Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI K.n.y. MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga mabweni pamoja na miundombinu mingine katika Chuo cha VETA Kitangali?

Supplementary Question 1

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza maswali ya nyongeza. Kwanza; kwa kuwa changamoto ya miundombinu katika Chuo cha VETA cha Kitangali ni kubwa sana; na kwa kuwa wanafunzi wanaotoka sehemu hiyo wanatoka katika maeneo mbalimbali vijijini. Je, ni lini sasa Serikali itakamilisha mradi huo na kujenga mabweni kwa ajili ya wanafunzi wanaotoka sehemu mbalimbali ikiwepo wanaotoka kwenye Jimbo la Mheshimiwa Maimuma Mtanda?

Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili; kwa kuwa changamoto ya vijana wanaomaliza Sekondari na Shule za Msingi imekuwa ni kubwa, vijana wengi wanamaliza shule na wengi wanatarajia sasa kwenda kwenye vyuo hivi vya VETA kupata elimu. Je, Serikali ina mkakati gani sasa wa kuhakikisha kwenye hivi Vyuo vya VETA vyote nchi nzima wanaweka miundombinu na mabweni ili watoto mbalimbali wanaomaliza shule kutoka vijijini waweze kwenda kwenye Vyuo vya VETA na kupata mafunzo na ujuzi wa mbalimbali? Ahsante sana. (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI YA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyoeleza kwenye jibu langu la msingi kwamba katika mwaka wa fedha 2018/2019, Serikali iliweza kupeleka fedha kwa ajili ya ujenzi wa baadhi ya mbiundombinu katika chuo hiki; na naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge katika mwaka wa fedha ujao, tutahakikisha kwamba maeneo haya ambayo ameyataja hasahasa katika hiki Chuo cha Kitangali kupitia mapato ya ndani ya VETA tutakwenda kuongeza miundombinu katika eneo hili ikiwemo pamoja na mabweni.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwenye swali lake la pili, ni kweli tukiri kwamba tunajenga VETA katika wilaya zote Tanzania, lakini focus yetu kwanza ilikuwa ni ujenzi wa miundombinu ya vyuo hivi na tumeweza sasa kukamilisha karibu katika Wilaya 77 nchini. Kuna wilaya chache ambazo bado hatujazifikia, tunaamini katika kipindi kijacho kwanza tutakwenda kukamilisha kwenye wilaya hizi ambazo hazina Vyuo vya VETA, lakini vilevile kuhakikisha kwamba haya maeneo ambayo yana upungufu wa mabweni nao vilevile tunaweza kuwafikia kwa ajili ya kukamilisha miundombinu hii ili wanafunzi wetu, vijana wetu, waweze kupata mafunzo katika maeneo hayo.

Mheshimwa Naibu Spika, nakushukuru sana.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI K.n.y. MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga mabweni pamoja na miundombinu mingine katika Chuo cha VETA Kitangali?

Supplementary Question 2

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ili niweze kuuliza swali la nyongeza. Kwa kuwa sera ya Serikali ni kuwa na VETA kila wilaya. Je, ni lini Serikali itajenga Chuo cha VETA Wilaya ya Maswa? (Makofi)

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Midimu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyokwishaeleza kwenye majibu ya swali la msingi, kwamba Sera yetu kama Serikali ni kuhakikisha kwamba tunakuwa na Chuo cha VETA katika kila wilaya nchini ikiwemo na Wilaya ya Maswa. Namwomba tu Mheshimiwa Mbunge awe na subira katika hiki ambacho Serikali tunaendelea kutafuta fedha na tunaamini katika mwaka ujao wa fedha tutaweza kuzifikia baadhi ya wilaya lakini tutaipa kipaumbele vilevile Wilaya ya Maswa; kuhakikisha kwamba miongoni mwa vile vyuo vichache ambavyo vitapata fedha basi tuweze kutekeleza mradi huo katika Wilaya ya Maswa. Nashukuru sana.

Name

Dr. Charles Stephen Kimei

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vunjo

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI K.n.y. MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga mabweni pamoja na miundombinu mingine katika Chuo cha VETA Kitangali?

