Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, lini Serikali itamaliza tatizo la kukatika kwa umeme katika Manispaa ya Morogoro?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Licha ya majibu mazuri ya Serikali, nina maswali madogo mawili.

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza. Kata ya Mgambazi ipo kwenye Manispaa ya Morogoro, lakini mpaka sasa hivi Mtaa mzima wa Mgambazi pamoja na Chambilazi na Vilengwe hawajapatiwa umeme, licha ya kuwa kwenye Manispaa ya Morogoro: Je, ni lini watapata umeme? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Kijiji cha Zongo ambacho kiko kwenye Kata ya Kisemo pamoja na Kijiji cha Bwakila Juu katika Halmashauri ya Wilaya ya Morogoro Vijijini, hawajapata umeme. Ni lini vijiji hivi vitapatiwa umeme? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Dkt. Christine Ishengoma kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na umeme katika Mitaa ya Mungazi, Chambilazi na Vilengwe tayari tumeshaiweka kwenye Mpango wa fedha wa 2025 na mitaa hii itapatiwa umeme.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na Vijiji vya Zongo na Bwakila Juu, tayari wakandarasi wamepatiwa site na muda wowote kazi itaanza, ahsante. (Makofi)

Name

Josephine Johnson Genzabuke

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, lini Serikali itamaliza tatizo la kukatika kwa umeme katika Manispaa ya Morogoro?

Supplementary Question 2

MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Serikali iliahidi kufunga umeme katika shule zote za sekondari na taasisi za dini, lakini zipo shule ambazo hazijaweza kufungiwa umeme; je, ni lini Serikali itafunga umeme katika Shule ya Sekondari Kimenyi, katika Halmashauri ya Kasulu DC? (Makofi)

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Genzabuke, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tayari kuna miradi inaendelea kwenye vijiji vyote ya kupeleka umeme. Mwanzoni ilikuwa kilomita moja, tumeongeza kilometa mbili ili taasisi nyingi zifikiwe. Kwa shule hii ya Kimenyi kama haipo katika scope ambayo ipo sasa hivi, tutahakikisha kwamba tunaweka fedha kwenye mwaka ujao ili na wenyewe waweze kupatiwa umeme, ahsante.

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, lini Serikali itamaliza tatizo la kukatika kwa umeme katika Manispaa ya Morogoro?

Supplementary Question 3

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Wananchi wa Kilwa wamekuwa ni wanufaika wakubwa wa umeme wa gesi unaozalishwa katika Kituo cha Somanga.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kukiboresha kituo hiki ili kumaliza changamoto kubwa inayokabili wananchi wa Kilwa katika huduma ya umeme? (Makofi)

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Ndulane, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tayari tumeanza mkakati wa kurekebisha kufanya matengenezo kwenye visima vyetu ambavyo vinazalisha gesi na tumeshaanza Mnazi Bay, Songosongo pamoja na Madimba. Kwa Somanga pia tutahakikisha tunaweka kwenye mkakati ili tuweze kukiboresha na wananchi wa Kilwa waweze kupata umeme wa uhakika, ahsante.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, lini Serikali itamaliza tatizo la kukatika kwa umeme katika Manispaa ya Morogoro?

Supplementary Question 4

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa kuwa tatizo la kukatika umeme katika Manispaa ya Morogoro linafanana na tatizo lililopo katika Wilaya na Mkoa wa Kilimanjaro, hususan Kata ya Uru Kusini; ni lini sasa TANESCO itarekebisha tatizo hilo kabisa?

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Shally Raymond, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tatizo la kukatika kwa umeme halipo tu Morogoro na Kilimanjaro, limekuwepo kwa Tanzania nzima. Serikali tumechukua hatua. Mwanzoni tulianza na upungufu wa Megawati 421 wastani hapo. Mpaka kufikia leo tumefanikiwa kupunguza upungufu kwa wastani wa Megawati 218. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, tunachukua hatua.

