Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Hassan Seleman Mtenga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mtwara Mjini

Primary Question

MHE. HASSAN S. MTENGA aliuliza: - Je, ni lini Serikali itajenga Daraja la Mto Ruvuma ili kufungua Shughuli za Kibiashara?

Supplementary Question 1

MHE. HASSAN S. MTENGA: Mheshimiwa Spika, kwanza nishukuru kwa majibu mazuri, lakini nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza; naomba commitment ya Serikali, ni lini ujenzi huo wa daraja utaanza?

Mheshimiwa Spika, swali la pili; ni lini Mheshimiwa Waziri tutaongozana nami ili twende kwenye eneo husika ambalo tunalizungumzia la kujenga daraja apate ufumbuzi zaidi?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI NA UCHUKUZI (MHE. FREDY A. MWAKIBETE): Mheshimiwa Spika, ahsante. Napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Hassan Selemani Mtenga kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, la kwanza anataka commitment ya Serikali kwamba, lini ujenzi huu hasa utaanza katika daraja hili la Mto Ruvuma, eneo la Kilambo. Nimpongeze Mheshimiwa Mbunge kwa namna ambavyo amekuwa akifuatilia suala zima la daraja hili katika Mto huu Ruvuma, sababu tunatambua kwamba, daraja hili ni kiungo muhimu kati ya Nchi yetu ya Tanzania na Nchi ya Msumbiji. Kwa maana hiyo, mazungumzo ambayo tutayaanza hivi karibuni pamoja na Nchi ya Msumbiji kupitia Wizara yetu ya Mambo ya Nje, tutafanya commitment kupitia pia Wakala wetu wa Barabara Nchini (TANROADS) ili tuanze sasa mchakato mzima wa kuanza kujenga daraja hili, maana daraja hili lazima lijengwe na nchi mbili kati ya Tanzania na Msumbiji.

Mheshimiwa Spika, swali la pili, Kwenda naye kuona hili eneo. Nataka nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge, mara baada ya Bunge hili la Bajeti, mwezi Julai nitakuwa na ziara, hivyo nitakwenda kwa Mheshimiwa Mbunge kutembelea eneo hili. (Makofi)