Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER L. MIDIMU aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga Kituo cha Afya katika Kata za Luguru na Sawida Wilayani Itilima?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Spika, ninakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwanza kabisa nimpongeze Naibu Waziri kwa majibu mazuri.

Mheshimiwa Spika, nimpongeze Mheshimiwa Rais kwa kuendelea kujenga Vituo vya Afya na Hospitali za Wilaya tena nzuri za kisasa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Kata ya Luguru ni kata yenye idadi ya watu wengi, kituo cha afya kikijengwa Kata ya Luguru kitahudumia Kata ya Sawida na Kata ya Kinamweli. Je, Serikali ina mpango gani wa kuharakisha ujenzi wa kituo cha afya Kata Luguru?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; vituo vya afya vya Mkoa wa Simiyu na hospitali za wilaya tuna upungufu wa vifaa tiba na Watumishi.

Je, ni lini Serikali itatuletea vifaa tiba vya kutosha na watumishi wa kutosha? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, Mheshimiwa Esther Lukago Midimu, kwamba tayari Serikali ilishamwelekeza Katibu Tawala wa Mkoa na Mganga Mkuu wa Mkoa wa Simiyu pia na Mkurugenzi wa Halmashauri ya Itilima kuwasilisha maombi ya ujenzi wa Kituo cha Afya cha Luguru ili tuweze kuandaa fedha kwa ajili ya kwenda kuanza ujenzi katika kituo hicho cha afya.

Mheshimiwa Spika, pili, Serikali imeendelea kupeleka vifaa tiba pia imeendelea kuajiri watumishi wa sekta ya afya na kuwapeleka katika Halmashauri zetu kote na Halmashauri ya Wilaya ya Itilima ni moja ya Halmashauri ambazo tayari zimepelekewa zaidi ya shilingi bilioni moja ya fedha kwa ajili ya vifaa tiba. Pia imeshapelekewa Watumishi wa Sekta ya Afya na nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kila mara ambapo fedha itapatikana itaendelea kupelekwa kwa ajili ya vifaa tiba, lakini pia Watumishi wataendelea kupelekwa Itilima, ahsante.