Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Michael Constantino Mwakamo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Vijijini

Primary Question

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO aliuliza:- Je, lini Serikali itawasilisha Bungeni Muswada wa Sheria ya Wazee?

Supplementary Question 1

MHE. MICHAEL C. MWAKAMO: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa majibu ya Serikali, lakini naomba niulize maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza: Kwa kuwa Muswada huu una muda mrefu takribani miaka 20 sasa na lilikuwa ni tegemeo la wazee wengi kupokea sheria hii: Je, Serikali inaweza ikatueleza vikwazo vilivyosababisha kuichelewesha sheria hii kutungwa? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Kwa kuwa wazee hawa wamelitumikia Taifa hili kwa muda mrefu: Je, Serikali ina mipango gani ya haraka ya kuwahudumia wazee hawa ili waweze kupata huduma zinazostahili kwenye ofisi za Serikali wakati wakiwa wanasubiri sheria hiyo? (Makofi)

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUMU: Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ili Muswada ukamilike na ufikishwe Bungeni kuna taratibu na sheria na miongozo ambayo iliyowekwa na sasa inafanyiwa kazi. Mara baada ya kumalizika Muswada huo, utawasilishwa Bungeni kwa wakati. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inajali sana wazee; na katika Sheria mpya ambayo imetungwa tumeweka kipengele cha ulinzi na usalama kwa wazee. Kwa hiyo, kupitia Bunge lako tukufu naelekeza kwamba taasisi zote za Serikali na binafsi ziweze kuweka utaratibu maalum wa kuwasaidia wazee katika huduma za jamii pale wanapofika sehemu hizo, kwani Serikali inawapenda wazee na wazee ni tunu ya Taifa letu, ahsante. (Makofi)