Mheshimiwa Spika, nilieleza hapa kwamba Bwawa la Mwalimu Nyerere tumefikia 94.01% na tumeshaanza majaribio. Pia, nimesema hapa tumeongeza uzalishaji kwenye visima vetu vya Songo Songo pamoja na Madiba ili kuweza kuongeza gesi ili tuweze kupunguza changamoto hii ya upatikanaji wa umeme. Tayari tunafanya matengenezo kwenye mitambo yetu yote ili kuboresha hali. Nina uhakika Waheshimiwa mmeona hali ya upatikanaji wa umeme imeanza kutengemaa.

Mheshimiwa Spika, niwahakikishie tutaendelea kufanya kazi hii nzuri ili kuhakikisha tunaiondoa nchi katika changamoto ya umeme, ahsante. (Makofi)

Name

Athumani Almas Maige

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tabora Kaskazini

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, lini Serikali itamaliza tatizo la kukatika kwa umeme katika Manispaa ya Morogoro?

Supplementary Question 5

MHE. ATHUMAN A. MAIGE: Mheshimiwa Spika, Wilaya ya Uyui Makao Makuu yake ni Isikizya, kilometa 35 kutoka Tabora Mjini, na lipo tatizo kubwa kweli la umeme. Watumishi pale; DC na Wakurugenzi hawafanyi kazi kutwa nzima, umeme unakatika zaidi ya mara tano kwa siku; je, Serikali ina mpango gani wa kuweka umeme wa kudumu pale Isikizya? (Makofi)

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Almas Maige, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tayari Serikali tumechukua hatua katika Halmashauri ya Uyui na katika Mkoa mzima wa Tabora. Tumechukua hatua na tuna mradi unaendelea wa kujenga vituo vya kupooza umeme na line za kusafirisha umeme. Kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, baada ya mradi huo kukamilika ndani ya miezi 18, tatizo la kukatikakatika kwa umeme unaotakana na line ndefu kutoka Tabora Mjini mpaka Uyui mpaka kwenye Jimbo la Mheshimiwa Sitta tutakuwa tumelipunguza.

Mheshimiwa Spika, pia nimwelekeze Meneja wa TANESCO Mkoa wa Tabora ahakikishe ratiba wanazozipanga zinazingatia maeneo ambayo yanatoa huduma kwa wananchi hususan maeneo ambayo yanatoa hospitali, vituo vya afya pamoja na shule na maeneo mengine ambayo yanatoa huduma kwa wananchi, ahsante.

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, lini Serikali itamaliza tatizo la kukatika kwa umeme katika Manispaa ya Morogoro?

Supplementary Question 6

MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, wakati wa Bunge la Bajeti, Serikali iliahidi kupeleka turbine ya megawati 20 kule Mtwara kama hatua za dharura za kupunguza tatizo la upungufu wa umeme ambalo linasababisha kukatikakatika kwa umeme; je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi hiyo? (Makofi)

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Anastazia Wambura kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli tuliaahidi kupeleka hii taibai kutoka Ubungo kwenda Mtwara. Baada ya tathmini ya kina tulijirididha mtambo huu hautafanya kazi vizuri pale Mtwara. Tumeshaongea na Kampuni ya CSI juu ya kuzalisha umeme hapo na tumeshakamilisha, na tuna kituo cha kupoza umeme tunakijenga hiyari ambacho tunategemea kitakamilika ndani ya mwezi huu. Kikikamilika basi, umeme ambao utatolewa na Kampuni ya CSI utaweza kwenda kwenye Mkoa mzima wa Mtwara na Lindi na hivyo tutakuwa tumeondoa kabisa changamoto ya umeme kwa Mikoa miwili.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, tunawaomba Waheshimiwa Wabunge na wananchi wa Mtwara na Lindi watuvumilie kidogo mpaka mwishoni mwa mwezi huu tutakuwa tumekamilisha na kuwapatia umeme wa uhakika, ahsante.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, lini Serikali itamaliza tatizo la kukatika kwa umeme katika Manispaa ya Morogoro?

Supplementary Question 7

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Ipo dhamira ya Serikali ya kupeleka umeme vijijini kote na umeme kufika maeneo ya mbali kabisa kutoka Mkoa wa Singida ambako ndio sub-station kubwa ilipo eneo la Rungwa, lakini umeme unafika ukiwa faint na Serikali ilikuwa na dhamira ya kujenga kito cha kupoza umeme kwa maana ya sub-station katika eneo la Mitundu. Je, Serikali inaanza lini kujenga kituo cha kupoza umeme Mitundu, ili kusaidia wananchi, ili waweze kujiwezesha na viwanda vidogo vidogo?

