Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Suma Ikenda Fyandomo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SUMA I. FYANDOMO aliuliza:- Je, lini Wilaya ya Rungwe italetewa Mwenyekiti wa Baraza la Ardhi?

Supplementary Question 1

MHE. SUMA I. FYANDOMO: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, ninaipongeza sana Serikali ya Awamu ya Sita ya Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan kwamba ni sikivu sana, kwa sababu niliuliza hili swali la imelitekeleza. Nina maswali mawili ya nyongeza.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuyaelimisha Mabaraza ya Kata ili yasitoe hukumu kwenye mashauri ya ardhi?
Swali langu la pili, katika Wilaya ya Chunya hakuna kabisa Baraza la Ardhi, ukizingatia wananchi wa Chunya wanatoka Kambikatoto, Kipambawe, Mafieko, Bintimanyanga, Matwiga, Luhanga, Ifumbo na Shoga wanakwenda kushtaki mashauri yao kwenye Jiji la Mbeya.

Je, ni lini Serikali itawaepushia shida hiyo wananchi wa Wilaya ya Chunya?

Name

Jerry William Silaa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ukonga

Answer

WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI: Mheshimiwa Spika, Mabaraza ya Ardhi ya Kata yameanzishwa chini ya Sheria Sura ya 206 na kupitia Bunge lako Tukufu kwenye Marekebisho ya Sheria Namba 3 ya Mwaka 2021 Mabaraza haya yalipunguziwa nguvu ya kimaamuzi na yanapaswa kufanya usuluhishi ndani ya siku 30 baada ya shauri kufikishwa.

Mheshimiwa Spika, tuliongea na Waandishi wa Habari lakini naomba kutumia Bunge lako Tukufu kuwatangazia wananchi wote kwamba Mabaraza ya Ardhi ya Kata nguvu yake ya kisheria ni kufanya usuluhishi ndani ya siku 30 tokea shauri lifikishwe mbele yake. Baada ya hapo kama usuluhishi utashindwa kufanyika mashauri yawasilishwe kwenye Mabaraza ya Ardhi ya Wilaya. Ninaomba tena kupitia Bunge lako, Wakurugenzi wa Halmashauri maana Mabaraza ya Ardhi ya Kata yanasimamiwa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI na Wakurugenzi wa Halmashauri wanasimamia kwa niaba yake, Waendelee kusimamia mabaraza haya ili wananchi waendelee kupata haki zao. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, ni kweli kati ya Mabaraza ya Wilaya zote 139 ni Mabaraza 94 tu ndiyo yenye Wenyeviti wa Baraza la Wilaya. Tayari ofisi yangu imeendelea kufanya mawasiliano ya kuomba vibali vya ajiri kwa ajili ya kupata ajira ya kuajiri Wenyeviti wengine 45, lakini kwenye maeneo yote ikiwemo Wilaya ya Chunya kwenye maeneo aliyotaja Mheshimiwa Mbunge ikiwemo Maeneo ya Bintimanyanga na maeneo ya Shoga tunaendelea kutoa maelezo kwa Msajaili wa Baraza la Ardhi la Wilaya kutumia Wenyeviti wa Mabaraza ya Ardhi ya Wilaya ya jirani kwenda kwenye mabaraza haya kwenda kusikilza mashauri mpaka pale Serikali itakapokamilisha Wenyeviti kwenye Mabaraza ya Wilaya zote, ninakushukuru. (Makofi)