Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Edwin Enosy Swalle

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lupembe

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kupeleka Watumishi, Vifaa Tiba na Tendanishi kwenye Vituo vya Afya na Zahanati katika Jimbo la Lupembe?

Supplementary Question 1

MHE. EDWIN E. SWALLE: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa majibu mazuri ya Serikali. Jimbo la Lupembe, wananchi wamejenga zahanati nyingi sana. Tunazo zahanati mpya za Welela, Havanga, Lima, Tagamenda, Ikondo na kila mahali. Pia kuna vituo vya afya kama Ikondo, Mtwango, ni vipya kabisa: Ni nini mpango wa Serikali kupeleka watumishi wa afya kwenye vituo hivi ili vianze kufanya kazi mapema? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Kwa kuwa afya ni pamoja na kuwa na magari ya wagonjwa, Serikali ina mpango gani wa kupeleka gari la wagonjwa kwa maana ya ambulance katika Jimbo la Lupembe?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nawapongeza wananchi wa Jimbo la Lupembe kwa kujitolea nguvu zao na kujenga zahanati na kuanza ujenzi wa vituo vya afya. Nampongeza sana Mheshimiwa Mbunge kwa ufuatiliaji mzuri. Kwa hakika Serikali hii ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan imeendelea kuleta fedha katika Wilaya ya Njombe na katika Jimbo la Lupembe.

Mheshimiwa Spika, hivi sasa tunaongelea Kituo cha Afya cha Ikuna kinaendelea kujengwa, lakini pia zahanati zimepata fedha shilingi milioni 50 kwa ajili ya ukamilishaji. Vile vile watumishi wataendelea kuletwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Njombe kwa maana ya watumishi wa kada za afya kama ambavyo zilishapelekwa 72, lakini ajira nyingine zinazofuata watatoa kipaumbele katika Halmashauri hii.

Mheshimiwa Spika, siku tatu zilizopita Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan amegawa magari ya wagonjwa 199 katika halmashauri zetu zote na magari ya usimamizi wa huduma za afya na Halmashauri ya Wilaya ya Njombe Jimbo la Lupembe limepata gari hilo. Kwa hiyo, nikuhakikishie kwamba gari lipo njiani linafika wakati wowote kwa ajili ya kuhudumia wananchi.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kupeleka Watumishi, Vifaa Tiba na Tendanishi kwenye Vituo vya Afya na Zahanati katika Jimbo la Lupembe?

Supplementary Question 2

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, je, upi mkakati wa Serikali kuhakikisha kwamba watumishi wanapelekwa katika Kituo cha Afya cha Songwe katika Kata ya Nanyara ambacho kina upungufu mkubwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, mkakati wa Serikali, kwanza tumeainisha maeneo yenye upungufu mkubwa wa watumishi na ajira zinazofuata tutahakikisha kituo hiki kinapatiwa watumishi wa sekta ya afya, ahsante.

Name

Deus Clement Sangu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kwela

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kupeleka Watumishi, Vifaa Tiba na Tendanishi kwenye Vituo vya Afya na Zahanati katika Jimbo la Lupembe?

Supplementary Question 3

MHE. DEUS C. SANGU: Mheshimiwa Spika, nashukuru. Serikali imejenga vituo vya afya vitatu katika Kata ya Kaegesa, Kipeta na Kaoze: Je, ni upi mkakati wa kupeleka vifaatiba na watumishi katika vituo hivyo vya afya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, Serikali katika mwaka wa fedha huu imetenga jumla ya shilingi bilioni 69.9 kwa ajili ya ununuzi wa vifaatiba kwa ajili ya kupeleka kwenye vituo vya afya. Mwaka wa fedha uliopita, halmashauri zote zilipata vifaatiba. Kwa hiyo nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba zoezi hili ni endelevu na tutapeleka vifaa tiba kwa ajili ya vituo hivi vya afya lakini na pia tutapeleka watumishi kwa ajili ya kuhakikisha kwamba vituo hivi vinaanza kutoa huduma, ahsante.

Name

Yahaya Omary Massare

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Manyoni Magharibi

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kupeleka Watumishi, Vifaa Tiba na Tendanishi kwenye Vituo vya Afya na Zahanati katika Jimbo la Lupembe?

Supplementary Question 4

MHE. YAHAYA O. MASSARE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Je, ni lini Serikali itapeleka vifaatiba katiba Halmashauri ya Itigi ambapo tumejenga zahanati na vituo vya afya lakini vifaa tiba na watumishi ni haba?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Katika mwaka wa fedha uliopita, Halmashauri ya Itigi pia imepata vifaatiba, pia mwaka huu wa fedha, bajeti hii ambayo inatekelezwa, tutapeleka vifaatiba na fursa za ajira zitakapojitokeza, tutahakikisha tunatoa kipaumbele kwa watumishi ili Halmashauri ya Itigi iweze kupata huduma bora za afya. Ahsante.

Name

Anastazia James Wambura

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kupeleka Watumishi, Vifaa Tiba na Tendanishi kwenye Vituo vya Afya na Zahanati katika Jimbo la Lupembe?

Supplementary Question 5

MHE. ANASTAZIA J. WAMBURA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Mkoa wa Mtwara una zahanati sita ambazo hazijaanza kutoa huduma kutokana na kutokupata mgao wa watumishi katika ajira mpya: Je, ni lini Serikali itapeleka watumishi ili kusudi zahanati hizi ziweze kuanza kufanya kazi?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, tulishatoa maelekezo kwa Wakurugenzi na Makatibu Tawala wa Mikoa kwamba pale zahanati zinapokamilika, hatuna sababu ya kuziacha zisianze kutoa huduma za awali. Natumia fursa hii kwanza kumkumbusha Mkurugenzi wa Halmashauri hiyo na Katibu Tawala wa Mkoa wa Mtwara kwamba watumie utaratibu wa kuwa-reallocate watumishi ndani ya halmashauri ili angalau huduma za OPD zianze kwenye zahanati hizi.

