Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Christine Gabriel Ishengoma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CHRISTINE G. ISHENGOMA aliuliza: - Je, Serikali ina mpango gani wa kufungua Ubalozi wa Tanzania nchini Pakistan?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. CHRISTINE G. ISHENGOMA: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana, nashukuru sana kwa majibu mazuri ya Serikali, lakini hata hivyo nina swali la nyongeza.

Kwa kuwa nchi yetu imefaidika sana kutokana na balozi mbalimbali ambazo tumefungua nchi mbalimbali na hasa kwenye uwekezaji, biashara, pamoja na utalii na hasa kwenye biashara ya mazao ya kilimo.

Je, nchi hii ya Pakistan kwa sababu wana ubalozi wao hapa nchini tunashirikianaje pamoja na nchi hii?

Name

Amber. Mbarouk Nassor Mbarouk

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Nominated

Answer

NAIBU WAZIRI WA MAMBO YA NJE NA USHIRIKIANO WA AFRIKA MASHARIKI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana; naomba kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Dkt. Christine Gabriel Ishengoma, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Naibu Spika, ingawa Tanzania haina ubalozi nchini Pakistan lakini tunawakilishwa na ubalozi wetu ambao upo Abu Dhabi UAE. Kwa hiyo, mahusiano ya nchi zetu mbili hizi ni makubwa na tumekuwa tukishirikiana katika masuala mbalimbali hasa ya kibiashara ambapo nchi yetu imekuwa ikisafirisha kwenda Pakistan bidhaa kama pamba, chai na madini ya vito kama vile Tanzanite pamoja na nafaka kama vile maharage. Lakini pia kutoka Pakistan tumekuwa pia tukishirikiana nao na tumekuwa tuki-import bidhaa za dawa za binadamu pamoja na dawa za viwanda vya nguo na nafaka. Nashukuru sana.