Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Neema Kichiki Lugangira

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA K.n.y. MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Jengo jipya la Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo?

Supplementary Question 1

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA: Mheshimiwa Naibu Spika, suala la ucheleweshaji sio la Biharamulo, kwa sababu Biharamulo walishawasilisha Mkoani na Mkoani wanaleta moja kwa moja TAMISEMI. Jengo la Halmashauri ya Biharamulo, liko kwenye miradi ya kimkakati ya Mkoa wa Kagera.

Mheshimiwa Naibu Spika, ningependa kuuliza maswali mawili ya nyongeza kwa niaba ya Mheshimiwa Engineer Ezra Chiwelesa. Swali la kwanza, maombi yalikuwa ni bilioni 3.4 lakini Serikali imetenga bilioni 2.7 kwa mwaka wa fedha 2023/2024 lakini kwa uchumi wa Biharamulo haitaweza kupata hiyo milioni 700 inayosalia.

Je, Serikali ina mpango gani waku-top up kiasi hicho cha fedha tukifika wakati huo?

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa kuwa Serikali tayari imeshaweka commitment na ahadi kwamba itatenga hiyo bajeti ya bilioni 2.7; je, bado kuna haja tena ya kuandika maombi haya au hakuna haja?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Neema Lugangira, Mbunge wa Viti Maalum ambayo ameuliza kwa niaba ya Mheshimiwa Engineer Ezra John Chiwelesa kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, jambo la msingi bila kujali vimechelewa wapi ni suala la kwamba jengo la utawala la Halmashauri litatengwa kwenye mwaka wa fedha 2023/2024. Lakini kiasi ambacho kimeombwa ni Bilioni 3.475 lakini mpango wa Serikali tumefanya standardization ya majengo yetu yote ya halmashauri ili kuepukana na variation ya majengo ambayo yamekuwa yanajengwa kwenye Halmashauri zetu.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa hiyo, kwa sasa Halmashauri zote zitakuwa na mchoro mmoja na kila halmashauri itapata bilioni 2.7, kwa hiyo hatuna haja ya kuongeza fedha hiyo, hiyo ndiyo fedha kulingana na mchoro huo ili kuhakikisha kwamba tunakuwa na standardization. Lakini pale ambapo tutalazimika kuwa na variation ya mchoro kulingana na mazingira, basi tutaona namna ya kufanya.

Name

Muharami Shabani Mkenge

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. NEEMA K. LUGANGIRA K.n.y. MHE. ENG. EZRA J. CHIWELESA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Jengo jipya la Halmashauri ya Wilaya ya Biharamulo?

Supplementary Question 2

MHE. MUHARAMI S. MKENGE: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kumuuliza swali la nyongeza Mheshimiwa Waziri. Halmashauri ya Wilaya ya Bagamoyo, wafanyakazi wake wanakaa sehemu tofauti tofauti, kutokana na uchakavu wa jengo, na jengo kuwa na nafasi ndogo. Je, ni lini Serikali itatujengea jengo jipya na maombi tulishapeleka?

Name

Dr. Festo John Dugange

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Wanging'ombe

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DKT. FESTO J. DUGANGE): Mheshimiwa Naibu Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Muharami, Mbunge wa Jimbo la Bagamoyo kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Naibu Spika, Serikali inaendelea kujenga majengo haya ya utawala, mpaka sasa takribani jumla ya Bilioni 224.5 zimetumika kwa majengo ya Halmashauri 95, tunafahamu Bagamoyo mlileta maombi hayo, nikuhakikishie kwamba tunaendelea kutafuta fedha na baada ya hapo tutaanza shughuli za ujenzi wa jengo la Halmashauri. Ahsante. (Makofi)