Mheshimiwa Spika, namhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba tutatoa kipaumbele kwenye ajira zinazofuata ili watumishi wafike katika zahanati hizi. Ahsante.

Name

Joseph Kasheku Musukuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Geita

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kupeleka Watumishi, Vifaa Tiba na Tendanishi kwenye Vituo vya Afya na Zahanati katika Jimbo la Lupembe?

Supplementary Question 6

MHE. JOSEPH K. MUSUKUMA: Mheshimiwa Spika, ni lini Serikali itaanza ujenzi wa kituo cha afya Nkome?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ni kweli Zahanati ya Nkome inazalisha wakina mama wengi sana kwa mwezi na inahudumia wananchi wengi kwa ujumla wake. Pia, nimhakikishie kwamba tayari imekwishaingizwa kwenye orodha ya vituo vya afya ambavyo vinatafutiwa fedha kwa ajili ya kujengwa ili iweze kutoa huduma kwa ngazi ya kituo cha afya. Ahsante.

Name

Zuberi Mohamedi Kuchauka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Liwale

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kupeleka Watumishi, Vifaa Tiba na Tendanishi kwenye Vituo vya Afya na Zahanati katika Jimbo la Lupembe?

Supplementary Question 7

MHE. ZUBERI M. KUCHAUKA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa nafasi. Pamoja na kwamba Serikali imekuwa ikipeleka vifaa tiba kwenye baadhi ya zahanati zetu na vituo vya afya lakini bado kuna tatizo la vifaa tiba hivyo kukosa watumiaji (wataalamu). Nini kauli ya Serikali kupeleka watumishi kwenye hizi zahanati na vituo vya afya ambavyo vina vifaa tiba?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba tumekuwa na upungufu wa wataalamu wa kutumia baadhi ya vifaa tiba ambavyo vimepelekwa katika vituo vyetu. Kwa kulitambua hilo, Serikali imeandaa utaratibu wa mafunzo ya muda mfupi wa miezi mitatu mpaka miezi sita kwa wataalamu wa mionzi na wataalamu wengine ili tuweze kuziba hili gap la wataalamu wa kutumia vifaa hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, wataalamu hao tayari wamekwishaingia katika ngazi ya masomo na tunahakikisha mapema iwezekanavyo wakihitimu wanapelekwa kwenye vituo vyetu ili waweze kutumia vifaa hivyo ipasavyo. Ahsante.

Name

Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kupeleka Watumishi, Vifaa Tiba na Tendanishi kwenye Vituo vya Afya na Zahanati katika Jimbo la Lupembe?

Supplementary Question 8

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kituo cha Afya cha Chikolopola kina mtumishi mmoja tu. Lakini pia Zahanati ya Mputeni na zahanati ya Makanyama haina watumishi kabisa. Ni lini Serikali itapeleka watumishi katika maeneo haya?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba, kama ambavyo katika mwaka wa fedha uliopita halmashauri hii ya Masasi vijijini walipata watumishi. Nafahamu kwamba bado wanaupungufu mkubwa katika Kituo cha Afya cha Chikolopola. Nimhakikishie kwamba tutatoa kipaumbele kwenye ajira zitakazofuata ili waweze kupata watumishi wa kutosha katika eneo hilo. ahsante.

Name

Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kupeleka Watumishi, Vifaa Tiba na Tendanishi kwenye Vituo vya Afya na Zahanati katika Jimbo la Lupembe?

Supplementary Question 9

MHE. TARIMBA G. ABBAS: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana. Pale Jimbo la Kinondoni, kwa kupitia fedha za mfuko wa Jimbo tumejenga jengo la mionzi kwa maana ya (Radiology).

Je, Serikali iko tayari sasa kutupatia vifaa tiba kama vile x-ray, ultrasound pamoja na wafanyakazi ili kituo kile kiweze kuanza kazi? Nakushukuru

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Kwanza nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa kutenga fedha kupitia Mfuko wa Jimbo na kujenga Jengo la mionzi na nafahamu amekuwa akifuatilia mara kwa mara. Nimhakikishie kwamba Serikali itashirikiana na halmashauri ya Kinondoni kupitia mapato ya ndani ili waweze kununua baadhi vifaa tiba ambavyo viko ndani ya uwezo wao kama ultrasound, wakati Serikali kuu inaangalia uwezekano wa kupata fedha kwa ajili ya x-ray ili wananchi wapate huduma bora, ahsante.

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. EDWIN E. SWALLE aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kupeleka Watumishi, Vifaa Tiba na Tendanishi kwenye Vituo vya Afya na Zahanati katika Jimbo la Lupembe?

Supplementary Question 10

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa mujibu wa taarifa ya CAG iliyotoka mwezi Machi, 2023. Halmashauri 106 zilikuwa na idara na vitengo ambavyo vinaongozwa na watumishi 747 wasiokuwa na sifa. Matokeo yake ufanisi ni duni. Ni lini Serikali itaenda kuziba nafasi hizo?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ni kweli kwamba kuna baadhi ya halmshauri ambazo zina wakuu wa idara na vitengo ambao hawajathibitishwa. Kwa sababu hizo Serikali inafanya utaratibu ikiwemo upekuzi lakini pia kuwatafuta wenye sifa za kuweza kujaza nafasi hizo ili waweze kutekeleza majukumu yao ipasavyo.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba Serikali iko kazini. Tunafanya vetting ya wataalamu wenye sifa hizo ili waende kujaza nafasi za wakuu wa idara na waweze kutoa huduma ipasavyo. Ahsante.