Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Latifa Khamis Juwakali

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LATIFA KHAMIS JUWAKALI aliuza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha Bodi ya Mitaji kwa wahitimu wa elimu ya juu kama ilivyo kwa Bodi ya Mikopo ya wanafunzi wa Elimu ya Juu?

Supplementary Question 1

MHE. LATIFA KHAMIS JUWAKALI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Nikushukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri ya Serikali nilikuwa na swali moja la nyongeza.

Je, Serikali inatoa tamko gani sasa kuhakikisha kila muhitimu anapewa kipaumbele anaporudi au anapomaliza au anapohitimu katika elimu yake ya elimu ya juu ili aweze kupata mikopo katika halmashauri waweze kujiajiri na ili kuweza kurejesha mikopo kwa wakati? Ahsante. (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Latifa Khamis Juwakali, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu kwenye majibu yangu ya msingi kwamba halmashauri zetu zimekuwa zikitenga asilimia 10 ya mapato ya ndani kwa ajili ya kutoa mikopo ambayo ni kwa ratio ya 4:4:2 asilimia nne kwa vijana, asilimia nne kwa wanawake na asilimia mbili kwa watu wenye ulemavu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mikopo ile inatolewa kwa mujibu wa sheria na zipo kanuni ambazo tumekwenda kuzifanyia marekebisho mwanzoni ilikuwa vijana ni lazima wawe vijana 10 katika kikundi lakini hivi sasa ni vijana tano tu wanaunda kikundi wawe na shughuli maalum ya kufanya na mikopo ile wanaweza kupata.

Kwa hiyo, sisi kauli kama Serikali ni kuwahakikishia tu vijana kwamba wajiunge kwenye vikundi ambavyo ni vya ujasiriamali na sasa hivi haihitajiki kwamba iwe tayari umeshaanza kufanya shughuli hata kama una wazo tu lakufanyakazi fulani au shughuli fulani mikopo ile unaweza kupata.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kauli yetu kwa vijana hawa wajiunge kwenye vikundi na kutumia kanuni zile zilizopo kuhakikisha kwamba halmashauri zetu zinawapata mikopo hii ili waweze kukidhi maisha yao, lakini waweze kurejesha mikopo ile elimu ya juu waliyoichukua. Nakushukuru sana.

Name

Rashid Abdallah Shangazi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mlalo

Primary Question

MHE. LATIFA KHAMIS JUWAKALI aliuza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha Bodi ya Mitaji kwa wahitimu wa elimu ya juu kama ilivyo kwa Bodi ya Mikopo ya wanafunzi wa Elimu ya Juu?

Supplementary Question 2

MHE. RASHID A. SHANGAZI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, majibu ya Serikali yamejikita kwenye mfuko mmoja tu ambao ni asilimia 10 ya mapato ya halmashauri, lakini Serikali inamifuko zaidi ya 45 ya kuondoa umaskini.

Je, haioni sasa ni wakati muafaka wa kuanza kuwakopesha wanafunzi kwa kutumia dhamana ya vyeti vyao ambavyo wamevipata vya kitaaluma ili kuondoa hili tatizo? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu swali dogo la Mheshimiwa Rashid Shangazi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza Mheshimiwa Shangazi amezungumza suala la vyeti na mwanafunzi akishapata cheti haitwi tena mwanafunzi anaitwa muhitimu. Kwa hiyo, naomba nilifanyie marekebisho hapo namna gani wahitimu wetu sasa wanaweza kutumia vyeti vyao kuweza ku-access hiyo mikopo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba tuchukue ushauri wa Mheshimiwa Shangazi, twende tukaufanyie kazi tuufanyie na tathimini ya kina kwasababu sasa ni suala mtambuka si suala la Wizara ya Elimu peke yake hapa itaingia Wizara Fedha, lakini Wizara ya Vijana na Wizara nyingine ambazo zinashughulika na mambo ya vijana na mikopo kwa ujumla.

Kwa hiyo, naomba tuchukue ushauri wa Mheshimiwa Mbunge twende tukaufanyie tathimini ya kina ili tuweze kuangalia je, hivi vyeti vinaweza vikatumika kama bond ya kuwapatia mikopo vijana wetu. Nakushukuru sana.

Name

Ester Amos Bulaya

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LATIFA KHAMIS JUWAKALI aliuza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha Bodi ya Mitaji kwa wahitimu wa elimu ya juu kama ilivyo kwa Bodi ya Mikopo ya wanafunzi wa Elimu ya Juu?