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, ahsante. naomba kujibu swali la Mheshimiwa Yahaya Massare, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli mpango huo upo, na nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, tunatafuta fedha na pili, mchakato huo wa upatikanaji wa fedha ukikamilika basi tutaanza kujenga kituo hiki cha kupoza umeme, ahsante.

Name

Dorothy George Kilave

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Temeke

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, lini Serikali itamaliza tatizo la kukatika kwa umeme katika Manispaa ya Morogoro?

Supplementary Question 8

MHE. DOROTHY G. KILAVE: Mheshimiwa Spika, kwa kuniona. Naomba kuuliza swali. Je, ratiba ya mgawo wa umeme katika Jimbo letu la Temeke umekuwa ni wa muda mrefu sana na ratiba yake haifuatilii kadiri ya ratiba zinavyokuja kwamba, umeme utakatika kuanzia muda fulani mpaka muda fulani, sasa umekuwa ni wa muda mrefu sana. Kuanzia jana mpaka leo saa hizi Temeke hatuna umeme, je, una tamko gani Waziri, ili kule Temeke waweze kutuletea umeme kulingana na mgawo? (Makofi)

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Dorothy Kilave, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama nilivyotangulia kusema, kidogo tumetengemaa kwenye suala la upatikanaji wa umeme, na kwa Mkoa wa Dar es Salaam tunafahamu maeneo mengi kwa sasahivi yanaweza yakapitisha hata siku mbili mpaka tatu bila kukatika kwa umeme. Kwa hili ambalo ambalo ameniambia Mheshimiwa Mbunge inaonekana ni suala ambalo ni specific, yaani ni mahususi. Naomba nilifuatilie, Mheshimiwa Mbunge, nikitoka hapa na nitakupatia majibu, ahsante. (Makofi)

Name

Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, lini Serikali itamaliza tatizo la kukatika kwa umeme katika Manispaa ya Morogoro?

Supplementary Question 9

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, tarehe 10 Agosti, 2021 TANESCO na STAMICO waliasaini makubaliano ya kuzalisha megawati 200 kutoka kwenye Mgodi wa Makaa ya Mawe Kiwira; je, mpango huo umefikia wapi?

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Ally Jumbe, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mpango huu bado upo na tunautekeleza kulingana na upatikanaji wa fedha, ahsante.

Name

Innocent Edward Kalogeris

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, lini Serikali itamaliza tatizo la kukatika kwa umeme katika Manispaa ya Morogoro?

Supplementary Question 10

MHE. INNOCENT E. KALOGERIS: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa swali la nyongeza:-

Mheshimiwa Spika, nini mpango wa Serikali katika kupeleka umeme katika Shule ya Sekondari ya Tawa katika Halmashauri ya Morogoro Vijijini.

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Innocent Kalogeris, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, tayari tuna miradi ambayo inaendelea kwenye kila Mkoa kuhusiana na kupeleka umeme. Nitafuatilia kuona kama Shule ya Sekondari Tawa ipo katika mipango ambayo tunayo, na kama hamna, basi tutafanya jitihada za ziada, ili kuhakikisha Shule ya Sekondari Tawa inapatiwa umeme, ahsante.

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, lini Serikali itamaliza tatizo la kukatika kwa umeme katika Manispaa ya Morogoro?

Supplementary Question 11

MHE. ZAYTUN S. SWAI: Mheshimiwa Spika, ahsante, je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha maeneo ya uzalishaji pamoja na hoteli za kitalii kama za Mkoa wa Arusha hazipati adha ya ukatikaji wa umeme?

Name

Judith Salvio Kapinga

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zaytun Swai, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimeshatangulia kusema hapo awali, Serikali tunafanya jitihada mbalimbali kuhakikisha tunapunguza adha ya upatikanaji wa umeme. Na kwa kadiri ya mipango hii, nimhakikishie, maeneo haya ya uzalishaji yataendelea kuendelea kupata umeme wa uhakika kwa kadiri ambavyo tunaboresha upatikanaji wa umeme. Ahsante. (Makofi)