Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Ally Juma Makoa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kondoa Mjini

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka gari la wagonjwa katika Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Kondoa?

Supplementary Question 1

MHE. ALLY J. MAKOA: Mheshimiwa Spika, pamoja na kwamba nimeuliza swali ni lini, nilitegemea ningeambiwa mwezi ujao maana yake imekuwa ni story ya muda mrefu; nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, je, vituo vya afya vilivyopo Kata ya Suruke, Kingale pamoja na sasa tunajenga Kolo vitakuwa miongoni mwa orodha ya mgao huo?

Mheshimiwa Spika, la pili; kumekuwa na hofu kubwa kwa wananchi wa Kondoa wanaopata huduma katika Hospitali ya Halmashauri ya Mji hasa wanapopata kesi ya kufanyiwa operation, sasa pamoja na ahadi hiyo ya kupatiwa ambulance wamekuwa wakipata rufaa kwa tabu sana kuletwa Hospitali ya Mkoa lakini hata hivyo, wananchi wamekuwa na mashaka makubwa.

Je, Serikali itakuwa tayari lini kwenda kujiridhisha na uwezo wa madaktari pamoja na vifaatiba vilivyopo katika Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Kondoa? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ally Juma Makoa, Mbunge wa Jimbo la Kondoa Mjini, kama ifuatayo: -

Mheshimiwa Spika, fedha ambazo zinakwenda kununua magari haya ya wagonjwa 195 ambazo zinatoka kwenye mpango wa UVIKO-19 zitakwenda kununua magari haya na yatapelekwa kwenye Halmashauri zote 184 lakini ni maamuzi ya halmashauri kuona uhitaji mkubwa katika ngazi ya hospitali au katika kituo cha afya ambako gari litapelekwa. Kwa hiyo, ni maamuzi ya halmashauri kuona kipaumbele kwa wakati huo gari hilo litakwenda kwenye kituo cha afya au kwenye hospitali ya halmashauri.

Mheshimiwa Spika, kwa sababu tunapanga kununua magari haya na UNICEF kuna uwezekano mkubwa magari ya wagonjwa yakaongezeka zaidi ya 195. Kwa hiyo, tunauhakika vituo vyetu pia ambavyo vimekamilika vitapata magari ya wagonjwa.

Mheshimiwa Spika, kuhusiana na uhakika wa huduma katika Hospitali ya Mji wa Kondoa kwa maana ya uwezo wa madaktari na vifaatiba; madaktari wote wanaoajiriwa kwa ngazi zao wanakuwa wamesajiliwa na Serikali imejiridhisha juu ya uwezo wao wa kutoa huduma. Kwa hiyo, niwatoe hofu wananchi wa Mji wa Kondoa kwamba madaktari waliopo pale ambao wamepelekwa na Serikali wana uwezo unaotakiwa, wanatoa huduma ambazo zinatakiwa, lakini kama kuna mapungufu Serikali tutafuatilia na kuchukua hatua katika maeneo hayo. Ahsante. (Makofi)

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka gari la wagonjwa katika Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Kondoa?

Supplementary Question 2

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Katika Jimbo la Kilwa Kaskazini lenye hospitali moja na vituo vya afya vitatu kumekuwa na changamoto kubwa ya uwepo wa gari la wagonjwa. Je, Serikali ina mpango gani wa kupeleka magari ya wagonjwa ya kutosha ili kutoa huduma kwa wagonjwa wa dharura? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Francis Kumba Ndulane, Mbunge wa Jimbo la Kilwa Kaskazini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba kati ya magari hayo 195 plus Halmashauri ya Kilwa ni miongoni mwa halmashauri ambazo zitapata magari hayo na tutafanya tathimini kuangalia umbali wa vituo hivi lakini na idadi ya wananchi wanao hudumiwa ili ikiwezekana tuongeze magari kwenye Wilaya hiyo ya Kilwa. Ahsante.

Name

Halima James Mdee

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka gari la wagonjwa katika Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Kondoa?

