Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Francis Kumba Ndulane

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kilwa Kaskazini

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza: - Mheshimiwa Spika, je, ni lini mradi mkubwa wa maji toka Mto Rufiji utaanza kutekelezwa ili kuwaondolea wananchi wa Kata 23 za Wilaya ya Kilwa tatizo la ukosefu wa maji safi na salama ambalo limekuwa likiwakabili kwa muda mrefu?

Supplementary Question 1

MHE. FRANCIS K. NDULANE: Mheshimiwa Spika, kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Kwanza nitoe shukrani kwa Serikali ambapo jana tuliweza kusaini Mkataba wa kuboresha huduma ya maji katika Mji wa Kilwa Masoko wenye thamani ya shilingi bilioni 81. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini niulize swali la nyongeza sasa, kumekuwa na hali chechefu katika utekelezaji wa miradi ambayo inahudumiwa na Mfuko wa Maji ikiwemo mradi ambao unatekelezwa katika Kijiji cha Kinjumbi kutokana na mlolongo mrefu wa malipo.

Je, Serikali ina utaratibu gani ambao umeupanga ili kupunguza mlolongo mrefu wa malipo ili miradi hii inayotekelezwa kwa mfuko wa maji iweze kuhudumiwa kwa ufanisi?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Ndulane, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, awali ya yote nipende kupokea shukrani kwa uzinduzi wa miradi ya maji ya miji 28, kwenye hili tumpongeze sana Mheshimiwa Rais na tumshukuru na tumuombee kwa sababu kazi aliyoifanya ni kazi iliyotukuka. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini kuhusiana na malipo ya Mfuko wa Maji kuwa na mlolongo mrefu, Mheshimiwa Mbunge unaelewa hapo nyuma kulikuwa na matumizi mabovu ya fedha katika hali ya udhibiti ilipaswa Wizara kuweka taratibu zote hizo, lakini tunaendelea kuziboresha kuhakikisha kwamba udhibiti utaendelea lakini pia fedha itatoka ndani ya wakati.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza: - Mheshimiwa Spika, je, ni lini mradi mkubwa wa maji toka Mto Rufiji utaanza kutekelezwa ili kuwaondolea wananchi wa Kata 23 za Wilaya ya Kilwa tatizo la ukosefu wa maji safi na salama ambalo limekuwa likiwakabili kwa muda mrefu?

Supplementary Question 2

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana na nakuomba kwa ruhusa ya kiti chako nitangulize shukrani kwa Mheshimiwa Rais Samia Suluhu Hassan kwa tamko lake la jana kwamba sasa mradi wa Mwanga, Same, Korogwe unakwenda kuanza tumepata usingizi watu wa Kilimanjaro.

Mheshimiwa Spika, baada ya shukrani hizo naomba nimuulize sasa Naibu Waziri; je, ni lini mradi mkubwa wa chanzo cha maji cha Ziwa Chala ambao utawapatia maji wananchi wa Holili, Ngoyoni, Chala na wengine tambarare ya Rombo utaanza?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Shally Raymond kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, ni kweli Mradi wa Ziwa Chala unatarajiwa sana kuona kwamba unakwenda kutatua tatizo la maji, lakini Ziwa Chala tukitaka kutumia mradi ule maana yake ni mradi wa ku-pump, ni mradi ambao utaleta gharama kubwa na matokeo yake wananchi watalipa huduma kwa gharama kubwa.

Mheshimiwa Spika, lakini tayari kuna miradi mitatu pale ya gravity inayoendelea kujengwa katika Mji wa Rombo na tunatarajia miradi hii ikija kukamilika kwa sababu ni miradi ya miserereko itakuwa ni miradi rafiki kwa wananchi na tatizo la maji linakwenda kukoma.

Name

Abdallah Dadi Chikota

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nanyamba

Primary Question

MHE. FRANCIS K. NDULANE aliuliza: - Mheshimiwa Spika, je, ni lini mradi mkubwa wa maji toka Mto Rufiji utaanza kutekelezwa ili kuwaondolea wananchi wa Kata 23 za Wilaya ya Kilwa tatizo la ukosefu wa maji safi na salama ambalo limekuwa likiwakabili kwa muda mrefu?

Supplementary Question 3

MHE. ABDALLAH D. CHIKOTA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi, nami niungane na wenzangu kuipongeza Serikali kwa kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa Mradi wa Makonde ambao mkataba umesainiwa jana. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, lakini ningependa kujua sasa kuna mradi mkubwa wa kutoa maji mto Ruvuma, Kijiji cha Mahechini kupeleka Manispaa ya Mtwara mradi ambao utanufaisha Jimbo la Nanyamba Mtwara Vijijini na Manispaa ya Mtwara; je, mradi huu utaanza kutekelezwa lini?

Name

Maryprisca Winfred Mahundi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Abdallah Chikota kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, hakika nimeelewa anayeshukuru anaomba tena, tayari ni jana tu Mheshimiwa Rais ameweza kufanya jambo zito sana la kuona Mradi wa Makonde unaenda kufanyiwa kazi, lakini mradi huu wa Mto Ruvuma nao ni moja ya mikakati ya Wizara tunakwenda kuhakikisha maji ya Mto Ruvuma yanakwenda kutatua matatizo ya maeneo yote ambayo utayapitia. Mara tutakapopata fedha tutaingia kwenye mradi huu.