Supplementary Question 3

MHE. ESTER A. BULAYA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kuna baadhi ya wizara kama Wizara ya Kilimo mbali ya kwamba kuna mikopo kwenye halmashauri na mifuko mingine wao wamekuwa wakitoa motisha kwa vijana ambao wana invest kwenye kilimo. Unapozungumzia tatizo la ajira kwa graduate ni kwenye Wizara yako.

Je, hamuoni kwamba kama wizara mnapaswa kuwa na fungu maalum kwa ajili ya kuwasaidia vijana graduate wanaoenda kujiajiri wenyewe kama Wizara kama ambavyo mnavyofanya kwenye Bodi ya Mikopo na maeneo mengine? Ahsante.

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante, naomba kujibu swali dogo la Mheshimiwa Ester Bulaya kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu kwenye swali la Mheshimiwa Shangazi, sisi Wizara ya Elimu jukumu letu ni kuhakikisha kwamba tunaratibu utaratibu wa utoaji wa elimu nchini. Wanafunzi wakishahitimu linakuwa si jukumu la Wizara ya Elimu, lakini ni jukumu la Serikali.

Kwa hiyo, kwa vile umezungumza habari ya motisha kwa vijana wetu wanaokamilisha masomo yao na kuangalia namna gani tunaweza tukaratibu taratibu zao za kuweza kujiajiri au kupata ajira, tuchukue ushauri huo, lakini Mheshimiwa Ester nadhani baada tu ya kikao hiki kuna umuhimu wa kukaa. Kwa sababu sasa hivi tunafanya mapitio ya mitaala yetu huenda kuna kitu kinakosekana nadhani na wewe unaweza kuwa na input na Mungu akipenda tarehe 13 tutakuwa na kongamano kubwa sana pale Dar es Salaam la kuhakikisha kwamba mitaala yetu ile inakwenda kujibu maswali ya Waheshimiwa Wabunge juu ya suala hili la ajira pamoja na suala la umahiri kwenye masomo yetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naomba tuubebe ushauri wako twende tukaufanyie kazi kwa kushirikiana na Wizara ya Kilimo tuweze kuangalia namna gani bora ya kuweza kulifanyia kazi jambo hili. Nakushukuru sana.

Name

Ritta Enespher Kabati

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. LATIFA KHAMIS JUWAKALI aliuza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha Bodi ya Mitaji kwa wahitimu wa elimu ya juu kama ilivyo kwa Bodi ya Mikopo ya wanafunzi wa Elimu ya Juu?

Supplementary Question 4

MHE. DKT. RITTA E. KABATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ili niulize swali dogo la nyongeza.

Kwa kuwa sasa hivi kuna malalamiko mengi sana kwa baadhi ya wanafunzi wanufaika wa hii mikopo ya vyuo vikuu wamekuwa wakimaliza madeni yao lakini bado mfumo unaendelea kukata madeni yao.

Je, Serikali inasemaje kuhusiana na hawa wanafunzi ambao bado wanaendelea kukatwa wakati wameshamaliza madeni?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naomba kujibu swali dogo la Mheshimiwa Kabati kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza niweze kumpongeza Mheshimiwa Kabati kwa ufuatiliaji wa karibu wa jambo hili nadhani ameshakuja ofisini si chini ya mara moja/mara mbili kwa ajili ya kufuatilia jambo hili.

Mheshimiwa Kabati kwanza nikuondoe wasiwasi, sasa hivi utaratibu wetu kila mnufaika wa mikopo ile ana akaunti yake na katika akaunti ile inakuwa inaonyesha kwamba kiasi gani amelipa na kiasi gani kilichobaki kwamba hajalipa. Kwa mantiki hiyo iwapo kama kuna wanufaika ambao wanaendelea kukatwa wakati wameshamaliza ile mikopo, tuna dawati letu la malalamiko la kuonesha kwamba yeye amekamilisha, lakini bado anaendelea kulipwa au anaendelea kukatwa kwenye mishahara au kwenye mafao yake mengine.

Kwa hiyo, hili suala tunaendelea kulifanyia kwa sababu ni suala la kimfumo, lakini nikuondoe wasiwasi wale wote ambao wamekatwa kwa namna moja au nyingine tumekuwa tukizirudisha fedha hizi baada tu ya kuleta hayo malalamiko ili kuweza kuwarudishia wao wenyewe. Nakushukuru.