Supplementary Question 3

MHE. HALIMA J. MDEE: Mheshimiwa Spika, nashukuru, Halmashauri ya Kinondoni ina majimbo mawili; Jimbo la Kinondoni na Jimbo la Kawe lakini Jimbo la Kawe tumejenga hospitali kubwa sana ambayo itatumika na Bagamoyo na Kawe, lakini vilevile referral’s zinaweza zikaenda Mloganzila. Sasa kutokana na ukubwa na upekee wa hospitali ya Kawe iliyokuwa Mabwepande hamzani kwamba Jimbo la Kawe linatakiwa lipate gari kwa upekee? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Halima James Mdee, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba tunafahamu hospitali kubwa ya Mabwepande katika Halmashauri ya Manispaa ya Kinondoni imejengwa, imekamilika itaanza kutoa huduma wakati wowote hivi sasa tumeanza na huduma za OPD na ni lazima tutapeleka gari la wagonjwa pale kulingana na ukubwa wa hospitali ile na Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Kawe pia amekuwa akikumbushia sana kuhusiana na umuhimu wa gari hilo. (Kicheko)

Kwa hiyo, nikupongeze sana Mheshimiwa Mdee kwa kushirikiana sana na Mheshimiwa Mbunge wa Jimbo la Kawe, ahsante.

Name

Tarimba Gulam Abbas

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kinondoni

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka gari la wagonjwa katika Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Kondoa?

Supplementary Question 4

MHE. TARIMBA G. ABBAS: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi; pale kwenye Kata ya Tandale Jimbo la Kinondoni kuna kituo cha afya ambacho kinahudumia zaidi ya watu 1,000 kwa siku na Mheshimiwa Naibu Waziri anafahamu, lakini kituo kile hakina gari la wagonjwa nafahamu mtaleta magari hayo ambayo mmeyataja lakini kwa Kinondoni mahitaji ni makubwa.

Je, Serikali haioni umuhimu wa kuipelekea gari kituo cha Afya cha Tandale ili kuweza kuondoa matatizo hayo? Ahsante.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Abbas Tarimba, Mbunge wa Jimbo la Kinondoni kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimejibu kwenye majibu yangu ya msingi tunakwenda kununua magari 195 lakini tutaongeza magari mengine kwa sababu kwa utaratibu ambao tunanunua magari haya kupitia UNICEF tutapata saving ambayo tuna uhakika magari yataongezeka na kigezo cha kugawa magari haya itakuwa ni vitu vyenye idadi kubwa ya wagonjwa kama Tandale na maeneo mengine, lakini umbali kutoka kituo kile kwenda hospitali ya halmashauri.

Kwa hiyo, nimhakikishiwa Mheshimiwa Mbunge tutafanya tathimini ya uhitaji huo na pale ambapo vigezo vitafikiwa tutaleta gari pia katika vituo hivyo. Ahsante.

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka gari la wagonjwa katika Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Kondoa?

Supplementary Question 5

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa nafasi pamoja na mpango mzuri wa Serikali kupeleka magari ya wagonjwa kila halmashauri.

SPIKA: Taja kituo cha afya ama hospitali na uliza swali lako.

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Spika, na kwa kuwa Wilaya ya Hanang kuna upande wa juu ambapo kuna kata nane na tumejenga vituo viwili vya afya vya Basutu na Hirbadaw, je, Serikali ipo tayari kutuletea gari la pili?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Engineer Hhyuma, Mbunge wa Jimbo la Hanang kama ifuatavyo; nimhakikishie kwamba tufanya tathimini na kuona uhitaji wa magari katika vituo hivyo na tutapeleka kadri ya upatikanaji wa magari hayo. Ahsante.

Name

Boniphace Nyangindu Butondo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kishapu

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka gari la wagonjwa katika Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Kondoa?

Supplementary Question 6

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa kunipa na mimi nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Halmashauri ya Wilaya ya Kishapu inajumla ya vituo vya afya nane lakini vituo vitatu tu ambavyo vinamagari haya ambulance na jiografia ya wilaya yangu ni ngumu kweli kweli. Nilikuwa nataka niombe pamoja na mpango wa wizara kuhakikisha kwamba inatoa..

