Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Eng. Stella Martin Manyanya

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Nyasa

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka alama za kuongoza meli katika eneo la kuegesha meli kwenye Ziwa Nyasa?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na kwanza nimshukuru sana Mheshimiwa Waziri kwa majibu yake mazuri yenye kutia moyo. Pia, kwa niaba ya wananchi wa Jimbo la Nyasa na jirani zao tunapenda kushukuru sana na kumpongeza Mheshimiwa Rais kwa ujenzi wa Bandari ya Mbamba Bay. Baada ya hapo naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa Bandari ya Mbamba Bay itakuwa ni kubwa na ya kisasa na itahitaji mzigo mkubwa kwa ajili ya kuhudumia Tanzania pamoja na nchi za jirani. Je, Serikali ina mpango gani wa kuhakikisha sasa reli ya kutoka Mtwara mpaka Mbamba Bay inajengwa ili kuhakikisha kwamba bandari hii inatumika kiukamilifu?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili; kwa kuwa Bandari ya Mbamba Bay inategemeana sana mizigo yake na bandari ndogondogo zilizopo Kando ya Ziwa Nyasa. Bandari kama Liuli, Njambe, Lipingu na kule Manda katika Wilaya ya Ludewa. Nini mpango wa Serikali kuboresha bandari hizi ili ziweze kusaidia na kuhakikisha kwamba mizigo yote inachukuliwa vizuri?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimwa Mwenyekiti, kwanza kwa niaba ya Serikali nipokee pongezi za dhati za Mheshimiwa Manyanya kwa sababu ni kwa muda mrefu Wananchi wa Ruvuma na mikoa ya jirani wamekuwa wakitamani kuona bandari hii inafanyiwa uboreshaji na tayari Serikali ya Awamu ya Sita imeshaanza utekelezaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali lake pili anauliza kuhusu bandari ndogondogo kama za Liuli, Njambe na maeneo mengine. Hizi bandari zote zimejumuishwa katika mpango kabambe ambao ni The Updated National Proposed Master Plan 2022/2023 mpaka 2026/2027 ambazo zipo kwenye mpango wa kuboreshwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikija kwenye swali la kwanza ambalo ndio swali kubwa linaulizwa na Wabunge karibu wote wa Nyanda za Juu Kusini pamoja na Kusini. Kwamba ni lini sasa reli ya SGR ya kutoka Mtwara mpaka Mbamba Bay itaanza kujengwa na pengine reli hii wengine wanakwenda mbele zaidi wanataka kufahamu kuunganisha mpaka Liganga na Mchuchuma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pengine nieleze kwa ufupi tu kwamba, Serikali inao mpango kwamba inatambua umuhimu na ukubwa wa mradi huu wa SGR ya Southern Corridor ambao ndani yake una miradi zaidi ya sita.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja reli hii ikijengwa ya kilometa 1,000 kutoka Mtwara kwenda mpaka Mbamba Bay kwenda mpaka Liganga na Mchuchuma utawezesha kusafirisha makaa ya mawe ambapo Mungu ametujalia zaidi ya metric tons milioni 400 na yaligundulika zaidi ya miaka pengine mia moja iliyopita.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili itatusaidia makaa ya mawe yale yakishatengenezwa yataanza kuzalisha umeme zaidi ya megawati 600; nusu yake yakayeyushe chuma pale Liganga, nusu yake yaingie kwenye Gridi ya Taifa lakini kama haitoshi meli hii pia inakwenda kutoa ajira na inakwenda kutoa pia chuma ambacho kinakwenda kutengenezea magari na vitu mbalimbali.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninyi mnafahamu Watanzania kwamba kwa sehemu kubwa zaidi ya asilimia 100 tunaagiza chuma kutoka nje jambo ambalo linachukua fedha zetu nyingi zaidi. Hivyo basi, Serikali kwa kutumbua umuhimu huo mkubwa; moja, imeshaanza kutengeneza uboreshaji mkubwa wa Bandari ya Mtwara ili mzigo upatikane kwa wingi zaidi; lakini pili, inaongeza bandari nyingine ya pili ya kisiwa mgao ili bidhaa chafu zote kwa maana ya makaa ya mawe, simenti na kadhalika ipitie pale.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tatu ipo kwenye mpango wa kuhuisha stadi iliyofanyika miaka ya nyuma kwa maana ya kutafuta mshauri mwelekezi kuhuisha ile reli ili tuweze kujua mahitaji yake ni yapi. Mara tu baada ya kukamiliisha tunategemea kuanza kuijenga kwa mfumo wa PPP na hatimaye tunaamini likikamilika hili ni moja kati ya mambo ambayo Mheshimiwa Rais wetu anayapigania na kwa msaada wa Mwenyezi Mungu atakayakamilisha na hivyo kwenda kufufua uchumi wetu kwa kiasi kikubwa zaidi.

