Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Yustina Arcadius Rahhi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. YUSTINA A. RAHHI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha uwekaji wa samani na vifaa vya kufundishia katika Vituo vya Rasilimali za Kilimo?

Supplementary Question 1

MHE. YUSTINA A. RAHHI: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini nina maswali mawili madogo ya nyongeza. Swali langu la kwanza; ni vituo vingapi vya rasilimali za kilimo vilikwishabadilishwa matumizi katika Serikali za Mitaa na kwa maagizo sasa ya Waziri ni vingapi sasa vimerudishwa ili kuendelea na matumizi yake ya kawaida?

Mheshimiwa Spika, swali langu la pili; Serikali ina mpango gani sasa kuwateua waratibu watakaoratibu mafunzo katika Vituo hivyo vya Rasilimali za Kilimo ili kuratibu mafunzo kwa wakulima na wafugaji na kwamba vitengewe bajeti kidogo ili kuweza kufanya kazi kwa ufanisi?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Yustina Arcadius Rahhi, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, swali la kwanza, ni kweli nahitaji takwimu, nitaomba nimpatie Mheshimiwa Mbunge takwimu sahihi baada ya kuwa nimejiridhisha ni vituo vingapi ambavyo vimebadilishwa matumizi. Hata hivyo, tayari tumeshawaandikia wahusika kwa maana ya kurudisha vituo hivi kurudi katika matumizi yake ya awali kwa ajili ya kuwa ni sehemu ya rasilimali za kilimo. Kwa hiyo, baadaye nitampatia taarifa sahihi Mheshimiwa Mbunge.

Mheshimiwa Spika, la pili la kuhusu uteuzi wa Waratibu, tunapokea ushauri wa Mheshimiwa Mbunge, tutalifanyia kazi ili kuwepo na waratibu katika vituo hivi na lengo kubwa ni kuhakikisha kwamba tunatoa elimu ambayo itamfikia mkulima kwa wakati.

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. YUSTINA A. RAHHI aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha uwekaji wa samani na vifaa vya kufundishia katika Vituo vya Rasilimali za Kilimo?

Supplementary Question 2

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Pale Jimboni Kibaha kwenye Kitongoji cha Disunyala kipo Kituo cha Rasilimali za Kilimo kilichoanza kujengwa tangu mwaka 2007 na mpaka leo hakijakamilika kujengwa. Je, nini mpango wa Serikali kumalizia kituo kile?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Michael Mwakamo, Mbunge, kama ifutavyo: -

Mheshimiwa Spika, jambo hili Mheshimiwa Mbunge alishalileta ofisini, tumezungumza na tulimpa ahadi ya kwamba lengo letu ni kuhakikisha kwamba tunakamilisha Vituo vyote vya Rasilimali za Kilimo vipo katika Kata ili mwisho wa siku tuweze kuwafikia wakulima kwa ukaribu. Katika baadhi ya maeneo tumelenga kuvifanya vituo hivi kuwa ni mechanization center ambayo itasaidia wakulima kwenda kukopa au kukodisha vifaa vya kilimo kupitia centers hizo. Kwa hiyo, nimuahidi Mheshimiwa Mbunge kwamba, pale kwake pia tutakamilisha ili mwisho wa siku malengo yaliyokusudiwa yaweze kutimia.