Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Cecilia Daniel Paresso

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CECILIA D. PARESSO aliuliza:- Je, kwa nini Serikali ilivunja Mradi wa Maji wa KAVIWASU katika Mji wa Karatu bila kuwashirikisha wananchi?

Supplementary Question 1

MHE. CECILIA D. PARESSO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali madogo mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, mchakato wa uvunjwaji wa Bodi hii haukishirisha wananchi na hapa mmekiri mlienda kwenye Mamlaka ya Serikali, kwa wawakilishi wa wananchi lakini hamkufika kwa wananchi. Je, ni lini mtafika kwa wananchi na kuwapa sababu za kwa nini mlivunja mradi huu? (Makofi)

Swali la pili, mmeeleza kwamba baada ya chombo hiki kuundwa kuna ufanisi wa maji, naomba niwaambie Wizara hakuna ufanisi wowote matokeo yake tumerudi kwenye adha kubwa ya ukosefu wa maji katika Mji wa Karatu. Ni lini na kwa haraka mtarekebisha tatizo hili ili wananchi waweze kupata maji kwa uhakika? (Makofi)

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Cecilia Paresso, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, naomba nirudie tena Mheshimiwa Waziri yeye mweyewe, Jumaa Hamidu Aweso na Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo walishirikiana na Waheshimiwa Madiwani waliweza kushirikisha wananchi. Kama wananchi hawakupata taarifa wote basi kuendelea kutoa elimu ni moja ya jukumu la Wizara, kwa hiyo tutaendelea kutoa elimu kwa sababu dhamira ya Wizara ni njema kabisa, lengo la kuunganisha hivi vyombo ni kupunguza mzigo wa gharama za bei kwa wananchi na kabla ya kuviunganisha mwananchi aliweza kulipia unit ya maji shilingi 2,000 na baada ya kuviunganisha tunamshukuru sana Mheshimiwa Waziri alihakikisha bei zimeshuka na sasa hivi ni shilingi 1,300.

Mheshimiwa Spika, kuonesha ufanisi mkubwa wa mradi wa huduma ya maji, tayari Wizara, Karatu tumeiangalia kwa jicho la kipekee kabisa na tayari kazi zinaendelea, tutahakikisha huduma ya maji Karatu wataendelea kuboreshewa lengo ni kupata maji safi na salama bombani yakiwa ya kutosha.

SPIKA: Mheshimiwa Naibu Waziri ahsante sana kwa majibu yako kwa maswali ya Waheshimiwa Wabunge. Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo, Mheshimiwa Mwanakhamis Kassim Said, Mbunge wa Magomeni, sasa aulize swali lake.