Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA K.n.y. MHE. NORAH W. MZERU aliuliza:- Je, lini Serikali itamalizia ujenzi wa zahanati ya Uwanja wa Ndege katika Kata ya Mafisa Mkoani Morogoro?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwanza kabisa naishukuru Serikali kwa ujenzi wa Zahanati, Vituo vya Afya na Hospitali kwenye Mkoa wetu wa Morogoro. Hii Zahanati ya Uwanja wa Ndege ina upungufu wa wafanyakazi hasa manesi na madaktari. Je, ni lini mtapeleka hao Manesi na Madaktari ili kutimiza ikama? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, Kituo cha Afya Mafiga kimekuwa na tatizo sana la theatre na wanawake wengi wajawazito wanapenda sana kujifungulia pale, na mara wanapopata matatizo, wanapelekwa Hospitali Kubwa ambapo kuna mwendo. Je, ni lini Kituo hiki cha theatre kitajengwa? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Dkt. Christine Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunafahamu kwamba Zahanati hii ya Uwanja wa Ndege ina watumishi watano; Afisa Tabibu mmoja, Wauguzi wawili, Mtaalamu wa Maabara mmoja na Mhudumu wa Afya mmoja. Kwa idadi ya wananchi ambao wanatibiwa pale, tunahitaji kuongeza wataalamu. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, tayari Serikali imeshaitambua Zahanati hiyo, mara ajira zitakapojitokeza, tutahakikisha tunawapa kipaumbele kwa ajili ya kuongeza idadi ya watumishi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikijibu swali la pili, Kituo cha Afya cha Mafiga ni kweli kipo mjini na kinahudumia wananchi wengi na kina upungufu wa baadhi ya miundombinu ikiwepo majengo ya upasuaji na majengo mengine. Tushamwelekeza Mkurugenzi wa Manispaa ya Morogoro kuandaa mchoro wa upanuzi wa Kituo cha Afya cha Mafiga. Nitumie fursa hii kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba tutafuatilia ili tuweze kuona umefikia hatua gani na tuone uwezekano wa kuongeza majengo katika Kituo cha Afya cha Mafiga, ahsante. (Makofi)

Name

Seif Khamis Said Gulamali

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manonga

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA K.n.y. MHE. NORAH W. MZERU aliuliza:- Je, lini Serikali itamalizia ujenzi wa zahanati ya Uwanja wa Ndege katika Kata ya Mafisa Mkoani Morogoro?

Supplementary Question 2

MHE. SEIF K. S. GULAMALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru na naomba kumwuliza Mheshimiwa Naibu Waziri; je, ni lini Serikali itaongeza fedha za ujenzi wa Zahanati kwenye vijiji hasa Majimbo ya Vijijini? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Gulamali, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali imekuwa ikijenga Vituo vya Afya katika maeneo ya vijijini kwa kuchangia nguvu za wananchi kwa kutoa shilingi milioni 50 kwa ajili ya umaliziaji. Fedha hiyo shilingi milioni 50 ilianza kutolewa mwaka 2016/2017 na ukizingatia kasi ya inflation kwa sasa, tumeshapitia bajeti za ujenzi wa Vituo vya Afya, Zahanati na pia Hospitali za Wilaya. Kwa hiyo, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba tayari Serikali imeshafanya kazi hiyo ya kubadili au kuongeza kiasi cha fedha kwa ajili ya ukamilishaji wa zahanati. Taarifa rasmi itatolewa na Waheshimiwa Wabunge mtaipata na fedha zinazokuja zitakuwa na mabadiliko ili kuendana na inflation iliyojitokeza, ahsante. (Makofi)

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA K.n.y. MHE. NORAH W. MZERU aliuliza:- Je, lini Serikali itamalizia ujenzi wa zahanati ya Uwanja wa Ndege katika Kata ya Mafisa Mkoani Morogoro?

Supplementary Question 3

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi. Baadhi ya zahanati ambazo zimejengwa Makao Makuu ya Kata hasa Sirop, Dirma, Laghanga, Getanuwas na Ishponga hazina jengo la mama na mtoto; je, Serikali ina kauli gani ili kuboresha afya ya mama na mtoto?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Engineer Samweli Hhayuma, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, zahanati zote ambazo zimejengwa na zina upungufu wa majengo ya Huduma za Afya ya Mama, Baba na Mtoto, tumeshatoa ramani nyingine kwa ajili ya kuongeza majengo hayo kwenye zahanati hizo ili huduma hizi ziweke kupatikana. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba zahanati ambazo amezitaja hapa tutazipa kipaumbele pia kuhakikisha kwamba zinajenga majengo hayo, ahsante.

Name

Yustina Arcadius Rahhi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA K.n.y. MHE. NORAH W. MZERU aliuliza:- Je, lini Serikali itamalizia ujenzi wa zahanati ya Uwanja wa Ndege katika Kata ya Mafisa Mkoani Morogoro?

Supplementary Question 4

MHE. YUSTINA A. RAHHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Nami naomba kuuliza swali la nyongeza. Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa Zahanati ya Nahasey Wilayani Mbulu ambayo iko katika mazingira magumu hasa sehemu ya mama na mtoto na kutoa huduma? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, zahanati hizi ambazo zinaendelea kujengwa katika maeneo yetu, zinatumia fedha za mapato ya ndani na pia fedha kutoka Serikali Kuu. Kwa hiyo, naichukua hoja ya Mheshimiwa Mbunge na baada ya hapa tutafuatilia kule Bunda tuone chanzo cha fedha ambacho kinaweza kupatikana mapema iwezekanavyo ili tuweze kukamilisha ujenzi wa zahanati hii yakiwemo hayo majengo ya Huduma ya Afya ya Mama, Baba na Mtoto, ahsante.