SPIKA: Mheshimiwa Butondo uliza swali unataka gari iletwe/ipelekwe wapi?

MHE. BONIPHACE N. BUTONDO: Mheshimiwa Spika, ninaomba kuletewa gari na lipelekwe katika Tarafa ya Mondo ambayo itaongeza uwepo wa magari katika Tarafa hiyo.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza Mheshimiwa Boniphace Butondo, Mbunge wa Jimbo la Kishapu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimuhakikishie kwamba katika tathimini ambayo tutafanya kubaini uhitaji wa magari ya wagonjwa na vigezo kama vinafikiwa tutafanya pia katika vituo vya afya ya Kishapu ili tuweze kufanya maamuzi hayo, ahsante.

Name

Hawa Subira Mwaifunga

Sex

Male

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka gari la wagonjwa katika Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Kondoa?

Supplementary Question 7

MHE. HAWA S. MWAIFUNGA: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kuniona; Hospitali ya Rufaa ya Kitete ina changamoto kubwa sana ya magari ya kupebea wagonjwa. Je, katika magari hayo 195 hospitali hii ipo katika list?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, ahsante sana, naomba kujibu swali la nyongeza Mheshimiwa Hawa Mwaifunga, Mbunge wa Viti Maalumu kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, magari haya 195 ni magari ambayo yatanunuliwa na Ofisi ya Rais TAMISEMI kwa ajili ya vituo vya huduma za afya za msingi kwa maana zahanati, vituo vya afya na hospitali za halmashauri, lakini nikuhakikishie kwamba kupitia Wizara ya Afya Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan ametenga fedha kununua magari mengi kwa ajili ya wagonjwa kwenye hospitali za rufaa za mikoa kanda na hospitali ya Taifa. Kwa hiyo hospitali ya Kitete ni sehemu ya wizara ya afya na magari hayo pia yapo kwa ajili ya hospitali hiyo kupitia wizaza ya afya, ahsante.

Name

Kilumbe Shabani Ng'enda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kigoma Mjini

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka gari la wagonjwa katika Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Kondoa?

Supplementary Question 8

MHE. KILUMBE S. NG'ENDA: Mheshimiwa Spika, mimi najua nimo katika mgao wa magari, lakini nilichotaka kujua kwa sababu Wabunge tumekuwa tukipigia kelele sana suala hili la magari. Je, ofisi yako itaandaa utaratibu ili kila Mbunge apokee gari hii kwenye eneo lake? (Makofi/Kicheko)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza Mheshimiwa Kirumbe Ng’enda, Mbunge wa Jimbo la Kigoma Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, magari haya yanakwenda kwenye Halmashauri zetu ambako sisi Waheshimiwa Wabunge tunatoka huko, tunatambua kuna halmashauri zenye jimbo zaidi ya moja, consideration itafanyika kuona idadi ya vituo katika jimbo husika lakini pia uhitaji wa magari ya wagonjwa na tutapeleka hivyo. Ahsante.

Name

Nicholaus George Ngassa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Igunga

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka gari la wagonjwa katika Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Kondoa?

Supplementary Question 9

MHE. NICHOLAUS G. NGASSA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Kituo cha Afya Igulubi kilichopo kwenye Jimbo la Igunga kimejengwa kwa milioni 500 na Serikali ya Chama cha Mapinduzi na kituo kipya hakina gari la wagonjwa. Je, nini kauli ya Serikali kuhusu hilo? Ahsante sana.

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza Mheshimiwa Nicholaus Ngassa, Mbunge wa Jimbo la Igunga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kituo hiki cha afya ambacho kimekamilika ni sehemu ya vituo ambavyo vinahitaji magari ya wagonjwa, lakini safari ni hatua tutafanya tathimini kuona vigezo hivyo na kama itatimiza vigezo basi itapata gari la wagonjwa.

