Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Lucy John Sabu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. VINCENT P. MBOGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Soko katika Mji Mdogo wa Chala Wilayani Nkasi?

Supplementary Question 1

MHE. LUCY J. SABU: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa fursa hii, naomba kuuliza swali dogo la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itajenga soko la kisasa katika Wilaya ya Bariadi, Mkoani Simiyu ukizingatia Wilaya ya Bariadi ni Makao Makuu ya Mkoa wa Simiyu? Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Lucy Sabu, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tulishatoa maelekezo katika Halmashauri zote ambazo zinahitaji miradi ya kimkakati kuandika maandiko ili Ofisi ya Rais TAMISEMI tutafute fedha na kuileta katika hayo maeneo ili waweze kupata masoko ya kisasa ikiwemo hiyo Halmashauri ya Bariadi. Kwa hiyo, niwape tu hilo agizo kwamba walete hayo maandiko yao nasi tutayafanyia kazi. Ahsante sana.

Name

Vincent Paul Mbogo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nkasi Kusini

Primary Question

MHE. VINCENT P. MBOGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Soko katika Mji Mdogo wa Chala Wilayani Nkasi?

Supplementary Question 2

MHE. VINCENT P. MBOGO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, katika swali langu la msingi naomba kuongeza swali moja la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Tarafa ya Wampembe ina Kata Nne ambazo kuna biashara kubwa sana ya samaki ambayo inafanyika na nchi jirani hakuna soko. Je, ni lini Serikali itawajengea soko kwa ajili ya biashara zao za samaki Kata ya Wampembe? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Vincent Paul Mbogo, Mbunge wa Jimbo la Nkasi Kusini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, mimi ningemuomba Mheshimiwa Mbunge, kwanza tumalize soko la Chala halafu baada ya hapo kama vipaumbele vinavyofuatia, maana yake linalofuatia ni hilo eneo ambalo amelifikisha hapa Mheshimiwa Mbunge. Ahsante sana.

Name

Ndaisaba George Ruhoro

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ngara

Primary Question

MHE. VINCENT P. MBOGO aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Soko katika Mji Mdogo wa Chala Wilayani Nkasi?

Supplementary Question 3

MHE. NDAISABA G. RUHORO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Naomba sasa kuuliza swali la nyongeza.

Je, ni lini Serikali itaanza kuwajengea wananchi wa Jimbo la Ngara soko la kimkakati eneo la Kabanga? Ahsante.

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Ndaisaba George, Mbunge wa Jimbo la Ngara kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ninatambua kwamba Halmashauri ya Ngara imeshaleta andiko lake na wataalam katika Ofisi ya Rais, TAMISEMI wapo kulipitia ili tutafute fedha kwa ajili ya ujenzi. Kwa hiyo, niwaagize tu wafanye haraka kwenye mapitio ya hilo andiko na kutafuta fedha ili eneo hilo la Mheshimiwa Mbunge alilolianisha waweze kujengewa soko. Ahsante sana. (Makofi)