Name

Sylivia Francis Sigula

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka alama za kuongoza meli katika eneo la kuegesha meli kwenye Ziwa Nyasa?

Supplementary Question 2

MHE. SYLVIA F. SIGULA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, ukanda wa Ziwa Tanganyika yaani Mkoa wa Kigoma, Rukwa na Katavi tumesubiri kwa muda mrefu ukarabati wa meli ya MV Liemba. Je, ni lini Serikali itakamilisha ukarabati wa meli ya MV Liemba ili kunusuru usafiri huo?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimwa Mwenyekiti, Serikali ya awamu ya sita imejipambanua katika kutenda. MV Liemba ni kiungio kubwa la Ziwa Tanganyika na wananchi wote wanaotumia ziwa hilo. Tumekwishasaini mkataba mwaka jana mwezi Novemba na ndani ya mwaka mmoja tutakuwa tumeshakamilisha ukarabati na ili Wananchi wa Kigoma na maeneo jirani wasubiri kwa hamu tunakwenda kukamilisha meli yao.

Name

Hassan Seleman Mtenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka alama za kuongoza meli katika eneo la kuegesha meli kwenye Ziwa Nyasa?

Supplementary Question 3

MHE. HASSAN S. MTENGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa kuna agenda ya Mtwara Corridor na tunapozungumza Mtwara Corridor tunazungumza bandari, tunazungumza Airport pia tunazungumza reli ya Liganga na Mchuchuma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, umekuwa ni wimbo toka mwaka 2020 mpaka leo hii Serikali kila ikija hapa wanasema ipo kwenye mpango. Tunataka sasa tufahamu ni lini sasa ujenzi wa reli hii ya Liganga na Mchuchuma.

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimwa Mwenyekiti, nafikiri Mheshimiwa Mtenga anataka kupata pengine ufafanuzi wa ziada. Nimekwishasema na naomba nirejee. Tulishaanza SGR ya kutoka Dar es Salaam kwenda mpaka Isaka, tumekwishaenda na SGR kutoka Dar es Salaam tumekwenda mpaka Kigoma sasa tunakwenda mpaka Msongati Burundi. Awamu inayofuatia Serikali ya Awamu ya Sita imejipambanua na imejiwekea malengo ya kwenda SGR Kusini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimtoe mashaka uongozi wa Serikali ya Awamu ya Sita unakwenda kujenga reli ya SGR ya kusini ambayo ni Mtwara Corridor kama nilivyosema. Hii inakwenda kuungana pamoja na uboreshaji mkubwa wa Airport kama nilivyosema sambamba na uboreshaji mkubwa wa maeneo ambayo nimeyaeleza pale awali, kwa hiyo, nimtoe mashaka Mheshimiwa Mbunge.

Name

Kavejuru Eliadory Felix

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Buhigwe

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka alama za kuongoza meli katika eneo la kuegesha meli kwenye Ziwa Nyasa?

Supplementary Question 4

MHE. KAVEJURU E. FELIX: Mheshimiwa Mwenyekiti, nikushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Serikali imekuwa ikitoa ahadi ya kujenga meli kwa ajili ya abiria na mizigo katika Ziwa Tanganyika ili kutatua changamoto ya usafiri katika Mikoa ya Kigoma, Katavi na Rukwa. Je, ujenzi huo utatekelezwa lini?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimwa Mwenyekiti, siyo tu meli ya mizigo na abiria kama alivyouliza Mheshimiwa Mbunge. Serikali imesaini tayari mkataba, tumeanza kujenga kiwanda cha kutengeneza meli nyingi nyingi katika Ziwa Tanganyika. Ambapo kiwanda hicho kitahusika na kutengeneza meli za mizigo na abiria na kukarabati zilizopo, hili linakwenda sambamba na uboreshaji mkubwa wa meli ambazo zipo za akina Mwongozo, Sangala pamoja na kina Liemba kama ilivyoulizwa na Mheshimiwa Sylvia pale awali.

Name

Venant Daud Protas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igalula

Primary Question

MHE. ENG. STELLA M. MANYANYA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kuweka alama za kuongoza meli katika eneo la kuegesha meli kwenye Ziwa Nyasa?

Supplementary Question 5

MHE. VENANT D. PROTAS: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwanza niwapongeze Serikali kwa kujenga reli ya kisasa ambayo ya SGR kutoka Makutupora Tabora. Reli ile mpaka sasa hivi wamefukua makaburi ya watu wa Igalula, watu wa Goweko, Tula hamjawalipa mpaka leo. Je, ni lini mtawalipa fedha ambazo mliwarudishia msiba mpaka leo hamjawalipa kwa sababu reli inataka ipite?

Name

David Mwakiposa Kihenzile

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kusini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI: Mheshimwa Mwenyekiti, hii hoja ya Mheshimiwa Venant naomba niichukue tuifatilie halafu tuifanyie kazi baada ya kupata taarifa zake za kina.