Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. David Mathayo David

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Same Magharibi

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza: - Je, ni lini Serikali itasaidia kukarabati mifereji ya Marwa, Kwasita, Magereza, Gunge na Kirua katika Bonde la Mto Pangani?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. DAVID M. DAVID: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza. La kwanza; ningemuomba Mheshimiwa Waziri pengine baada ya Bunge tuweze kutembelea katika skimu hizi ili tuweze kuziona zile ambazo kwa kweli ndizo zinazotakiwa zitengewe fedha kwa ajili ya upembuzi yakinifu.

Mheshimiwa Spika, la pili, katika Kata ya Makanya kuna korongo ambalo wakati mvua inanyesha ndilo linategemewa sana katika umwagiliaji. Ningeomba Serikali, hasa Waziri tuweze kutembelea naye pamoja ili aweze kuliona hilo Korongo ili na lenyewe liwekwe katika mpango wa kufanyiwa upembuzi yakinifu ili wananchi wa Makanya waweze kupata chakula kwa mwaka mzima. Ahsante.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge, Dkt. David Mathayo David, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nipo tayari kuongozana na Mheshimiwa Mbunge kwenda kutembelea skimu hizo kuziangalia na ukarabati ambao unahitajika. Vilevile kwa sababu nia yetu ni kuhakikisha hatupotezi maji, Kata ya Makanya kwenye eneo ambapo kuna korongo kubwa ambalo linatuamisha maji tutakwenda pia kuona. Lengo letu ni kuyatumia maji ipasavyo kwa ajili ya kilimo cha nchi yetu.

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza: - Je, ni lini Serikali itasaidia kukarabati mifereji ya Marwa, Kwasita, Magereza, Gunge na Kirua katika Bonde la Mto Pangani?

Supplementary Question 2

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kuniona. Mto wa Motale unahudumia Kata ya Masama Magharibi na Masama Kati na ni skimu kubwa sana inayotegemewa ndani ya Jimbo la Hai. Je, ni lini Serikali itafanya ukarabati wa skimu hii ikizingatiwa sasa hivi ndani ya Jimbo la Hai kuna changamoto kubwa ya ukosefu wa mahindi? Kwa hivyo, mto huu unaweza kutumika kuweza kufanya kilimo cha umwagiliaji. Ahsante.

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Saashisha Mafuwe, Mbunge wa Hai, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli tunafahamu umuhimu wa Mto Motale katika kuhakikisha kwamba wakulima wa Wilaya ya Hai wanafanya kilimo cha umwagiliaji. Jambo alilolisema la ukarabati, namwahidi Mbunge kwamba mimi, yeye na watalaam wetu tutaongozana kwa ajili ya kwenda kuangalia eneo husika. Baadaye baada ya kushauriwa vyema, basi tunaona namna ya kuingiza katika mpango wa Serikali ili wananchi wa Hai waweze kunufaika na kilimo cha umwagiliaji. (Makofi)

Name

Vita Rashid Kawawa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Namtumbo

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza: - Je, ni lini Serikali itasaidia kukarabati mifereji ya Marwa, Kwasita, Magereza, Gunge na Kirua katika Bonde la Mto Pangani?

Supplementary Question 3

MHE. VITA RASHID KAWAWA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii ya kuuliza swali la nyongeza. Naomba kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba, ni lini watakamilisha Mradi wa Umwagiliaji wa Bonde la Liuni ambao ulianzishwa muda mrefu lakini haujakamilika Likonde na kufanya ukarabati katika kilimo cha umwagiliaji Kijiji cha Nambecha?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Vita Kawawa, Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, maeneo ambayo Mheshimiwa Mbunge ameyatamka ni maeneo ambayo yapo katika mkakati wa Wizara kuhakikisha tunawezesha wakulima wa eneo hilo kulima kupitia kilimo cha umwagiliaji. Nimtoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba tutatuma wataalam wetu kwenda kuyaangalia maeneo hayo ili baadaye tuingie katika mpango wetu wa Serikali kuhakikisha kwamba tunakarabati skimu hizo.

Name

Iddi Kassim Iddi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Msalala

Primary Question

MHE. DKT. DAVID M. DAVID aliuliza: - Je, ni lini Serikali itasaidia kukarabati mifereji ya Marwa, Kwasita, Magereza, Gunge na Kirua katika Bonde la Mto Pangani?

Supplementary Question 4

MHE. IDDI K. IDDI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Mradi wa Chela ni mradi wa muda mrefu sana. Swali langu, je, ni lini sasa Serikali itakwenda kuweka fedha za ukarabati wa Mradi wa Umwagiliaji wa Chela pia na kukarabati mitaro ile na miundombinu kwa ujumla?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Iddi Kassim, Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hili naomba niliseme katika Bunge letu Tukufu kwamba, kwa kutambua kuna umuhimu mkubwa sana wa ukarabati wa miradi mbalimbali ya umwagiliaji; Wizara tumeiagiza Tume ya Maendeleo ya Umwagiliaji kuhakikisha inaipitia miradi yote nchi nzima kwa ajili ya kufanya tathmini na kujua status zake, tujue ipi inahitaji ukarabati mkubwa, ipi inahitaji ukarabati mdogo, ipi inatakiwa tuanze upya, lengo letu ni kuhakikisha miradi hii inafanya kazi.

Mheshimiwa Spika, kwa Mheshimiwa Mbunge nimwaahidi tu kwamba, katika hayo ambayo ameyasema pia tutaingiza katika mpango wetu ili tuhakikishe kwamba wananchi wake wananufaika na kilimo cha umwagiliaji.