambao wamejenga Barabara ya Kibaoni na Ifakara Mjini sokoni ambazo mpaka sasa hivi zimeshaharibika? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Asenga, naomba nitumie Bunge lako Tukufu hili kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, kumwelekeza Meneja wa TARURA Mkoa wa Morogoro kuhakikisha Mkandarasi ambaye alijenga barabara hizi alizozitaja Mheshimiwa Asenga, kama mkataba wake ulikuwa bado haujaisha, aweze kurudi na kurekebisha yale maeneo ambayo tayari yameharibika bado barabara ni mpya kabisa. (Makofi)