Name

Hassan Zidadu Kungu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduru Kaskazini

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka gari la wagonjwa katika Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Kondoa?

Supplementary Question 10

MHE. HASSAN Z. KUNGU: Mheshimiwa Spika, kituo cha afya cha Matembanga kiko kilometa 80 kutoka hospitali ya Wilaya ya Tunduru Mjini na tayari tunaishukuru Serikali majengo ya upasuaji yamekamilika na vifaa vyote vimekamilika na tumeanza upasuaji hapa majizi na kituo kile hakina gari la wagonjwa.

Je, Serikali ina mpango gani wa kupatia gari la wagonjwa kituo kile?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza Mheshimiwa Kungu, Mbunge wa Jimbo la Tunduru Kaskazini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie kwamba tunafanya tathimini ya vituo vya afya ambavyo vimekamilika na vinatoa huduma za upasuaji kikiwemo kituo hiki na kuona uwezekano wa kupata gari la wagonjwa, lakini itategemea idadi ya magari ambayo tunayo na kipaumbele cha halmashauri kulingana na vigezo vya kitaalamu vya uhitaji wa magari ya wagonjwa.

Name

Munde Abdallah Tambwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka gari la wagonjwa katika Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Kondoa?

Supplementary Question 11

MHE. MUNDE T. ABDALLAH: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa zahanati ya Town Clinic ya Tabora Manispaa ambayo Naibu Waziri anaifahamu vizuri ina wagonjwa wengi na haina gari la wagonjwa; ni lini sasa Serikali itatuletea gari la wagonjwa kwa ajili ya kusaidia kata hizo 30 ambazo inaitumia?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza Mheshimiwa Munde Abdallah, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, tunatambua kwamba zahanati hii inahudumia wananchi wengi, lakini kigezo cha gari ya gari la wagonjwa ni kuwa kituo cha afya au hospitali ya halmashauri, lakini kwa sababu ya upekee wa zahanati hii tutafanya tathimini na kuona uwezekano wa kupeleka gari baada ya kujiridhisha na vigezo ambavyo vinatakiwa, ahsante.

Name

Shabani Hamisi Taletale

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Morogoro Kusini Mashariki

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka gari la wagonjwa katika Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Kondoa?

Supplementary Question 12

MHE. HAMISI S. TALETALE: Mheshimiwa Spika, kwa kuwa kituo cha afya cha Kata ya Mkuyuni kinachangamoto ya gari la wagonjwa; je, na sisi lini tutaletewa gari la wagonjwa?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Hamisi Taletale, Mbunge wa Jimbo la Morogoro Kusini Mashariki kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, magari haya yatakayo kuja yatapelekwa kwenye vituo vyetu vikiwemo vya Morogoro ambavyo vitakidhi vigezo. Kwa hiyo nimuhakikishie Mheshimiwa Mbunge tutawasiliana tuone namna ya kufanya tathimini kwenye kituo hiki kama kinakidhi vigezo hivyo, ahsante.

Name

Stanslaus Shing'oma Mabula

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nyamagana

Primary Question

MHE. ALLY J. MAKOA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itapeleka gari la wagonjwa katika Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Kondoa?

Supplementary Question 13

MHE. STANSLAUS S. MABULA: Mheshimiwa Spika, ahsante; ni lini Serikali itakuwa tayari kupeleka gari la wagonjwa Kituo cha Afya Bulale kulingana na Geografia yake ilivyo mbali? (Makofi)

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza Mheshimiwa Stanslaus Mabula, Mbunge wa Jimbo la Nyamagana, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Kituo cha Afya cha Bulale nakifahamu tulishafanya ziara pale, kiko mbali na kinahudumiwa wananchi wengi naomba Mheshimiwa Mbunge shirikiana na halmashauri kuweka kipaumbele cha kituo au hospitali ambayo tunahitaji kupata gari ili ikipatikana tupeleke hapo, lakini baadaye tutaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya kupeleka magari katika kituo hicho pia.