Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hamida Mohamedi Abdallah

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Lindi Mjini

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha Kilimo katika eneo la Ngongo Mkoani Lindi ambapo tayari hekari 120 zimetengwa kwa ajili hiyo?

Supplementary Question 1

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, kwanza nishukuru kwa majibu ya Serikali, lakini ningependa kujua katika eneo la Ngongo, sisi Manispaa tulishatoa hekari 120; nini msukumo wa Serikali kuhakikisha kwamba fedha zinapatikana na kuwawezesha Chuo Kikuu cha Dar es salaam kuja kujenga Chuo cha Kilimo campus ya Lindi? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Hamida Mohamed Abdalaah Mbunge wa Lindi Mjini kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nachukuwa fursa hii kumpongeza sana Mheshimiwa Mbunge amekuwa akilifuatilia sana jambo hili na hii si mara ya kwanza kuliulizia. Sisi kama Wizara ya Kilimo tumefanya mawasiliano na wenzetu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia jambo hili limeshaanza na ndani ya muda mfupi ujao wataendelea na taratibu za kuhakikisha kwamba mchakato huu unakamilika, ili ujenzi uanze mara moja.

Kwa hiyo, nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge ya kwamba Serikali inafanya kazi kwa pamoja na wenzetu Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia chini ya Chuo Kikuu cha Dar es salaam wako tayari kuendelea na mchakato huu na hatua zimefikia sehemu nzuri.

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha Kilimo katika eneo la Ngongo Mkoani Lindi ambapo tayari hekari 120 zimetengwa kwa ajili hiyo?

Supplementary Question 2

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Mwenyekiti nashukuru kwa kuniona na kunipa nafasi.

Rais Samia Suluhu Hassan ameonesha nia ya kuimarisha na kuboresha kilimo na kiasi kwamba tumeongeza bajeti yetu ya kilimo; je, Serikali iko tayari kwa kushirikiana na Vyuo vya Kilimo kutusaidia sisi wananchi huko vijijini kwa kutuletea wale wanafunzi ambao wanakuwa kwenye mafunzo ya vitendo ili waje kushirikiana na wananchi katika kuimarisha nakuboresha kilimo?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Cosato Chumi, Mbunge kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumekuwa na programu hiyo ya kuwahusisha wale vijana ambao wako chini ya Ofisi ya Waziri Mkuu kupitia programu ya uhanagenzi na tutaendelea kuifanya hivyo kuhakikisha kwamba wanafikia maeneo mengi zaidi lengo hapa ni kuhakikisha kwamba wanawafikia wakulima wengi zaidi, na wakulima wanapata elimu ya kilimo bora ili kuongeza tija na kufikia malengo ambayo tumejiwekea ya kukuza Sekta ya Kilimo kwa asilimia 10 ifikapo mwaka 2030.

Name

Khadija Hassan Aboud

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha Kilimo katika eneo la Ngongo Mkoani Lindi ambapo tayari hekari 120 zimetengwa kwa ajili hiyo?

Supplementary Question 3

MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, kwanza naipongeza Serikali katika kuhamasisha kilimo na huduma za ugani suala langu Serikali kupitia Wizara ya Kilimo imenunua pikipiki kwa ajili ya Maafisa Ugani, lakini bado pikipiki hayo hayajagawiwa ili kuepusha uchakavu, ni lini Serikali itayagawa pikipiki hizo kwa walengwa ili yakafanya kazi kwa wakulima? Ahsante. (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Khadija Hassan Aboud kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli bajeti ya Wizara ya Kilimo na hasa katika eneo la huduma za ugani, imeongezeka kutoka shilingi milioni 600 mpaka shilingi bilioni 15 kwa ndani ya miaka miwili kazi kubwa ambayo Mheshimiwa Rais ameifanya na ndani ya bajeti hiyo pia na sisi tulinunua vifaa kwa maana ya pikipiki, kwa ajili ya kuwapatia Maafisa Ugani.

Nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba zilikuwepo na taratibu za ndani za kuzifuata ambazo zimekamilika na kuanzia jana zoezi la usambazaji pikipiki limeanza, jana Mkoa wa Dodoma wamechukuwa pikipiki 264, leo Singida watachukuwa 161 na kesho kutwa Tabora na maeneo mengine wataendelea kuzichukuwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo Mheshimiwa Mbunge nikuondoe hofu pikipiki zile ndani ya muda mrefu zitaondoka eneo hilo ili ziweze kuwafikia Maafisa Ugani.

Name

Nusrat Shaaban Hanje

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. HAMIDA M. ABDALLAH aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha Kilimo katika eneo la Ngongo Mkoani Lindi ambapo tayari hekari 120 zimetengwa kwa ajili hiyo?

Supplementary Question 4

MHE. NUSRAT S. HANJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kuwa Kanda ya Kati hususani Mkoa wa Singida na Dodoma ni miongoni mwa mikoa ambayo ni ya kimkakati hususani kwenye zao la alizeti ukiwemo mkoa wa kwako Mheshimiwa Naibu Waziri.

Je, Serikali haioni haja ya kuhakikisha kwamba sasa tunapata Chuo cha Kilimo kwenye Kanda ya Kati kuhakikisha kwamba fedha zinazotengwa na Serikali zinakuwa na tija?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Nusrat Hanje, Mbunge wa Viti Maaalum kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Vyuo vyetu vya kilimo vimegawanya katika kanda na Kanda ya Kati pia yenyewe inapata huduma kupitia vyuo hivi, lakini sambamba na hizo tunazo taasisi mbalimbali ambazo zinafanya kazi katika Mkoa wetu wa Dodoma pamoja na Singida ambazo lengo lake kuu ni kuhakikisha kwamba tunawajengea uwezo wakulima wetu kulima kilimo cha alizeti kwa tija.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge ya kwamba tumezingatia sana ikolojia ya Dodoma na Singida na tumeweka nguvu ya kutosha kuhakikisha wakulima wetu wanapata elimu ya kutosha juu ya kilimo cha alizeti na mwisho wa siku tuondoe tatizo la upungufu wa mafuta ambalo tunalo hapa nchini.