Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Saashisha Elinikyo Mafuwe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hai

Primary Question

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE K.n.y. MHE. JULIANA D. MASABURI aliuliza:- Je, lini Serikali itakipandisha hadhi Chuo cha Maendeleo ya Jamii Musoma ili kiweze kutoa shahada?

Supplementary Question 1

MHE. SAASHISHA E. MAFUWE: Mheshimiwa Spika, ahsante, na kwa niaba ya Mheshimiwa Juliana Didas Masaburi, nashukuru sana kwa majibu ya Serikali. Pamoja na hayo majibu ya Serikali, katika chuo hiki, wanafunzi wanapata taabu sana maeneo ya kuishi ili kupata taaluma pale. Ni upi mpango wa Serikali kuhakikisha inajenga mabweni kwenye eneo hili na chuo hiki ili wanafunzi wapate sehemu ya kukaa?

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Katika Kanda ya Kaskazini, mikoa yote hakuna Chuo cha Maendeleo ya Jamii; je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Chuo cha Maendeleo ya Jamii katika Jimbo la Hai ambapo tayari tumeshapanga eneo la kujenga lipo tayari?

Name

Mwanaidi Ali Khamis

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAENDELEO YA JAMII, JINSIA, WANAWAKE NA MAKUNDI MAALUM: Mheshimiwa Spika, ahsante, napenda kujibu maswali ya nyongeza mawili kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, tunatambua kuwa umuhimu wa miundombinu ya utoshelevu katika kujenga mabweni ya wanafunzi katika vyuo, Serikali itaendelea kutenga rasilimali fedha ili kuweza kuendelea kujenga mabweni hayo katika kila sehemu ya vyuo ili wanafunzi wapate kuwa na maendeleo mazuri na kuwa karibu na kuishi maeneo ya shule.

Mheshimiwa Spika, swali lake la pili, ushauri wake tumeupokea na tunawapongeza Wanajimbo la Hai kwa kuwa na kiwanja cha kujenga Chuo cha Maendeleo ya Jamii. Wameona umuhimu wa vyuo hivi. Wizara itaendelea kutenga fedha kadiri bajeti itakavyoruhusu, katika mwaka wa fedha 2025, kuona vipi Chuo hiki tunakijenga ili wananchi waweze kuwa na chuo katika Mkoa wao, ahsante. (Makofi)