Supplementary Question 3

MHE. DKT. CHARLES S. KIMEI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru sana kwa kunipa fursa hii ili niweze kuuliza swali dogo la nyongeza. Je, Serikali ina mpango gani wa kukarabati Chuo cha Ufundi Stadi cha Mangaria kilicho kwenye Kata ya Mamba Kaskazini na kukipa vifaa vya kufundishia?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Kimei kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kama nilivyokwishaeleza awali kwamba Serikali bado tunaendelea na mchakato wa utafutaji wa fedha; kwanza tuweze kufanya ujenzi kwenye wilaya ambazo hazina hivi vyuo. Hata hivyo, nimwondoe wasiwasi Mheshimiwa Dkt. Kimei, kwa vile ametaja suala la ukarabati katika Chuo hicho cha Mamba, nitamwomba tu baada ya kikao hiki cha leo tuweze kuonana baadaye ili kwanza tuweze kutuma timu yetu ya wataalam kwenda kule Mamba, iende ikafanye tathmini ya kina, tuweze kujua gharama za ukarabati ukaohitajika pale ni kiasi gani ili tuweze kuingiza kwenye mipango yetu na tukipata tuweze kukipa kipaumbele cha ukarabati chuo hiki. Nakushukuru sana.

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI K.n.y. MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga mabweni pamoja na miundombinu mingine katika Chuo cha VETA Kitangali?

Supplementary Question 4

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru. Mwaka 2014 tuliweza kubadilisha Sheria ya Skill Development Levy ambapo zilikuwa asilimia nne zote ziende VETA kwa ajili ya kuboresha ujuzi na miundombinu ya VETA, lakini 2014 tulibadilisha kwa sababu by then tulikuwa hatuna VETA nyingi na sasa hivi Serikali imejenga VETA nyingi sana.

Je, Serikali sasa haioni ni wakati muafaka warudishe ile sheria tuibadilishe, hizi asilimia mbili ambazo zilipelekwa Bodi ya Mikopo kwa ajili kukopesha wanafunzi wa elimu ya juu ziweze kurudishwa VETA; zitumike kama ilivyokuwa imedhamiriwa awali?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la Mheshimiwa Esther Matiko, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nishukuru kwa swali lake la msingi na kuona umuhimu wa taaluma hii ya VETA katika nchi yetu. Hata hivyo, kwanza nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Esther kwanza Serikali imekuwa ikipeleka ruzuku kwenye vyuo hivi, ruzuku zile za uendeshaji, ndiyo kwa maana unaona hata zile ada zake ziko chini sana kwa wanafunzi wa kutwa ni Sh.60,000 na kwa wale wa mabweni ni Sh.120,000. Kwa vile Mheshimiwa amezungumza habari ya sheria kwamba tuirejeshe hapa Bungeni ili tuweze kuirekebisha ili basi ile asilimia nne iweze kwenda kuongeza nguvu kwenye eneo lile la VETA.

Mheshimiwa Naibu Spika, naomba tubebe ushauri wake Mheshimiwa Matiko twende tukaufanyie kazi, tufanye tathmini ya kina, tukiona kuna haja ya kuleta hiyo sheria hapa ili tuweze kubadilisha, tuweze kufanya hivyo. Nakushukuru sana.

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. MARIAM N. KISANGI K.n.y. MHE. MAIMUNA S. MTANDA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga mabweni pamoja na miundombinu mingine katika Chuo cha VETA Kitangali?

Supplementary Question 5

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Chuo cha VETA Mikumi ni chuo ambacho kilijengwa na Irish people kwa ajili ya Halmashauri ya Wilaya ya Kilosa na kwa nia njema kabisa Chuo kile tuliikabidhi Serikali. Tangu tumeikabidhi Serikali hakuna jitihada zozote za kujenga ama kukarabati miundombinu ya chuo kile hasa ukizingatia kwamba hali yake ni mbaya na hakina mabweni. Sasa nini kauli ya Serikali kuhusiana na ujenzi wa miundombinu hasa mabweni katika Chuo cha VETA?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Naomba kujibu swali dogo la nyongeza la kaka yangu Mheshimiwa Londo, Mbunge wa Mikumi, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Londo kwa ufuatiliaji wa karibu wa chuo hiki, siyo mara moja wala mara mbili tumeshawahi kukutana.

Mheshimwa Naibu Spika, naomba Mheshimiwa Londo aridhie baada ya kikao hiki tuweze kukutana ili kuangalia kitu gani cha kufanya na vilevile tuweze kutuma timu kwenye eneo hili kwa ajili ya kufanya tathmini kama tutakavyofanya kwa Mheshimiwa Kimei, tuweze kufanya vilevile na kwake, kuangalia thamani ya ukarabati pamoja na uongezaji wa miundombinu kwenye eneo lile ili tuweze kutekeleza kwa wakati.

Mheshimwa Naibu Spika, nakushukuru sana.